-
Sehemu ya 1: Mafundisho ya KikristoTengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
-
-
mtakuwa kama Mungu, mkijua mema na mabaya.’”—Mwa. 3:2-5.
• “Shetani akamjibu Yehova: ‘Ngozi kwa ngozi. Mtu atatoa kila kitu alicho nacho ili aokoe uhai wake.’”—Ayu. 2:4.
23. Unaweza kuthibitishaje kwamba mashtaka ya Shetani ni ya uwongo?
• ‘Mtumikie Mungu kwa moyo kamili.’—1 Nya. 28:9.
• “Mpaka nitakapokufa, sitaukana utimilifu wangu!”—Ayu. 27:5.
24. Kwa nini watu wanakufa?
• “Kupitia mtu mmoja dhambi iliingia katika ulimwengu na kifo kupitia dhambi, basi kifo kikaenea kwa watu wote kwa sababu wote walikuwa wamefanya dhambi.”—Rom. 5:12.
25. Watu waliokufa wako katika hali gani?
• “Walio hai wanajua kwamba watakufa, lakini waliokufa hawajui jambo lolote kamwe.”—Mhu. 9:5.
26. Kuna tumaini gani kwa watu waliokufa?
• “Kutakuwa na ufufuo wa waadilifu na wasio waadilifu pia.”—Mdo. 24:15.
27. Ni watu wangapi wataenda mbinguni kutawala pamoja na Yesu?
• “Tazama! Mwanakondoo amesimama juu ya Mlima Sayuni, na pamoja naye 144,000 walioandikwa jina lake na jina la Baba yake kwenye mapaji ya nyuso zao.”—Ufu. 14:1.
-
-
Sehemu ya 2: Maisha ya KikristoTengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
-
-
MASWALI KWA AJILI YA WALE WANAOTAKA KUBATIZWA
Sehemu ya 2: Maisha ya Kikristo
Kwa kujifunza Biblia, umepata ujuzi kuhusu yale ambayo Yehova anataka ufanye na jinsi ya kuishi kupatana na viwango vyake vya uadilifu. Ili uishi kupatana na mambo ambayo umejifunza, huenda ulihitaji kufanya mabadiliko kadhaa kuelekea mwenendo wako na mtazamo wako kuhusu maisha. Sasa, kwa kuwa umeazimia kuishi kupatana na viwango vya uadilifu vya Yehova, unaweza kumtolea utumishi unaokubalika ukiwa mhudumu wa habari njema.
Kuzungumzia maswali yafuatayo kutakusaidia kukazia akilini matakwa ya uadilifu ya Yehova na kukukumbusha baadhi ya mambo unayoweza kufanya ili uwe mtumishi wake anayekubalika. Habari hii itakazia umuhimu wa kufanya mambo yote ukiwa na dhamiri njema na kwa njia itakayomletea Yehova heshima.—2 Kor. 1:12; 1 Tim. 1:19; 1 Pet. 3:16, 21.
Tangu ulipoanza kujifunza Biblia mpaka sasa, ni wazi kwamba una hamu ya kujitiisha chini ya utawala wa Yehova na kuwa sehemu ya tengenezo lake. Maswali na marejeo ya Maandiko yatakusaidia kuchunguza ikiwa unaelewa maana ya kujitiisha chini ya mpango uliowekwa na Yehova, iwe ni katika kutaniko, familia, au inapohusu siasa za mfumo huu wa mambo. Bila shaka, utathamini sana mipango iliyowekwa na Yehova ya kuwaelimisha na kuwaimarisha watu wake kiroho. Mipango hiyo inatia ndani mikutano ya kutaniko ambayo unapaswa kuendelea kuhudhuria na kushiriki kadiri hali zako zinavyokuruhusu.
-