-
Onyesha Uaminifu wa Kikristo Mtu wa Ukoo Anapotengwa na UshirikaHuduma ya Ufalme—2002 | Agosti
-
-
2 Jinsi ya Kuwatendea Wale Waliotengwa na Ushirika: Neno la Mungu linawaamuru Wakristo wasishirikiane na mtu ambaye ametengwa na kutaniko: “Mkome kuchangamana katika ushirika pamoja na yeyote aitwaye ndugu ambaye ni mwasherati au mtu mwenye pupa au mwabudu-sanamu au mtukanaji au mlevi au mnyang’anyi, wala hata kula pamoja na mtu wa namna hiyo. . . . Ondoeni yule mtu mwovu miongoni mwenu wenyewe.” (1 Kor. 5:11, 13) Maneno ya Yesu katika Mathayo 18:17 pia yanahusiana na habari hiyo: “Mwache [aliyetengwa na ushirika] awe kwako kama vile mtu wa mataifa na kama mkusanya-kodi.” Wasikilizaji wa Yesu walijua vizuri kwamba Wayahudi wa wakati huo hawakuwa wakichangamana na watu wasio Wayahudi na kwamba jamii iliwatenga wakusanya-kodi. Kwa hiyo Yesu alikuwa akiwaagiza wafuasi wake wasishirikiane na watu waliotengwa na ushirika.—Ona gazeti Mnara wa Mlinzi la Januari 1, 1982, ukurasa wa 10-12.
3 Hiyo yamaanisha kwamba Wakristo waaminifu hawashirikiani kiroho na mtu yeyote aliyetengwa na kutaniko. Lakini mengi zaidi yanahusika. Neno la Mungu lasema kwamba ‘hatupaswi hata kula pamoja na mtu wa namna hiyo.’ (1 Kor. 5:11) Kwa hiyo, twaepuka pia kushirikiana na mtu aliyetengwa na ushirika katika shughuli za kirafiki. Hiyo inamaanisha kwamba hatutashirikiana naye katika tafrija, sherehe, michezo, au kwenda naye madukani au kwenye majumba ya sinema au kula pamoja naye nyumbani au mkahawani.
4 Vipi kuongea na mtu aliyetengwa na ushirika? Ingawa Biblia haitaji kila hali, 2 Yohana 10 inatusaidia kuona maoni ya Yehova kuhusu jambo hilo: “Ikiwa yeyote aja kwenu na haleti ufundishaji huu, msimpokee kamwe nyumbani mwenu wala kusema salamu kwake.” Kuhusu jambo hili, gazeti Mnara wa Mlinzi la Januari 1, 1982, lilisema hivi kwenye ukurasa wa 17: “Kusema neno fupi tu la ‘Jambo’ (Habari?) kunaweza kuwa ndiyo hatua ya kwanza inayopanuka na kuwa mazungumzo na hata kuwa urafiki. Je! tungetaka kuichukua hatua hiyo ya kwanza kumwelekea mtu aliyetengwa na ushirika?”
5 Kwa kweli, ni kama tu vile ambavyo toleo hilohilo la Mnara wa Mlinzi linavyosema kwenye ukurasa wa 23: “Jambo la uhakika ni kwamba wakati Mkristo anapojiacha atende dhambi kisha inakuwa lazima atengwe na ushirika, yeye anapoteza mambo mengi: msimamo wake wenye kukubaliwa na Mungu; . . . ushirika mtamu pamoja na kina ndugu, kutia na mwingi wa ushirika aliokuwa nao pamoja na watu wa ukoo wake walio Wakristo.”
-
-
Onyesha Uaminifu wa Kikristo Mtu wa Ukoo Anapotengwa na UshirikaHuduma ya Ufalme—2002 | Agosti
-
-
12 Manufaa za Kuwa Mwaminifu kwa Yehova: Kuna manufaa ya kufuata mpango wa Kimaandiko wa kutenga na ushirika na kuepuka watenda makosa wasiotubu. Huhifadhi usafi wa kutaniko na kuonyesha kuwa sisi tunafuata viwango vya juu vya Biblia. (1 Pet. 1:14-16) Hutulinda na madhara. (Gal. 5:7-9) Pia humpa mkosaji fursa ya kunufaika kikamili na nidhamu aliyopata, ambayo itamsaidia atokeze “tunda lenye kufanya amani, yaani, uadilifu.”—Ebr. 12:11.
13 Baada ya kusikiliza hotuba moja kwenye kusanyiko la mzunguko, ndugu mmoja na dada yake wa kimwili waligundua kwamba wanahitaji kufanya marekebisho katika njia ambayo walimtendea mama yao aliyekuwa akiishi kwingineko na ambaye alikuwa ametengwa na ushirika kwa miaka sita. Upesi baada ya kusanyiko, ndugu huyo aliongea na mama yake, na baada ya kumhakikishia upendo wao, akamweleza kwamba hawawezi tena kuongea naye isipokuwa kuwe na mambo muhimu ya familia yaliyohitaji wawasiliane. Punde baada ya hapo, mama yake alianza kuhudhuria mikutano na baadaye akarudishwa. Pia, mume wake asiyeamini alianza kujifunza na baada ya muda fulani akabatizwa.
14 Kufuata kwa uaminifu mpango wa kutenga na ushirika ulio katika Maandiko huonyesha upendo wetu kwa Yehova na humtolea jibu yule anayemlaumu. (Mit. 27:11) Tukifanya hivyo tuna hakika tutapata baraka za Yehova. Mfalme Daudi aliandika hivi kumhusu Yehova: “Nimeshika maagizo yake yote, sikuacha kufuata masharti yake. Wewe ni mwaminifu kwa walio waaminifu.”—2 Sam. 22:23, 26, Biblia Habari Njema.
-