Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ed kur. 27-30
  • Daraka la Wazazi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Daraka la Wazazi
  • Mashahidi wa Yehova na Elimu
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Wafanyakazi Wenzao, Si Washindani
  • Matatizo ya Shule Leo
  • Kushirikiana na Mfumo wa Shule
    Shule na Mashahidi wa Yehova
  • Funguo za Elimu Nzuri
    Amkeni!—1995
  • Wazazi—Wazoezeni Watoto Wenu Kwa Upendo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Wazazi—Wasaidieni Watoto Wenu Wampende Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2022
Pata Habari Zaidi
Mashahidi wa Yehova na Elimu
ed kur. 27-30
Picha katika ukurasa wa 26-27

Daraka la Wazazi

Bila shaka, kulea watoto kuwa watu wazima wenye usawaziko katika jamii ya leo si jambo rahisi.

Picture on page 28

Waelimishaji wana daraka kuu katika kutokeza watu wazima vijana waliorekebishwa vizuri

TAASISI ya Kitaifa ya Afya ya Akilini ya Marekani ilitangaza matokeo ya uchunguzi fulani wa wazazi walioonwa kuwa wenye mafanikio—wale ambao watoto wao, wenye umri wa miaka zaidi ya 21, “walikuwa watu wazima wenye matokeo ambao walionekana kuwa wenye kubadilikana vizuri na jamii yetu.” Wazazi hao waliulizwa hivi: ‘Kwa msingi wa ono lenu kibinafsi, ni shauri gani zuri zaidi mwezalo kutolea wazazi wengine?’ Majibu ya kawaida zaidi yalikuwa haya: ‘Onyesha upendo mwingi,’ ‘toa nidhamu kwa njia ya kujenga,’ ‘tumia wakati pamoja nao,’ ‘fundisha watoto wako tofauti kati ya mema na mabaya,’ ‘sitawisha hali ya kustahiana,’ ‘wasikilize kikweli,’ ‘toa mwongozo badala ya hotuba,’ na ‘mwe wenye maoni ya kihalisi.’

Hata hivyo, wazazi hawako peke yao katika kujitahidi kutokeza watu wazima vijana waliorekebishwa vizuri. Waelimishaji pia wana daraka katika hilo. Mshauri fulani wa shule mwenye uzoefu alionelea hivi: “Kusudi hasa la elimu rasmi ni kutegemeza wazazi katika kutokeza watu wazima vijana wenye kuchukua madaraka ambao wamesitawishwa vizuri kiakili, kimwili, na kihisiamoyo.”

Kwa hiyo wazazi na waelimishaji wana lengo lilelile—kutokeza vijana ambao baadaye watakuwa watu wazima wakomavu na wenye usawaziko wanaofurahia maisha na wawezao kuona mahali pao katika jamii wanamoishi.

Wafanyakazi Wenzao, Si Washindani

Hata hivyo, matatizo hutokea wakati wazazi wanaposhindwa kushirikiana na waelimishaji. Kwa kielelezo, wazazi fulani hawajali hata kidogo elimu ya watoto wao; wengine hujaribu kushindana na walimu. Likizungumzia hali hii, jarida moja la Kifaransa lilisema hivi: “Mwalimu hawi tena peke yake katika kusimamia mambo. Wazazi, wanaokazia kupita kiasi mafanikio ya watoto wao, huchanganua vitabu vya shule, huamua na kuchambua njia za kufundisha, nao hukasirika mara iyo hiyo kwa sababu ya maksi mbaya za kwanza za mtoto wao.” Matendo hayo yaweza kuingilia haki za walimu.

Picha katika ukurasa wa 29

Mashahidi wa Yehova huhisi kwamba watoto wao wanatumikiwa vizuri zaidi wakati wazazi wanaposhirikiana na waelimishaji, wakipendezwa na elimu ya watoto wao kwa bidii na kwa njia yenye kusaidia

Mashahidi wa Yehova huhisi kwamba watoto wao wanatumikiwa vizuri zaidi wakati wazazi wanaposhirikiana na waelimishaji, wakipendezwa na elimu ya watoto wao kwa bidii na kwa njia yenye kusaidia. Wao huamini kwamba ushirikiano huo ni wa maana hasa kwa sababu kazi yako ukiwa mwelimishaji imezidi kuwa ngumu.

Matatizo ya Shule Leo

Zikionyesha hali ya jamii ambayo hizo ni sehemu yayo, shule hazilindwi dhidi ya matatizo ya jamii kwa ujumla. Matatizo ya kijamii yameongezeka upesi kwa muda wa miaka ambayo imepita. Likifafanua hali katika shule moja Marekani, The New York Times liliripoti hivi: “Wanafunzi hulala darasani, wao hutishana kwenye vijia vya shule vilivyojaa michoro na maandishi, wao huwashusha wale wanafunzi wema. . . . Karibu wanafunzi wote wanakabiliana na matatizo kama vile kutunza watoto, kushughulika na wazazi walio gerezani, na kuponyoka ujeuri wa magenge. Katika siku yoyote ile, karibu mmoja kati ya watano hukosa shule.”

Lenye kutia hofu zaidi ni lile tatizo la kimataifa lenye kuongezeka la ujeuri shuleni. Mahali pa mapigano ya mara kwa mara yanayohusisha kusukumana pamechukuliwa na ufyatuaji-risasi na uchomaji-visu ulio wa kawaida. Silaha zimekuja kuwa za kawaida zaidi, mashambulio yamekuwa mabaya zaidi, watoto wakielekea kuwa wajeuri upesi zaidi na wakiwa wachanga zaidi.

Bila shaka, si kila nchi inayokabili hali hizo za kuhuzunisha. Hata hivyo, waelimishaji wengi ulimwenguni pote hukabili ile hali itajwayo katika lile gazeti la Kifaransa la kila juma Le Point: “Mwalimu hastahiwi tena; yeye hana mamlaka.”

Picha katika ukurasa wa 30

Wazazi wenye mafanikio hutumia wakati pamoja na watoto wao

Kutostahi huko kwa mamlaka kwatokeza hatari halisi kwa watoto wote. Kwa hiyo Mashahidi wa Yehova hujaribu kukaza kikiki katika watoto wao utii na staha kwa mamlaka, sifa ambazo mara nyingi hukosekana katika maisha ya shuleni leo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki