Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • sj uku. 30
  • Kushirikiana na Mfumo wa Shule

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kushirikiana na Mfumo wa Shule
  • Shule na Mashahidi wa Yehova
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Ushirikiano wa Wazazi
  • Funguo za Elimu Nzuri
    Amkeni!—1995
  • Wazazi—Iweni Watetezi wa Mtoto Wenu
    Amkeni!—1994
  • Wazazi—Wazoezeni Watoto Wenu Kwa Upendo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Kufurahisha Mioyo ya Wazazi Wako
    Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha
Pata Habari Zaidi
Shule na Mashahidi wa Yehova
sj uku. 30

Kushirikiana na Mfumo wa Shule

Mashahidi wa Yehova wanaamini kwamba elimu nzuri ni mojapo mambo ya maana zaidi sana ya urithi ambao watoto wanaweza kupewa. Lakini ni nani mwenye daraka la kwanza la kuelimisha mtoto? Je! ni walimu tu katika shule?

Inaonekana kama watu fulani wanafikiri hivyo. Lakini, watoto wanazaliwa kwa wazazi nao ni sehemu ya jamaa. Wao si mazao ya Serikali wala ya vyama vyo vyote vya serikali. Kwa sababu hiyo, wazazi ndio wenye daraka walilopewa na Mungu kuamua jambo ambalo watoto wao watafundishwa.

Hata hivyo, pia, walimu wa shule wanatoa utumishi bora, wenye kuthaminiwa sana. Na tunajua kwamba kazi yao si rahisi siku hizi zenye kuharibika kwa nidhamu. Wazazi wanaweza kufanya nini ili washirikiane nao?

Ushirikiano wa Wazazi

Kwanza, ni jambo la maana kwa wazazi kufahamiana na walimu wa watoto wao—wafanye mipango ya kuonana nao na kuzungumza nao. Bila shaka kuonana huko hakupasi kuwe na kusudi la kwenda kubishana, bali ni kuona jinsi wazazi na walimu wanavyoweza kushirikiana ili wasaidie maendeleo ya mtoto. Wazazi wanafurahi kusikiliza wakati mwalimu anapozungumza na pia wanampasha habari waziwazi juu ya jambo ambalo wanataka watoto wao wafanye.

Katika mkutano huo baba Shahidi au mama amepaswa amjulishe mwalimu kwamba wazazi wanatazamia watoto wao kuwa na mwenendo wa Kikristo unaofaa, na kwamba ikiwa watoto wanakuwa na adabu mbaya, wanataka wapashwe habari hiyo. Pia wazazi wamepaswa watoe uhakikisho wa kuonyesha watamuunga mkono mwalimu katika nidhamu yo yote yenye kufaa, inayotolewa, hata kuiongeza nyumbani.

Njia nyingine ambazo kwa hizo wazazi wanaweza kusaidia: Hakikisha watoto wanapata kiamshakinywa kizuri kabla ya kwenda shuleni. Hakikisha kwamba masomo yao ya nyumbani yamemalizika na kwamba wameenda na vitabu vyao vyote vya shule. Heshimu nyakati zote sheria za shule na kuonyesha unatazamia watoto pia waziheshimu. Watie moyo watoto wanaporudi nyumbani, waseme shughuli walizofanya shuleni na matatizo yo yote ambayo labda walipata huko.

Idara ya Afya, Elimu, na Usitawi wa Huduma za Jamii ya Marekani, inawaambia wazazi jinsi ya kutia moyo watoto wao wajifunze, ikisema hivi kupitia kichapo Helping Children Make Career Plans: Tips for Parents: “Saidia mtoto wako afahamu jinsi masomo yake ya shuleni yatakavyokuwa ya maana sana baadaye katika maamuzi ya kazi atakayofanya. Waonyeshe jinsi masomo ya kusoma, hesabu, na lugha yanavyotumiwa karibu katika kazi zote. Kwa kifupi, wasaidie wafahamu kwamba kuna sababu za maana sana za kwenda shuleni kuliko kwenda tu shuleni.”

Tunatumaini kwa unyofu wa moyo kwamba taarifa iliyo katika broshua hii itasaidia kuwe ushirikiano mzuri kati ya wakuu wa shule na jamaa za Mashahidi wa Yehova.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki