-
Daima Kaza Uangalifu kwa Kufundisha KwakoMnara wa Mlinzi—1999 | Machi 15
-
-
Kulingana na Waefeso 4:11-13, wanaume wamechaguliwa ili watumikie wakiwa “wachungaji na walimu, kwa kusudi la kuwarekebisha upya watakatifu, kwa ajili ya kazi ya huduma, kwa ajili ya kuujenga mwili wa Kristo.” Nyakati nyingine, usanifu wao wa kufundisha wahusisha uhitaji wa ‘kukaripia, kukemea, kuhimiza kwa bidii, kwa ustahimilivu wote.’ (2 Timotheo 4:2) Kazi ya walimu ilikuwa muhimu sana hivi kwamba, alipowaandikia Wakorintho, Paulo aliwaorodhesha walimu punde tu baada ya mitume na manabii.—1 Wakorintho 12:28.
-
-
Daima Kaza Uangalifu kwa Kufundisha KwakoMnara wa Mlinzi—1999 | Machi 15
-
-
Wanashawishwa Kuamini
5, 6. (a) Ukristo wa kweli watofautianaje na ibada isiyo ya kweli? (b) Wazee huwasaidiaje wapya wafanye maamuzi yenye hekima?
5 Hivyo, Ukristo wa kweli hutofautiana sana na dini za uwongo zilizo nyingi ambazo hutafuta kudhibiti fikira za washiriki wao. Yesu alipokuwa duniani, viongozi wa kidini walitafuta kudhibiti karibu kila jambo katika maisha ya watu kupitia mapokeo ya kibinadamu yenye uonevu. (Luka 11:46) Mara nyingi makasisi wa Jumuiya ya Wakristo wamefanya vivyo hivyo.
6 Hata hivyo, ibada ya kweli ni “utumishi mtakatifu” ambao twautoa pamoja na ‘nguvu zetu za kufikiri kuzuri.’ (Waroma 12:1) Watumishi wa Yehova ‘wanashawishwa kuamini.’ (2 Timotheo 3:14) Nyakati fulani, wale wanaoongoza huenda wakahitaji kuanzisha miongozo na taratibu fulani ili kutaniko litende kazi kwa njia inayofaa. Hata hivyo, badala ya wazee kutafuta kuwafanyia Wakristo wenzao maamuzi, wao huwafundisha “kutofautisha lililo sahihi na lililo kosa pia.” (Waebrania 5:14) Kimsingi, wazee hufanya hivyo kwa kulilisha kutaniko “maneno ya imani na fundisho bora.”—1 Timotheo 4:6.
-