Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Usitawi wa Muundo wa Tengenezo
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Hata hivyo, kulingana na njia waliyoelewa mambo wakati ule, kuteuliwa kwa wazee, na mashemasi ili kuwasaidia, kulifanywa kwa kura ya kutaniko. Kila mwaka, au mara nyingi zaidi ikihitajiwa, sifa za wale wawezao kutumikia zilifikiriwa, na kura ikapigwa. Kwa msingi ulikuwa utaratibu wa kidemokrasi, lakini ambao ulibanwa na mipaka iliyokusudiwa kutenda kuwa ulinzi salama. Wote katika kutaniko walihimizwa wapitie kwa uangalifu sifa za Kibiblia na kuonyesha kwa kura, si maoni yao wenyewe, bali yale ambayo waliamini kuwa mapenzi ya Bwana. Kwa kuwa ni wale tu “waliojitakasa kabisa” waliokuwa na haki ya kupiga kura, kura yao ya umoja, ikiongozwa na Neno na roho ya Bwana, ilionwa kuwa yaonyesha mapenzi ya Bwana katika jambo hilo. Ijapokuwa huenda ikawa Ndugu Russell hakujua kabisa, pendekezo lake la mpango huo labda lilivutwa kwa kadiri fulani na azimio lake la kuepuka mfano wowote wa jamii ya makasisi iliyokwezwa na pia malezi yake mwenyewe akiwa tineja katika Congregational Church.

      Buku la Millennial Dawn liitwalo The New Creation (lililotangazwa katika 1904) lilipozungumza tena kirefu juu ya fungu la wazee na njia ambayo walipaswa kuteuliwa, uangalifu wa pekee ulielekezwa kwenye Matendo 14:23. Konkodansi zilizotungwa na James Strong na Robert Young zilitajwa kuwa mamlaka kwa maoni ya kwamba ile taarifa “walikuwa wamewaweka rasmi kuwa wazee” (KJ) yapasa kutafsiriwa “walikuwa wamewateua kuwa wazee kwa wonyesho wa mikono.”d Baadhi ya tafsiri za Biblia hata husema kwamba wazee ‘waliwekwa kwa kura.’ (Literal Translation of the Holy Bible ya Young; Emphasised Bible ya Rotherham) Lakini ni nani aliyepaswa kupiga kura hiyo?

      Kuchukua maoni ya kwamba kupiga kura kulipasa kufanywe na kutaniko lote hakukuleta matokeo yaliyotumainiwa sikuzote. Wale waliopiga kura walipaswa kuwa watu “waliojitakasa kabisa,” na baadhi ya wale waliochaguliwa walitimiza kikweli sifa za Kimaandiko nao walitumikia ndugu zao kwa unyenyekevu. Lakini kupiga kura mara nyingi kulionyesha upendeleo wa kibinafsi badala ya Neno na roho ya Mungu. Hivyo, katika Halle, Ujerumani, wakati wengine waliofikiri kwamba walipaswa kuwa wazee hawakupata vyeo walivyotaka, walisababisha migawanyiko mibaya. Katika Barmen, Ujerumani, miongoni mwa wale waliokuwa wachaguliwa katika 1927 mlikuwa wanaume waliopinga kazi ya Sosaiti, na kelele nyingi ilipigwa wakati wa kuonyesha mikono kwenye uchaguzi. Hivyo ilikuwa lazima kugeukia njia ya kupiga kura kwa siri.

      Huko nyuma katika 1916, miaka mingi kabla ya visa hivyo, Ndugu Russell, akiwa na hangaiko kubwa, alikuwa ameandika: “Hali mbaya sana ya mambo huwa katika Madarasa fulani wakati wa kufanywa uchaguzi. Watumishi wa Kanisa hujaribu kuwa watawala, madikteta—nyakati nyingine hata wakishika uenyekiti wa mkutano yaonekana kwa lengo la kuona kwamba wao na marafiki wao wa pekee watachaguliwa kuwa Wazee na Mashemasi. . . . Baadhi yao hujaribu kutumia Darasa kwa faida yao kwa siri kwa kuwa na uchaguzi wakati fulani unaowafaa hasa wao na marafiki wao. Wengine hutafuta kujaza mkutano marafiki wao, wakileta watu walio wageni, ambao hawana wazo la kuhudhuria kwa ukawaida kwenye Darasa, bali huja tu kwa sababu ya urafiki ili kupigia kura mmoja wa marafiki wao.”

  • Usitawi wa Muundo wa Tengenezo
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • [Sanduku katika ukurasa wa 207]

      Kwa Nini Badiliko?

      Alipoulizwa swali juu ya badiliko lake la maoni kuhusu kuteuliwa kwa wazee katika vile vikundi mbalimbali vya watu wa Bwana, C. T. Russell alijibu hivi:

      “Kwanza kabisa nafanya haraka kuwahakikishia kwamba mimi sijadai kamwe kuwa asiyeweza kufanya kosa. . . . Sisi hatukani kukua katika ujuzi, na kwamba twaona sasa kwa nuru iliyo tofauti kidogo mapenzi ya Bwana kwa habari ya Wazee au viongozi katika vile vikundi vidogo mbalimbali vya watu wake. Kosa letu katika uamuzi lilikuwa katika kutazamia mengi mno kutoka kwa ndugu zetu wapendwa ambao, wakija mapema katika Kweli, walipata kiasili kuwa viongozi wa makampuni haya madogo. Maoni ya kuwaziawazia tuliyokuwa nayo kuwahusu yalikuwa, kwamba ujuzi juu ya Kweli ungekuwa na matokeo ya kuwanyenyekeza sana, ukiwafanya wafahamu hali yao ya kutokuwa wa maana, na kwamba lolote walilojua na waliloweza kutolea wengine lilikuwa wakiwa vinywa vya Mungu na kwa sababu watumiwa naye. Matumaini yetu ya kuwaziawazia yalikuwa kwamba hao wangekuwa katika kila maana ya hilo neno vielelezo kwa kundi; na kwamba mwelekezo wa Bwana ukileta katika kampuni dogo mmoja au zaidi wenye uhodari wa kadiri hiyohiyo, au hodari zaidi, wa kuitoa Kweli, kwamba roho ya upendo ingewaongoza kustahiana kwa heshima mmoja na mwenzake, na hivyo kusaidiana na kuhimizana mmoja na mwenzake kushiriki katika utumishi wa Kanisa, mwili wa Kristo.

      “Tukiwa na wazo hilo akilini tulikata kauli kwamba vile vipimo vikubwa vya neema na kweli vilivyopo sasa na vinavyothaminiwa na watu wa Bwana waliojitakasa vingefanya isihitajiwe kwao kufuata mwendo ulioonyeshwa na mitume katika Kanisa la mapema. Kosa letu lilikuwa kushindwa kujua kwamba mipango iliyoonyeshwa na mitume chini ya usimamizi wa kimungu ni bora kuliko chochote ambacho wengine wangeweza kutunga, na kwamba Kanisa kwa ujumla litahitaji kuwa na kanuni hizo zilizoanzishwa na mitume mpaka sisi sote tuwe tumefanywa watimilifu na wakamilifu kwa kubadilishwa kwetu katika ufufuo, tuwe na ushirika wa moja kwa moja na Bwana-Mkubwa.

      “Kosa letu tulilifahamu hatua kwa hatua tulipoona miongoni mwa ndugu wapendwa kadiri fulani ya roho ya ushindani, na kwa upande wa wengi tamaa ya kushika uongozi wa mikutano kuwa cheo badala ya kuwa utumishi, na kutohusisha na kuzuia ndugu wengine wasisitawi wakiwa viongozi wenye uwezo uleule kiasili na wenye ujuzi uleule juu ya Kweli na uhodari katika kutumia upanga wa Roho.”—“Zion’s Watch Tower,” Machi 15, 1906, uku. 90.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki