Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Jinsi Hana Alivyopata Amani
    Mnara wa Mlinzi—2007 | Machi 15
    • Hana ni mwanamke tasa, lakini Penina, yule mke mwingine wa Elkana, ana watoto kadhaa. Penina anashindana na Hana.—1 Samweli 1:2b.

      Mwanamke tasa anadharauliwa miongoni mwa wanawake wa Israeli na hata watu wanaona kwamba kuwa tasa kunaonyesha mtu hastahili machoni pa Mungu. Lakini hakuna jambo linaloonyesha kwamba hali ya Hana ya kutoweza kupata watoto inathibitisha kwamba hana kibali cha Mungu. Hata hivyo, badala ya kujaribu kumfariji Hana, Penina anatumia uwezo wake wa kupata watoto kumuumiza kihisia mke mwenzake.

      Safari za Kwenda Patakatifu pa Yehova

      Hali hiyo ni yenye kufadhaisha, hata hivyo familia ya Elkana inafunga safari kila mwaka ili kutoa dhabihu katika patakatifu pa Yehova huko Shilo.a Inaelekea kwamba wanasafiri kwa miguu safari hiyo ya kilomita 60 hivi kwenda na kurudi. Haikosi kwamba hizo ni pindi ngumu hasa kwa Hana kwa sababu Penina na watoto wake wanapewa mafungu kadhaa ya dhabihu ya ushirika, lakini Hana anapewa fungu moja tu. Penina anatumia nafasi kama hizo kumsumbua Hana, akimfanya akasirike kwa sababu inaonekana kwamba Yehova “amefunga tumbo lake la uzazi.” Hana anateseka hivyo mwaka baada ya mwaka, na hilo linamfanya Hana alie na asile chakula. Safari ambazo zinapaswa kumletea shangwe zinamhuzunisha sana. Hata hivyo, Hana anafunga safari hizo za kwenda patakatifu pa Yehova.—1 Samweli 1:3-7.

      Je, unaona jinsi Hana alivyotuwekea mfano mzuri? Unafanya nini unapovunjika moyo? Je, unajitenga na wengine na kuacha kushirikiana na waamini wenzako? Hana hakufanya hivyo. Alikuwa na desturi ya kuwa kati ya waabudu wa Yehova. Tunapokabili hali ngumu, sisi pia tunapaswa kufanya hivyo.—Zaburi 26:12; 122:1; Methali 18:1; Waebrania 10:24, 25.

      Elkana anajaribu kumfariji Hana na kumhimiza afunue yaliyo moyoni mwake. “Hana, kwa nini unalia, na kwa nini huli chakula, na kwa nini moyo wako unahisi vibaya?” anamuuliza. “Je, mimi si bora kwako kuliko wana kumi?” (1 Samweli 1:8) Labda Elkana hajui kwamba Penina anamtendea Hana kwa njia isiyo ya fadhili, na huenda Hana anaona ni afadhali ateseke kimyakimya badala ya kulalamika. Vyovyote vile, Hana ambaye anathamini mambo ya kiroho, anatafuta amani kwa kumwendea Yehova katika sala.

  • Jinsi Hana Alivyopata Amani
    Mnara wa Mlinzi—2007 | Machi 15
    • Hana anatoa sala kwa njia ambayo inamfanya Kuhani Mkuu Eli afikiri kwamba Hana amelewa. Midomo yake inatetemeka, lakini Eli hasikii sauti yoyote, kwa kuwa Hana anasali moyoni mwake. Anasali kwa bidii sana. (1 Samweli 1:12-14) Wazia jinsi Hana anavyohisi Eli anapomshtumu kwamba amelewa! Hata hivyo, anamjibu kuhani huyo mkuu kwa heshima.

  • Jinsi Hana Alivyopata Amani
    Mnara wa Mlinzi—2007 | Machi 15
    • Simulizi la Hana ambalo liliongozwa na roho linaonyesha kwamba tunaweza kuumizwa kihisia na udhaifu wa watu wengine au dhihaka zao. Hata hivyo, hatupaswi kuruhusu majaribu kama hayo yatuondolee shangwe yetu ya kumtumikia Yehova. Yeye ndiye Msikiaji mkuu wa sala, ambaye anajibu vilio vya watu wake waaminifu, akiwakomboa kutoka katika mateso na kuwapa amani tele na baraka nyingine nyingi.—Zaburi 22:23-26; 34:6-8; 65:2.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki