-
Tangazeni Mfalme na Ufalme! (1919-1941)Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Jumamosi, Septemba 18, kufuatia hotuba yake ya asubuhi, Ndugu Rutherford alitoa kitabu chenye rangi-hudhurungi Enemies. Kilishutumu dini bandia kuwa “adui mkubwa, sikuzote akidhuru wanadamu.” Wanadini bandia walitambuliwa kuwa “mawakili wa Ibilisi, wawe wanajua hivyo au la.” Alipokuwa akitoa kitabu hicho kwa wasikilizaji, Ndugu Rutherford alisema hivi: “Mtaona kwamba jalada lacho ni rangi-hudhurungi, na kwa kukitumia sisi tutamtandika yule bi kizee.”h
-
-
Tangazeni Mfalme na Ufalme! (1919-1941)Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
h Rejezo kwa “kahaba mkubwa,” aliyetajwa katika Ufunuo Sura ya 17. Kitabu Enemies kilitaarifu hivi: “Matengenezo yote duniani ambayo yanapinga Mungu na ufalme wake . . . huchukua jina ‘Babiloni’ na ‘kahaba,’ na majina hayo hasa hutumika kwa lile tengenezo kuu la kidini, kanisa la Katoliki ya Roma.” (Ukurasa 198) Miaka mingi baadaye ilionwa kwamba kwa kweli kahaba huwakilisha milki ya ulimwengu ya dini zote bandia.
-