-
Nchi Ambazo Zilikuwa Sehemu ya Yugoslavia2009 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Hata hivyo, kikundi cha watu 30 wa makabila mbalimbali kilikuwa kikikutana katika nyumba ya Saliu. “Katika miaka hiyo,” anakumbuka Saliu, “mikutano ilifanywa katika Kiserbia, na tulipata vitabu kutoka Belgrade. Siku moja polisi walikuja kwa ghafula katika nyumba yangu. Wakati huo akina ndugu kutoka Belgrade walikuwa tu wameleta vitabu, na sote tulikuwa tukifurahia ushirika. Nilipowaambia polisi kwamba hao walikuwa ndugu zangu, hawangeweza kuelewa jinsi Waserbia na Waalbania wanavyoweza kuwa ndugu.”
-
-
Nchi Ambazo Zilikuwa Sehemu ya Yugoslavia2009 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
KUFINYANGWA NA MAONI YA YEHOVA
Dada mmoja alisema hivi: “Chuki kati ya Waserbia na Waalbania ilikuwa kali sana. Tulijifunza kuwachukia tangu utotoni. Si rahisi kuacha chuki hiyo hata baada ya kujifunza kweli. Wengi wetu tulilazimika kufanya mabadiliko makubwa ili tufuate maoni ya Yehova. Kwa sababu ya chuki hiyo, hata nilipokuwa nikijifunza kwamba Yehova ni upendo, nilikuwa nikimwepuka dada fulani katika kutaniko kwa sababu tu ni Mserbia. Hata hivyo, nilipoendelea kujifunza nilianza kutambua kwamba kweli ya Neno la Yehova inawaunganisha watu, lakini mafundisho ya dini nyingine yanawagawanya watu.” Je, nguvu za Neno la Mungu za kuwabadili watu zimemsaidia dada huyo kuvaa utu mpya wa Kikristo? Anasema hivi: “Sasa, ninafurahi kutumikia katika kutaniko moja na ndugu na dada zangu Waserbia.”—Kol. 3:7-11; Ebr. 4:12.
Umoja wa kweli wa Kikristo unaonekana wazi katika ulimwengu huu uliogawanyika kidini. Wakati watu walipokuwa wakiteketeza nyumba na kurusha guruneti kwa sababu ya roho ya utaifa, ndugu zetu walikuwa wakisafiri kwenda Belgrade, Serbia, kwa ajili ya kusanyiko mwezi wa Julai 1998. Waalbania, Wakroatia, Wamakedonia, na Waromani walisafiri pamoja katika mabasi kwa amani. Dashurie Gashi, ambaye alikuwa akienda kubatizwa kwenye kusanyiko hilo, anasema hivi: “Askari-jeshi walipolisimamisha basi, nyuso zao zilionyesha kwamba walikuwa wameshtuka. Hata ingawa kulikuwa na chuki kali ya kikabila katika nchi hizo, tulikuwa kikundi kimoja chenye umoja—watu wa Yehova.”
-