Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Louis Pasteur—Kilichofunuliwa na Kazi Yake
    Amkeni!—1996 | Desemba 8
    • Uhai Hutoka Katika Uhai

      Tangu nyakati za kale, dhana nyingi za ajabu zilikuwa zimetokezwa ili kueleza kutokea kwa wadudu, mabuu, au viumbe vinginevyo vipatikanavyo katika mata yenye kuoza. Kwa mfano, katika karne ya 17, mwanakemia Mbelgiji alidai kwamba alikuwa amefanya panya atokee kwa kuweka blausi chafu katika mtungi wenye ngano!

      Katika wakati wa Pasteur mjadala miongoni mwa wanasayansi ulikuwa umepamba moto. Ulikuwa mwito wa ushindani kwelikweli kukabili watetezi wa nadharia ya kwamba uhai ulijitokeza wenyewe kutoka kitu kisicho na uhai. Lakini kwa sababu ya kile alichokuwa amejifunza katika utafiti wake wa uchachukaji, Pasteur alikuwa na uhakika. Kwa hiyo alifanya majaribio yaliyonuiwa kukomesha kabisa-kabisa wazo la kwamba uhai ulijitokeza wenyewe.

      Jaribio lake akitumia chupa zenye shingo nyembamba ni mojapo majaribio yake yajulikanayo sana. Kirutubisho cha kiowevu kilichoachwa nje katika chupa isiyofunikwa huingia viini haraka. Hata hivyo, kiwekwapo katika chupa ambayo huishia kwa shingo nyembamba, kirutubisho hichohicho cha kiowevu hubaki bila kuingia viini. Kwa nini iwe hivyo?

      Maelezo ya Pasteur yalikuwa sahili: Zinapopitia kwenye shingo nyembamba, bakteria zilizo hewani zinaachwa kwenye uso wa glasi, hivi kwamba hewa haina viini inapofika kwenye kiowevu. Viini ambavyo hutokea katika chupa isiyofunikwa havijitokezi vyenyewe kutokana na kirutubisho cha kiowevu bali husafirishwa hewani.

      Ili kuonyesha kwamba hewa ni kisafirishaji kikuu cha vijiumbe-maradhi, Pasteur alikwenda hadi Mer de Glace, barafuto katika milima ya Alps ya Ufaransa. Kwenye kimo cha futi 6,000, yeye alifunua chupa zake zilizofunikwa na kuacha hewa iingie. Kati ya chupa 20, ni moja tu iliyoingiwa na viini. Kisha akaenda kwenye sehemu ya chini ya Milima ya Jura na kurudia jaribio lilo hilo. Hapa, kwa kuwa kimo kilikuwa chini sana, chupa nane ziliingiwa na viini. Hivyo akathibitisha kwamba kwa sababu ya hewa safi zaidi kwenye vimo vya juu zaidi, hakukuwa na hatari nyingi ya kuingiwa na viini.

      Kupitia kwa majaribio kama hayo Pasteur alionyesha kwa njia ya kusadikisha kwamba uhai hutokana na uhai uliokuwapo tu. Huo haujitokezi kinafsia, yaani, wenyewe.

  • Louis Pasteur—Kilichofunuliwa na Kazi Yake
    Amkeni!—1996 | Desemba 8
    • Mjadala wa uhai kujitokeza wenyewe, ambao Pasteur alihusika nao na ambao aliibuka akiwa mshindi, haukuwa ulaghai wa kisayansi tu. Ulikuwa zaidi ya hoja yenye kupendeza ya kuzungumziwa miongoni mwa wanasayansi wachache tu au watu wenye akili. Ulikuwa na umaana mkubwa zaidi—ulihusisha uthibitisho uliohusu kuwapo kwa Mungu.

      François Dagognet, mwanafalsafa Mfaransa aliyeshughulika hasa na sayansi, ataja kwamba “wapinzani [wa Pasteur], wenye kuamini nadharia kwamba hakuna uhai usioonekana na vilevile waatheisti, waliamini kwamba wangeweza kuthibitisha kwamba kiumbe chenye chembe moja kingeweza kutokea katika molekuli yenye kuoza. Hili liliwaruhusu kukataa kuwapo kwa Mungu. Hata hivyo, kulingana na Pasteur, hakukuwa na uwezekano wa uhai kutoka katika kifo.”

      Hadi leo hii uthibitisho wote kutoka majaribio, historia, biolojia, uchimbuzi wa vitu vya kale, na anthropolojia huendelea kuonyesha kile alichodhihirisha Pasteur—kwamba uhai waweza kuja tu kutoka uhai uliokuwapo, si kutoka kitu kisicho na uhai. Na uthibitisho huo pia huonyesha waziwazi kwamba uhai hutokezana “kulingana na aina yake,” kama usimulizi wa Biblia katika Mwanzo usemavyo. Wazao sikuzote huwa wa “jinsi,” au aina ileile na wazazi.—Mwanzo 1:11, 12, 20-25.

      Hivyo, kwa kujua au kwa kutojua, kupitia kazi yake Louis Pasteur aliandaa uthibitisho na ushahidi wenye nguvu dhidi ya nadharia ya mageuzi na uhitaji kamili wa kuwa na muumba ili uhai uwepo duniani. Kazi yake ilionyesha kile alichokubali mtunga-zaburi mnyenyekevu: “Jueni kwamba BWANA ndiye Mungu. Ndiye aliyetuumba na sisi tu watu wake.—Zaburi 100:3.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki