-
Matukio Muhimu ya Mwaka Uliopita2011 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Salvatore, anayeishi Marekani, ni kiziwi na mke wake ni Shahidi wa Yehova. Ingawa amejua kweli ya Biblia kwa miaka mingi, hakufanya maendeleo yoyote ya kiroho. Mke wake alipendekeza kwamba asome Biblia kila siku kwa mwaka mzima. Hata hivyo, hakuelewa alichokuwa akisoma, hivyo akakata tamaa. “Sitawahi kumpenda Yehova,” akasema.
Maisha ya Salvatore yalianza kubadilika alipoambiwa kwamba kulikuwa na sehemu ya Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya katika DVD ya Lugha ya Ishara ya Marekani. Baada ya kusoma kwa undani Neno la Mungu katika lugha ya ishara, alisema hivi kwa msisimuko, “Kwa hakika Mungu alitaka nimjue!” Salvatore alijifunza Biblia, na sasa anamtumikia Yehova kwa furaha akiwa Shahidi aliyebatizwa.
-
-
Matukio Muhimu ya Mwaka Uliopita2011 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Kila mara inapendeza sana kuona jinsi ambavyo vichapo katika lugha ya ishara vinagusa mioyo ya wapya. Natsue, mwanamke kiziwi huko Japani anasema hivi: “Nilianza kujifunza Biblia katika mwaka wa 1981 nikitumia vichapo vilivyoandikwa katika Kijapani. Kwa kuwa sikuelewa chochote na familia yangu ilianza kunipinga, niliacha kujifunza.”
Mnamo Aprili (Mwezi wa 4) 2007, mhubiri mmoja alinionyesha DVD Wewe Unaweza Kuwa Rafiki ya Mungu! katika Lugha ya Ishara ya Kijapani. Hiyo ilikuwa miaka 26 tangu nianze kujifunza Biblia. Mara moja, nilianza tena kujifunza na nikaona kwamba mahitaji yangu ya kiroho yanatoshelezwa. Nilibatizwa Novemba (Mwezi wa 11) 2008.”
-