Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kuwapo Kwa Kristo—kunamaanisha Nini Kwako?
    Mnara wa Mlinzi—2008 | Februari 15
    • Kizazi Kinachoona Ile Ishara

      10, 11. (a) Ni maelezo gani yaliyotolewa wakati uliopita kuhusu kile “kizazi” kinachotajwa katika Mathayo 24:34? (b) Ni nani ambao bila shaka wanafunzi wa Yesu walielewa kwamba wangekuwa sehemu ya “kizazi” hicho?

      10 Wakati uliopita, gazeti hili lilieleza kwamba katika karne ya kwanza, “kizazi hiki” kinachotajwa katika Mathayo 24:34 kilimaanisha “kizazi cha Wayahudi wasioamini ambao waliishi wakati huo.”b Ilionekana kwamba maelezo hayo yalipatana na akili kwa sababu pindi nyingine zote ambazo Yesu alitumia neno “kizazi” halikuwa na maana nzuri, na mara nyingi, Yesu alitumia kivumishi cha sifa mbaya kama vile “kiovu,” ili kufafanua kizazi alichokuwa akizungumzia. (Mt. 12:39; 17:17; Marko 8:38) Hivyo, ilieleweka kwamba katika utimizo wa leo, Yesu alikuwa akizungumza kuhusu kizazi kiovu cha wasio waamini ambao wangeona ishara ya “umalizio wa mfumo wa mambo” (syn·teʹlei·a) na ya mwisho wa mfumo (teʹlos).

      11 Ni kweli kwamba Yesu aliposema “kizazi” kiovu, alikuwa akizungumza na au kuhusu watu waovu wa siku zake. Lakini je, ni lazima “kizazi” anachozungumzia katika Mathayo 24:34 kiwe kilimaanisha watu waovu walioishi siku zake? Kumbuka kwamba wanafunzi wanne wa Yesu walimkaribia “faraghani.” (Mt. 24:3) Kwa kuwa Yesu hakutumia maneno au vivumishi vya sifa mbaya alipozungumza nao kuhusu “kizazi hiki,” bila shaka mitume hao wangeelewa kwamba wao pamoja na wanafunzi wenzao wangekuwa sehemu ya “kizazi” ambacho hakingepitilia mbali kamwe “mpaka mambo yote hayo yatukie.”

      12. Kulingana na mistari mingine katika Mathayo sura ya 24, Yesu alikuwa akizungumza kuhusu nani alipotumia neno “kizazi”?

      12 Tunakata kauli hiyo kwa msingi gani? Kwa kuchunguza kwa uangalifu mistari mingine katika sura hiyo. Kulingana na Mathayo 24:32, 33, Yesu alisema hivi: “Basi jifunzeni jambo hili kutokana na mtini kama mfano: Mara tu tawi lake changa linapokuwa jororo na kutoa majani, mnajua kwamba kiangazi kiko karibu. Vivyo hivyo ninyi pia, mnapoona mambo yote hayo, jueni kwamba yuko karibu milangoni.” (Linganisha Marko 13:28-30; Luka 21:30-32.) Kisha, tunasoma hivi kwenye Mathayo 24:34: “Kwa kweli ninawaambia ninyi kwamba kizazi hiki hakitapitilia mbali kamwe mpaka mambo yote hayo yatukie.”

      13, 14. Kwa nini tunaweza kusema kwamba ni lazima kile “kizazi” ambacho Yesu alizungumzia kilikuwa wanafunzi wake?

      13 Yesu alisema kwamba wanafunzi wake, ambao punde si punde wangetiwa mafuta kwa roho takatifu, ndio wangeweza kukata kauli fulani walipoona “mambo yote hayo” yakitukia. Kwa hiyo, lazima Yesu awe alikuwa akizungumza kuhusu wanafunzi wake aliposema hivi: “Kizazi hiki hakitapitilia mbali kamwe mpaka mambo yote hayo yatukie.”

      14 Tofauti na watu wasio waamini, wanafunzi wa Yesu wangeona ile ishara na pia wangeelewa maana ya ishara hiyo. ‘Wangejifunza’ kutokana na matukio ya ishara hiyo na ‘kujua’ kikweli maana yake. Wangetambua kabisa kwamba “yuko karibu, milangoni.” Ni kweli kwamba Wayahudi wasio waamini na pia Wakristo watiwa-mafuta waaminifu waliona maneno ya Yesu yakitimia kwa kadiri fulani katika karne ya kwanza, lakini ni wafuasi wake watiwa-mafuta tu walioishi wakati huo ndio wangejifunza kutokana na matukio hayo na kuelewa kikweli maana ya mambo waliyokuwa wakiona.

      15. (a) Ni nani wanaofanyiza “kizazi” cha siku zetu ambacho Yesu alizungumzia? (b) Kwa nini hatuwezi kuhesabu urefu kamili wa “kizazi hiki”? (Ona sanduku kwenye ukurasa wa 25.)

      15 Leo, watu ambao hawaelewi kweli ya Mungu wanafikiri kwamba ishara ya kuwapo kwa Yesu haijatokea kwa “wonyesho wenye kutokeza sana.” Wanasema kwamba mambo yote yanaendelea sawasawa tangu zamani. (2 Pet. 3:4) Kwa upande mwingine, ndugu waaminifu watiwa-mafuta wa Kristo, yaani, jamii ya Yohana ya leo, wametambua ishara hiyo kama umeme unaowaka nao wameelewa maana yake ya kweli. Wakiwa kikundi, watiwa-mafuta hao wanafanyiza “kizazi” cha siku zetu, jamii ambayo haitapitilia mbali kamwe “mpaka mambo yote hayo yatukie.”c Hilo linadokeza kwamba wengine kati ya ndugu za Kristo watiwa-mafuta bado watakuwa hai duniani wakati dhiki kuu iliyotabiriwa itakapoanza.

  • Kuwapo Kwa Kristo—kunamaanisha Nini Kwako?
    Mnara wa Mlinzi—2008 | Februari 15
    • c Inaonekana kwamba kizazi hiki kinaishi wakati wa kutimizwa kwa maono ya kwanza ya kitabu cha Ufunuo. (Ufu. 1:10–3:22) Sehemu hiyo ya siku ya Bwana inaanza mwaka wa 1914 mpaka mshiriki wa mwisho mtiwa-mafuta aliye mwaminifu atakapokufa na kufufuliwa.—Ona Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!, ukurasa wa 24, fungu la 4.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki