-
Latvia2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Mapainia hao wa mapema walitia ndani angalau ndugu kumi kutoka Ujerumani waliofika Latvia kusaidia kufanya kazi. Mmoja wao ni Johannes Berger, ambaye wakati huo alikuwa na umri wa miaka 22. Aliandika hivi: “Mapainia walipofika katika jiji la mgawo wao, walianza kwa kutoa hotuba za watu wote. Hivyo, tulitoa hotuba katika karibu majiji yote ya Latvia. Katika jiji la Sloka, tulikodi jumba la sinema, nami nilitoa hotuba kila Jumatatu (Siku ya 1) wakati wa majira ya baridi kali. Watu walitoka mbali huku wakiendesha farasi wao wadogo.” Akikumbuka nyakati hizo, anaongeza hivi: “Nilikuwa na mapendeleo mengi ya utumishi, ingawa sikuwa na elimu nyingi.”
-
-
Latvia2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Mwaka wa 1929, serikali ilisikiliza madai ya kanisa na kuwafukuza makolpota Wajerumani kutoka Latvia.
-