Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ‘Mkashangilie Daima kwa Ajili ya Hivi Niviumbavyo’
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Kumtumaini “Mungu wa Bahati Nzuri”

      13, 14. Ni mazoea gani yanayoonyesha kwamba watu wa Mungu wamemwacha, nao watapatwa na jambo gani?

      13 Sasa unabii wa Isaya unaelekezwa tena kwa wale ambao wamemwacha Yehova na kudumu katika ibada ya sanamu. Unasema hivi: “Ninyi mmwachao BWANA, na kuusahau mlima wangu mtakatifu, na kuandika meza kwa ajili ya Bahati [“mungu wa Bahati Nzuri,” “NW”], na kuijazia Ajali [“mungu wa Ajali,” “NW”] vyombo vya divai iliyochanganyika.” (Isaya 65:11) Kwa kutandika meza ya chakula na kinywaji mbele ya “mungu wa Bahati Nzuri” na “mungu wa Ajali,” Wayahudi hawa wenye kurudi nyuma wametumbukia katika mazoea ya ibada ya sanamu ya mataifa ya kipagani.b Itakuwaje kwa wowote wanaoitumaini miungu hiyo kwa ujinga-ujinga?

      14 Yehova anawaonya wazi hivi: “Mimi nitawaandikia [“nitawajalia,” “NW”] kuuawa kwa upanga, na ninyi nyote mtainama ili kuchinjwa; kwa sababu nilipoita hamkuitika; niliponena, hamkusikia; bali mlitenda yaliyo mabaya machoni pangu, mlichagua mambo nisiyoyafurahia.” (Isaya 65:12) Kwa kutumia Kiebrania cha awali, Yehova anagonganisha maneno ‘jalia’ na “ajali” kusema kwamba wale wanaomwabudu mungu huyo wa uwongo ‘watajaliwa kuuawa kwa upanga,’ maana yake kupatwa na uharibifu. Mara nyingi Yehova amewatumia manabii wake kuwahimiza watu hao watubu, lakini wamempuuza wakaamua kwa vichwa vigumu kufanya yale wanayojua ni mabaya machoni pake. Lo, wanamwonyesha Mungu madharau yaliyoje! Onyo la Mungu litatimizwa wakati taifa hilo litakapopatwa na maangamizi makubwa mwaka wa 607 K.W.K. Huo ni wakati ambao Yehova atawaruhusu Wababiloni waharibu Yerusalemu na hekalu lake. Hapo “mungu wa Bahati Nzuri” atashindwa kuwalinda wafuasi wake wenye bidii walioko Yuda na Yerusalemu.—2 Mambo ya Nyakati 36:17.

      15. Wakristo wa kweli wanaliitikiaje onyo linalopatikana kwenye Isaya 65:11, 12?

      15 Leo Wakristo wa kweli wanatii onyo linalopatikana kwenye Isaya 65:11, 12. Wao hawaamini “Bahati Nzuri,” kana kwamba ina nguvu nyingi zinazopita zile za asili ya kibinadamu katika kuwafanyia mambo ya hisani. Wao hukataa kutapanya mali zao kwa kujaribu kumtuliza “mungu wa Bahati Nzuri,” na kwa hiyo wanaepuka namna zote za kucheza kamari. Wanasadiki kwamba wale wanaojitoa kufanya mapenzi ya mungu huyo watapoteza kila kitu hatimaye, kwani Yehova anawaambia hivi watu wa namna hiyo: ‘Nitawajalia kuuawa kwa upanga.’

  • ‘Mkashangilie Daima kwa Ajili ya Hivi Niviumbavyo’
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Akitoa maelezo juu ya mstari huo, Jerome, mtafsiri wa Biblia (aliyezaliwa katika karne ya nne W.K.) anaeleza desturi fulani ya kale iliyofuatwa na waabudu-sanamu siku ya mwisho ya mwezi wa mwisho katika mwaka wao. Aliandika hivi: “Walikuwa wakitandika meza iliyojaa aina-aina za vyakula na kikombe kilichojazwa divai tamu ili kuhakikisha kwamba mazao waliyopata mwaka jana au yale watakayopata mwaka unaokuja yataleta bahati nzuri.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki