Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Matukio Muhimu ya Mwaka Uliopita
    2011 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • Mnamo Agosti (Mwezi wa 8) 2007, kikundi cha watungaji na wataalamu wa nyimbo walialikwa kusaidia Baraza Linaloongoza katika kazi hiyo. Nyimbo zote katika kitabu cha nyimbo cha awali zilikaguliwa kwa uangalifu ili kutambua matatizo katika mafundisho, msisitizo wa maneno, na matatizo ya muziki. Ilikuwa wazi kwamba muziki fulani wa awali ulikuwa sawa lakini nyimbo zilihitaji maneno mapya. Nyimbo nyingine zilizokuwa na maneno yanayofaa zilihitaji mabadiliko makubwa katika muziki. Kisha Halmashauri ya Ufundishaji ya Baraza Linaloongoza ikaidhinisha orodha fulani ya habari zinazoweza kufikiriwa ili kutunga nyimbo kwa ajili ya mikutano ya Kikristo, makusanyiko, na programu za kuweka wakfu.

  • Matukio Muhimu ya Mwaka Uliopita
    2011 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • Kazi hiyo yote ilipokuwa ikiendelea, Baraza Linaloongoza lilichunguza kwa uangalifu sana muundo na maneno ya kila wimbo. Nyimbo kadhaa kati za zile mpya ambazo Baraza Linaloongoza halikuwa linazifahamu zilirekodiwa na waimbaji ili Baraza Linaloongoza lizisikilize na kuzichunguza. Mara tu nyimbo hizo zilipoidhinishwa, zilitumwa kwenye ofisi za tawi zinazotafsiri ili maneno yatafsiriwe na vitabu vya nyimbo katika lugha hizo vitolewe wakati mmoja na vya Kiingereza.

      Isitoshe, katika mwaka wa 2007, Baraza Linaloongoza lilipanga ili kikundi cha waimbaji kirekodi nyimbo zitakazoyasaidia makutaniko yajifunze nyimbo hizo. Kwa miaka mingi, okestra ya wajitoleaji kutoka nchi 14 imekuwa ikikutana huko Patterson, New York, mara mbili kwa mwaka ili kurekodi muziki utakaotumiwa katika programu za elimu za Mashahidi wa Yehova, kutia ndani drama, video, na muziki kwa ajili ya makusanyiko. Ndugu na dada hao waliojitoa, ambao wengi wao ni watumishi wa wakati wote, wametumia wakati na mali zao kusafiri na kurekodi muziki kwa faida ya undugu wa ulimwenguni pote. Wote ni wanamuziki stadi. Muziki ambao okestra hiyo hurekodi hutumwa kwenye ofisi za tawi ulimwenguni pote ili utumiwe katika makusanyiko na kwa ajili ya nyimbo za sauti katika lugha mbalimbali. Nyingi kati ya nyimbo hizo za sauti zilizoimbwa katika ofisi mbalimbali zinaweza kupakuliwa katika Tovuti yetu ya www.pr418.com.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki