Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yehova Amekuwa Kimbilio Langu
    Mnara wa Mlinzi—1996 | Desemba 1
    • Upesi baada ya kuolewa, kaka ya mamangu alikuja kutuzuru kutoka Marekani. Alipata kuleta mojawapo ya mabuku ya Studies in the Scriptures, lililoandikwa na Charles Taze Russell. Kilikuwa kichapo cha Wanafunzi wa Biblia, wanaojulikana sasa kama Mashahidi wa Yehova.

      Dimitris alipokifungua hicho kitabu, aliona habari aliyokuwa ametaka kujua juu yayo tangu alipokuwa mtoto, “Inakuwaje kwa mwanadamu anapokufa?” Akiwa katika shule ya sekondari alikuwa amemwuliza mwanatheolojia wa Othodoksi ya Kigiriki kuhusu habari hiyohiyo lakini hakuwa amepokea jibu lenye kuridhisha. Elezo la wazi na lenye kupatana na akili lililoandaliwa katika hicho kichapo lilimpendeza Dimitris sana hivi kwamba alienda moja kwa moja hadi mkahawa wa kijiji, ambako wanaume katika Ugiriki walikuwa na desturi ya kukusanyika. Huko alisimulia mambo aliyokuwa amejifunza kutoka katika Biblia.

      Msimamo Wetu kwa Ajili ya Kweli ya Biblia

      Kufikia wakati huo—katika miaka ya mapema ya 1920—Ugiriki ilikuwa katikati ya vita nyingine. Dimitris aliandikishwa jeshini akatumwa barani Uturuki, katika Asia Ndogo. Alijeruhiwa akatumwa nyumbani. Baada ya kupona, niliambatana naye hadi Smirna, Asia Ndogo (sasa Izmir, Uturuki). Vita ilipoisha ghafula mwaka wa 1922, ilitubidi tutoroke. Kwa hakika, tuliponyoka chupuchupu hadi Samos, katika mashua iliyoharibika vibaya. Tulipowasili nyumbani, tulipiga magoti na kumshukuru Mungu—Mungu ambaye tulikuwa tungali na ujuzi mchache tu kumhusu.

      Upesi Dimitris akapewa mgawo wa kufundisha kwenye shule katika Vathy, mji mkuu wa kisiwa hicho. Aliendelea kusoma fasihi za Wanafunzi wa Biblia, na usiku mmoja wenye mvua nyingi wawili kati yao kutoka kisiwa cha Chios walituzuru. Walikuwa wamerudi kutoka Marekani ili kutumikia wakiwa makolpota, kama vile waeneza-evanjeli wa wakati wote walivyokuwa wakiitwa wakati huo. Tuliwapa makao usiku huo, nao wakatuambia mambo mengi kuhusu makusudi ya Mungu.

      Baadaye Dimitris aliniambia hivi: “Penelope, nang’amua kwamba hii ndiyo kweli, na ni lazima niifuate. Hili lamaanisha kwamba inanibidi niache kuimba katika Kanisa Othodoksi la Kigiriki, na kwamba siwezi kuhudhuria kanisa pamoja na watoto wa shule.” Ingawa ujuzi wetu juu ya Yehova ulikuwa mchache, tamaa yetu ya kumtumikia ilikuwa yenye nguvu. Kwa hiyo nilijibu hivi: “Sitakuwa kizuizi kwako. Songa mbele tu.”

      Akaendelea kusema kwa kusitasita kidogo: “Ndiyo, lakini mwendo wetu ukidhihirika, nitapoteza kazi yangu.”

  • Yehova Amekuwa Kimbilio Langu
    Mnara wa Mlinzi—1996 | Desemba 1
    • Mume wangu, akiwa amevutiwa na ujuzi wa huyo kolpota, akauliza: “Ni vipi kwamba waweza kuitumia Biblia kwa urahisi hivyo?”

      “Sisi hujifunza Biblia kwa utaratibu,” akajibu. Akiufungua mkoba wake, alitoa kile kitabu cha funzo The Harp of God akatuonyesha jinsi ya kukitumia kitabu hicho katika funzo hilo. Tulikuwa na hamu sana ya kujifunza hivi kwamba mume wangu na mimi, yule kolpota, na wanaume wengine wawili tukaambatana mara moja na mwenye duka hadi nyumbani kwake. Yule kolpota alitolea kila mmoja wetu nakala ya kitabu The Harp of God, nasi tukaanza kujifunza mara hiyohiyo. Tuliendelea na funzo letu hadi kupita sana usiku wa manane, kisha alfajiri ilipokaribia, tukaanza kujifunza nyimbo zilizoimbwa na Wanafunzi wa Biblia.

  • Yehova Amekuwa Kimbilio Langu
    Mnara wa Mlinzi—1996 | Desemba 1
    • Baadaye katika kiangazi hicho mume wangu nami tukaonyesha wakfu wetu kwa ubatizo wa maji.

  • Yehova Amekuwa Kimbilio Langu
    Mnara wa Mlinzi—1996 | Desemba 1
    • Karibu na wakati huo Dimitris aliachishwa kazi yake ya kufundisha, na kwa sababu ya ubaguzi dhidi yetu, ilikuwa karibu haiwezekani kupata kazi. Lakini kwa kuwa niliweza kushona nguo na Dimitris alikuwa stadi wa kupaka rangi, tuliweza kujiruzuku. Mwaka wa 1928 mume wangu, pamoja na ndugu Wakristo wengine wanne katika Samos, walihukumiwa kifungo cha miezi miwili gerezani kwa sababu ya kuhubiri habari njema. Nikiwa Mwanafunzi wa Biblia pekee aliye huru, niliweza kuwaandalia chakula gerezani.

  • Yehova Amekuwa Kimbilio Langu
    Mnara wa Mlinzi—1996 | Desemba 1
    • Ili kukabiliana kifedha, mume wangu aliuza uwanja ili niweze kuendelea na tiba.

  • Yehova Amekuwa Kimbilio Langu
    Mnara wa Mlinzi—1996 | Desemba 1
    • Upesi baada ya hapo, mwangalizi asafiriye alituzuru. Alisikitika sana kuniona nikiwa katika hali hiyo na Dimitris akiwa bila kazi. Kwa fadhili alitusaidia kufanya mipango ya kuishi Mytilene kwenye kisiwa cha Lesbos. Tulihamia huko mwaka wa 1934, na Dimitris akaweza kupata kazi ya kuajiriwa.

  • Yehova Amekuwa Kimbilio Langu
    Mnara wa Mlinzi—1996 | Desemba 1
    • Mume wangu alitumikia vifungo vya gerezani vilivyojumlika kuwa karibu muda wa mwaka mmoja. Tulipoanza siku yetu ya huduma, kwa kawaida tulipangia kupisha usiku kwenye kituo cha polisi tukiwa tumekamatwa. Hata hivyo Yehova hakutuacha kamwe. Sikuzote aliandaa moyo mkuu na nguvu zilizohitajiwa ili kuvumilia.

  • Yehova Amekuwa Kimbilio Langu
    Mnara wa Mlinzi—1996 | Desemba 1
    • Hata hivyo, mume wangu alipokuwa gerezani, ilinibidi nipitie eneo hilo ili kumtembelea. Siku moja yenye mvua nyingi mwanamke fulani alinialika nyumbani kwake ili kuniuliza ni kwa nini mume wangu alikuwa gerezani. Nilieleza kwamba ilikuwa kwa sababu ya kuhubiri habari njema ya Ufalme wa Mungu na kwamba alikuwa akiteseka sawa tu na vile Kristo alivyokuwa ameteseka.

  • Yehova Amekuwa Kimbilio Langu
    Mnara wa Mlinzi—1996 | Desemba 1
    • Katika miaka ambayo imepita Yehova amebariki jitihada za mume wangu na zangu za kumtumikia Yeye. Wale Mashahidi wachache sana wa Samos katika miaka ya 1920 wameongezeka wakawa makutaniko mawili na kikundi kimoja kukiwa na wahubiri wapatao 130. Na kwenye kisiwa cha Lesbos, kuna makutaniko manne na vikundi vitano vinavyotia ndani wapiga-mbiu 430 wa Ufalme. Mume wangu alipiga mbiu ya Ufalme wa Mungu kwa bidii hadi kifo chake mwaka wa 1977. Ni pendeleo lililoje kuona wale tuliowasaidia wangali wakiendelea kwa bidii katika huduma! Kwani, pamoja na watoto wao, wajukuu wao, na vitukuu wao, wao wanafanyiza umati mkubwa unaomwabudu Yehova kwa muungano!

  • Yehova Amekuwa Kimbilio Langu
    Mnara wa Mlinzi—1996 | Desemba 1
    • Pamoja na mume wake mwaka wa 1955

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki