Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Je! Ni Kawaida Kuhisi Hivi?
    Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa
    • Kuharibikiwa Mimba na Kuzaa Mtoto Mfu—Huzuni ya Mama

      Ingawa alikuwa na watoto wengine tayari, Monna alikuwa akitazamia kwa hamu kuzaliwa kwa mtoto wake mwingine. Hata kabla ya yeye kuzaliwa, alikuwa mtoto mchanga “aliyecheza naye, kuongea naye, na kuotea ndoto.”

      Ile kawaida ya kupata kifungo kati ya mama na mtoto asiyezaliwa ilikuwa yenye nguvu. Yeye aendelea hivi: “Rachel Anne alikuwa mtoto mchanga aliyepiga teke vitabu kutoka tumboni pangu [akiwa bado hajazaliwa], alifanya nikose usingizi usiku. Ningali naweza kukumbuka yale mateke madogo ya kwanza, kama vile midukuo ya upendo, yenye uanana. Kila wakati aliposonga, nilijawa na upendo mwingi. Nilimjua vizuri sana hivi kwamba nilijua alipokuwa akiumwa, alipokuwa mgonjwa.”

      Monna aendelea na simulizi lake hivi: “Daktari hakuniamini mpaka kulipokuwa kumechelewa mno. Aliniambia niache kuwa na wasiwasi. Naamini nilihisi alipokufa. Yeye aligeuka tu ghafula na kwa nguvu. Siku iliyofuata alikuwa amekufa.”

      Ono la Monna si tukio lisilo la kawaida. Kulingana na watunga-vitabu Friedman na Gradstein, katika kitabu chao Surviving Pregnancy Loss, karibu wanawake milioni moja kwa mwaka katika Marekani pekee huharibikiwa mimba. Bila shaka, hesabu ya ulimwenguni pote ni wengi zaidi.

      Mara nyingi watu hukosa kung’amua kwamba kuharibikiwa mimba au kuzaa mtoto mfu ni msiba kwa mwanamke na ni mmoja akumbukao—labda muda wote wa maisha yake. Kwa kielelezo, Veronica, ambaye amezeeka sasa, akumbuka kuharibikiwa kwake mimba mara kadhaa na hasa akumbuka yule mtoto mchanga mfu aliyemzaa, aliyekuwa hai hadi mwezi wa tisa na kuzaliwa akiwa na uzani wa kilo sita. Alimbeba akiwa amekufa ndani yake kwa yale majuma mawili ya mwisho. Alisema hivi: “Kumzaa mtoto mfu ni jambo mbaya sana kwa mama.”

      Maitikio ya akina mama hawa waliokata tamaa hayaeleweki sikuzote, hata na wanawake wengine. Mwanamke fulani aliyekuwa amepoteza mtoto wake kupitia mimba iliyoharibika aliandika hivi: “Yale ambayo nimejifunza kwa njia yenye maumivu sana ni kwamba kabla ya hilo kunipata, kwa kweli sikuwa na wazo lolote kuhusu yale ambayo marafiki zangu walilazimika kuvumilia. Sikugusika moyo upesi wala kuelewa vema hali yao kama vile nionavyo kwamba watu hawagusiki moyo wala kuelewa vema hali yangu.”

      Tatizo jingine kwa mama anayehuzunika ni kuona kwamba mume wake hahisi jinsi yeye anavyohisi juu ya hasara hiyo. Mke mmoja alieleza jambo hilo hivi: “Nilikatishwa tamaa kabisa na mume wangu wakati huo. Kulingana na maoni yake, kwa kweli hakukuwa na mimba yoyote. Hakuweza kuhisi ile huzuni niliyokuwa nikihisi. Alikuwa mwenye kusikitikia sana hofu zangu lakini si mwenye kusikitikia huzuni yangu.”

      Labda itikio hilo ni la asili kwa mume—yeye hawi na kifungo kilekile cha kimwili na cha kihisiamoyo (pamoja na kijusi) kama vile mke wake mjamzito huwa nacho. Hata hivyo, anahisi hasara fulani. Na ni muhimu kwamba mume na mke wang’amue kwamba wanateseka pamoja, ingawa ni kwa njia tofauti-tofauti. Wao wapaswa washiriki huzuni yao pamoja. Mume akificha huzuni yake, huenda mke wake akafikiri kwamba yeye hakugusika moyo upesi na hali hiyo. Kwa hiyo shirikini pamoja machozi, mawazo, na makumbatio yenu. Onyesheni kwamba mnahitajiana zaidi ya wakati mwingine wowote. Ndiyo, waume, onyesheni hisia-mwenzi yenu.

  • Je! Ni Kawaida Kuhisi Hivi?
    Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa
    • Ugonjwa wa Kifo cha Ghafula cha Kitoto—Kukabili Hiyo Huzuni

      Kifo cha ghafula cha mtoto mchanga ni msiba wenye kufadhaisha. Siku moja mtoto mchanga aonekanaye kuwa wa kawaida, mwenye afya nzuri ashindwa kuamka. Hilo halitazamiwi hata kidogo, kwani ni nani awaziaye kwamba kitoto au mtoto yeyote atakufa kabla ya wazazi wake? Mtoto mchanga ambaye amekuja kupendwa sana na mamake kwa ghafula awa chanzo cha huzuni kubwa.

      Hisia za kuwa na hatia zaanza kuja kwa wingi. Huenda wazazi wakahisi wao ndio wa kulaumiwa kwa ajili ya kifo hicho, kana kwamba kilisababishwa na uzembe fulani. Wanajiuliza, ‘Tungaliweza kufanya nini ili kukizuia?’b Katika hali nyingine, huenda mume, bila msingi wowote, akamlaumu mke wake bila kujua. Alipoenda kazini, yule mtoto mchanga alikuwa hai na mwenye afya nzuri. Alipofika nyumbani, mtoto huyo mchanga alikuwa amekufa kitandani mwake! Mke wake alikuwa akifanya nini? Yeye alikuwa wapi wakati huo? Ni lazima maswali hayo yenye kusumbua yajibiwe ili yasisababishe mkazo juu ya ndoa.

      Hali zisizotazamiwa na zisizoweza kuonwa kimbele zilisababisha msiba huo. Biblia husema: “Nikarudi, na kuona chini ya jua, ya kwamba si wenye mbio washindao katika michezo, wala si walio hodari washindao vitani, wala si wenye hekima wapatao chakula, wala si watu wa ufahamu wapatao mali, wala wenye ustadi wapatao upendeleo; lakini wakati na bahati [“tukio lisilotazamiwa,” NW] huwapata wote.”—Mhubiri 9:11.

      Wengine wanaweza kusaidiaje wakati familia inapofiwa na mtoto mchanga? Mama mmoja aliyefiwa aliitikia hivi: “Rafiki mmoja alikuja akaisafisha nyumba bila mimi kusema neno lolote. Wengine walitupikia chakula. Baadhi yao walisaidia kwa kunikumbatia tu—bila kusema maneno yoyote, kumbatio tu. Sikutaka kuongea juu yalo. Sikutaka kueleza tena na tena juu ya kile kilichotendeka. Sikuhitaji maswali ya kupeleleza, kana kwamba nilikuwa nimekosa kufanya jambo fulani. Nilikuwa ndiye mama [yake]; ningalifanya jambo lolote lile kumwokoa mtoto wangu mchanga.”

  • Je! Ni Kawaida Kuhisi Hivi?
    Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa
    • Hili laungwa mkono na kisa cha mama fulani, Anne, aliyekuwa amefiwa na mtoto wake mchanga Rachel kutokana na SIDS (Ugonjwa wa Kifo cha Ghafula cha Kitoto). Mume wake alieleza hivi: “Jambo la kushangaza ni kwamba wala Anne wala mimi hatukulia kwenye maziko. Wengine wote walikuwa wakitoa machozi.” Anne aliitikia hilo hivi: “Ndiyo, lakini nimelia vya kutosha sana kwa ajili ya sote wawili. Nafikiri niliathiriwa kwelikweli majuma machache baada ya msiba huo, siku moja nilipokuwa peke yangu nyumbani hatimaye. Nililia siku nzima. Lakini naamini hilo lilinisaidia. Nilisikia nafuu kwa kufanya hivyo. Nililazimika kuomboleza kifo cha mtoto wangu mchanga. Naamimi kwelikweli kwamba wapaswa kuacha watu wanaohuzunika watoe machozi. Ingawa ni itikio la asili kwa wengine kusema, ‘Usilie,’ kwa kweli hilo halisaidii.”

      Jinsi Wengine Huitikia

      Wengine wameitikiaje wanapohuzunishwa na kifo cha mpendwa? Kwa kielelezo, fikiria Juanita. Yeye ajua zinavyokuwa hisia wakati wa kufiwa na mtoto mchanga. Yeye alikuwa ameharibikiwa mimba mara tano. Sasa akawa mjamzito tena. Basi wakati aksidenti ya gari ilipomlazimisha alazwe hospitalini, ni wazi yeye alikuwa na wasiwasi. Majuma mawili baadaye alipatwa na utungu wa kuzaa—kabla ya wakati wake. Muda mfupi baadaye Vanessa mdogo akazaliwa—mwenye uzani zaidi kidogo ya gramu mia tisa. “Nilisisimuka sana,” Juanita akumbuka. “Hatimaye nikawa mama!”

      Lakini furaha yake ilikuwa ya muda mfupi tu. Siku nne baadaye Vanessa alikufa. Juanita akumbuka hivi: “Nilihisi utupu sana. Nilitwaliwa hali yangu ya kuwa mama. Nilihisi kutokuwa kamili. Iliumiza sana kuja nyumbani kwenye chumba tulichokuwa tumemtayarishia Vanessa na kuona zile shati ndogo za kuvaliwa ndani nilizokuwa nimemnunulia. Kwa miezi kadhaa iliyofuata, nilikumbuka upya ile siku ya kuzaliwa kwake. Sikutaka kushirikiana na yeyote yule.”

      Je! hilo ni itikio la kupita kiasi? Huenda ikawa vigumu kwa wengine kuelewa, lakini wale ambao, kama vile Juanita, wamepitia hali hiyo wanaeleza kwamba walihuzunikia mtoto wao mchanga sawa na vile ambavyo wangehuzunikia mtu fulani aliyekuwa ameishi kwa muda fulani. Wanasema kwamba, muda mrefu kabla ya mtoto kuzaliwa, huyo huwa anapendwa na wazazi wake. Kuna kifungo cha pekee pamoja na mama. Mtoto huyo mchanga anapokufa, mama huhisi kwamba mtu halisi amekufa. Na hilo ndilo jambo ambalo wengine wanahitaji kuelewa.

      Jinsi Kasirani na Kuhisi Una Hatia Kwaweza Kukuathiri

      Mama mwingine alionyesha hisia zake alipoambiwa kwamba mwana wake wa miaka sita alikuwa amekufa ghafula kwa sababu ya tatizo la moyo alilozaliwa nalo. “Nilipatwa na mfululizo wa maitikio—ganzi, kutoamini, kuhisi una hatia, na kasirani kuelekea mume wangu na daktari kwa ajili ya kutong’amua jinsi hali yake ilivyokuwa mbaya sana.”

  • Je! Ni Kawaida Kuhisi Hivi?
    Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa
    • Ile kawaida ya kuhuzunika kwa muda mrefu ya akina mama wengi huunga mkono yale ambayo wastadi wengi husema, kwamba kifo cha mtoto huacha pengo la daima maishani mwa wazazi, hasa mama.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki