-
Guyana2005 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Kutaniko la Charity pia lina Jumba jipya la Ufalme.
-
-
Guyana2005 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
“Wakati huo, mimi na Eustace tuliona kwamba kikundi hicho kilihitaji Jumba la Ufalme. Kwa hiyo, baada ya kukadiria gharama na kuzungumzia mradi huo pamoja na wengine, tulianza kujenga. Ndugu yangu Cecil Baird alitoa vifaa vingi vilivyotumiwa katika ujenzi, nao wengine wakasaidia kwa kufanya kazi. Ujenzi ulianza Juni 1992 na kuisha mapema mwaka uliofuata, kabla tu ya Ukumbusho. Tulishangaa kuwaona watu 800 waliokuja kusikiliza hotuba ambayo ilitolewa na Gordon Daniels, mwangalizi anayesafiri.
“Kikundi cha Baramita kimekuwa kutaniko tangu Aprili 1, 1996, na Jumba la Ufalme liliwekwa wakfu Mei 25, mwaka huohuo. Tangu wakati huo jumba hilo limepanuliwa na sasa linatoshea watu zaidi ya 500, na ndugu wanaweza kulitumia kwa makusanyiko ya mzunguko na ya pekee.
-