-
Guyana2005 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Wakati huohuo, huko Georgetown, mji mkuu wa Guyana, Edward Phillips alipata vichapo vya Wanafunzi wa Biblia wa Kimataifa, kama Mashahidi wa Yehova walivyoitwa wakati huo. Kwa kuwa Phillips alitaka sana kuwaeleza wengine mambo aliyokuwa akijifunza, aliwakusanya jamaa na marafiki nyumbani kwake kwa mazungumzo ya ukawaida na ya kirafiki kuhusu Biblia. Mnamo mwaka wa 1908 aliandika barua na kuomba mwakilishi wa Watch Tower Society atumwe Guyana, ambayo wakati huo iliitwa Guiana ya Uingereza.a Miaka minne baadaye, Evander J. Coward alifika Guyana na kutoa hotuba za Biblia kwa maelfu ya watu waliokusanyika kwenye kumbi za mji wa Georgetown na New Amsterdam.
Frederick, mwana wa Phillip, anakumbuka ziara ya Coward. Anaandika: “Baada ya muda mfupi, Ndugu Coward alijulikana sana mjini Georgetown, na kwa sababu ya mahubiri yake, watu wenye kupendezwa walianza kujiunga na kikundi chetu cha Wanafunzi wa Biblia. Wakati huo tulijifunza kitabu kuhusu kusudi la Mungu (The Divine Plan of the Ages), kitabu kuhusu uumbaji mpya (The New Creation), na vitabu vinginevyo. Baada ya muda mfupi hakukuwa na nafasi ya kutosha katika nyumba yetu, hivyo mnamo mwaka wa 1913, tukakodi chumba fulani cha juu kwenye jengo la Somerset House mjini Georgetown. Mikutano ya kutaniko ilifanywa katika chumba hicho hadi mwaka wa 1958.”
-
-
Guyana2005 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha katika ukurasa wa 138]
Jengo la Somerset House mjini Georgetown, Guyana, ambamo mikutano ilifanyiwa kuanzia mwaka wa 1913 hadi 1958
-