Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ‘Utaendelea Kuishi’ Kama Yeremia?
    Mungu Asema Nasi Kupitia Yeremia
    • Mambo yaliyoonwa yanaonyesha kwamba kuna faida kubwa kujishughulisha na utumishi wa Mungu na kushiriki kikamili katika utendaji wa kiroho. Kwa mfano, dada mmoja Shahidi  anayeshirikiana na kutaniko la Kichina anasema: “Upainia umenipa kusudi maishani. Nikiwa mseja, ninakuwa na shughuli nyingi, mambo mengi ya kufanya, na hivyo sijioni mpweke. Kila siku mimi huhisi nimeridhika ninapoona jinsi huduma yangu inavyowasaidia watu. Hilo hunipa shangwe kubwa.” Painia mwenye umri wa miaka 38 anasema: “Nafikiri siri ya kuwa mwenye furaha ni kuwa na maoni yanayofaa kuhusu hali yoyote ile maishani.” Dada mmoja mseja huko Ulaya Kusini alisema hivi waziwazi: “Maisha yangu hayakwenda nilivyokusudia, hata hivyo, nina furaha nami nitaendelea hivyo.”

      Picha katika ukurasa wa 97

      12, 13. (a) Tunapaswa kuwa na maoni gani yanayofaa kuhusu useja na ndoa? (b) Maisha na shauri la Paulo yanakazia nini kuhusu useja?

      12 Inawezekana kwamba Yeremia aliona kuwa maisha yake hayakwenda alivyotazamia alipokuwa kijana? Huenda alitambua pia kwamba hata kwa wale waliofunga ndoa na kuwa na watoto, mambo hayakwenda walivyotazamia. Dada mmoja painia nchini Hispania alisema: “Najua watu waliofunga ndoa walio na furaha na wengine wasio na furaha. Kujua hilo hunisaidia kuona kwamba furaha yangu haitegemei ikiwa nitafunga ndoa au hapana.” Bila shaka, kutokana na kisa cha Yeremia na wengine wengi, ni wazi kwamba mseja anaweza kuwa na maisha mazuri, yenye kuridhisha, na yenye furaha.

      “Mimi huthamini sana pindi ninazokuwa peke yangu. Ninaweza kuongea na Yehova katika sala. Ninaweza kutafakari na kujifunza kibinafsi bila kukengeushwa fikira. . . . Useja umechangia pakubwa shangwe yangu.”—Babette

  • ‘Utaendelea Kuishi’ Kama Yeremia?
    Mungu Asema Nasi Kupitia Yeremia
Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki