Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kuhukumu Kahaba Mwenye Sifa Mbaya
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • Kahaba Apanda Hayawani

      13. Ni mwono gani wenye kushangaza anaoona Yohana wakati malaika anapompeleka katika jangwa kwa nguvu ya roho?

      13 Unabii hufumbua nini zaidi kwa habari ya kahaba mkubwa na msiba wake? Kama Yohana anavyosimulia sasa, mandhari nyingine iliyo wazi sana yaonekana: “Na yeye [malaika] akapeleka mimi mbali kwa nguvu ya roho kuingia ndani ya jangwa. Na mimi nikaona mwanamke akiwa ameketi juu ya hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu ambaye alikuwa amejaa majina ya kufuru na ambaye alikuwa na vichwa saba na pembe kumi.”—Ufunuo 17:3, NW.

      14. Ni kwa nini inafaa kwamba Yohana alipelekwa jangwani?

      14 Ni kwa nini Yohana anapelekwa ndani ya jangwa? Tamko la mapema zaidi la uangamivu dhidi ya Babuloni wa kale lilielezwa kuwa “dhidi ya jangwa la bahari.” (Isaya 21:1, 9, NW) Hilo lilitoa onyo linalostahili kwamba, ujapokuwa ulinzi wake mwingi wa kimaji, Babuloni wa kale angekuwa ukiwa usio na uhai. Inafaa, basi, kwamba yampasa Yohana apelekwe katika njozi yake kwenye jangwa akaone msiba wa Babuloni Mkubwa. Yeye pia lazima awe ukiwa na utupu. (Ufunuo 18:19, 22, 23) Ingawa hivyo, Yohana anashangazwa na anachoona nje kule. Kahaba mkubwa hayuko peke yake! Yeye anaketi juu ya dubwana la hayawani-mwitu!

      15. Ziko tofauti gani kati ya hayawani-mwitu wa Ufunuo 13:1 na yule wa Ufunuo 17:3?

      15 Hayawani-mwitu huyu ana vichwa saba na pembe kumi. Basi, je! yeye ni hayawani-mwitu yule yule ambaye Yohana aliona mapema zaidi, ambaye pia alikuwa na vichwa saba na pembe kumi? (Ufunuo 13:1) La, ziko tofauti. Hayawani-mwitu huyu ni rangi-nyekundu-nyangavu na, tofauti na hayawani-mwitu aliyetangulia, hasemwi kuwa ana mataji. Badala ya yeye kuwa na majina ya kufuru juu ya vichwa vyake saba tu, yeye ‘anajaa majina ya kufuru.’ Hata hivyo, lazima pawe na uhusiano kati ya hayawani-mwitu mpya na yule aliyetangulia; mifanano kati yao ni mingi mno kuwa ya nasibu.

      16. Ni nini utambulisho wa huyo hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu, na imetaarifiwa nini kwa habari ya kusudi lake?

      16 Basi, hayawani-mwitu mpya rangi-nyekundu-nyangavu ni nini? Yeye ni lazima awe ule mfano wa hayawani-mwitu ambao ulitokezwa kwa himizo la hayawani-mwitu Uingereza-Amerika aliyekuwa na pembe mbili mithili ya mwana-kondoo. Baada ya mfano huo kuwa umefanywa, huyo hayawani-mwitu mwenye pembe mbili aliruhusiwa kuupa pumzi huo mfano wa hayawani-mwitu. (Ufunuo 13:14, 15) Yohana anaona sasa mfano ulio hai, unaopumua. Ni picha ya tengenezo la Ushirika wa Mataifa ambalo hayawani-mwitu mwenye pembe mbili alileta kwenye uhai katika 1920. Rais Wilson wa U.S. alikuwa na njozi ya kwamba Ushirika huo “ungekuwa baraza la kutolea watu wote haki na kufutilia mbali milele tisho la vita.” Lilipofufuliwa baada ya vita ya ulimwengu ya pili likiwa Umoja wa Mataifa, kusudi la katiba yalo lilikuwa “kudumisha amani na usalama wa kimataifa.”

      17. (a) Ni katika njia gani huyo hayawani-mwitu wa ufananisho rangi-nyekundu-nyangavu anajaa majina ya kufuru? (b) Ni nani anayempanda huyo hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu? (c) Dini ya Kibabuloni ilijifungamanishaje na Ushirika wa Mataifa na mwandamizi wao pale pale mwanzoni?

      17 Ni katika njia gani huyu hayawani-mwitu wa ufananisho anajaa majina ya kufuru? Katika njia ya kwamba wanadamu wameisimamisha sanamu hii ya kuabudiwa na mataifa mengi ikiwa kibadala cha Ufalme wa Mungu—itimize jambo ambalo Mungu husema ni Ufalme wake pekee unaoweza kutimiza. (Danieli 2:44; Mathayo 12:18, 21) Ingawa hivyo, jambo lenye kutokeza kuhusu njozi ya Yohana ni kwamba, Babuloni Mkubwa anapanda hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu. Kupatana na ukweli wa unabii, dini ya Kibabuloni, hasa katika Jumuiya ya Wakristo, imejifungamanisha yenyewe na Ushirika wa Mataifa na mwandamizi wao. Mapema kama Desemba 18, 1918, shirika ambalo sasa linajulikana kuwa Baraza la Taifa la Makanisa ya Kristo katika Amerika lilipitisha julisho-wazi lililojulisha wazi kwa sehemu hivi: “Ushirika kama huo si manufaa ya kisiasa tu; badala ya hivyo ni wonyesho wa kisiasa wa Ufalme wa Mungu duniani. . . . Kanisa linaweza kutoa roho ya nia njema, ambayo bila hiyo hakuna Ushirika wa Mataifa unaoweza kudumu. . . . Ushirika wa Mataifa una mizizi katika Gospeli. Kama Gospeli, lengo lao ni ‘amani duniani, nia njema kuelekea wanadamu.’”

      18. Viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo walionyeshaje uungaji-mkono wao kwa Ushirika wa Mataifa?

      18 Katika Januari 2, 1919, San Fransisco Chronicle lilikuwa na kichwa kikuu cha habari kwenye ukurasa wa kwanza: “Papa Asihi Ukubaliwe Ushirika wa Maitafa wa Wilson.” Katika Oktoba 16, 1919, ombi rasmi lililotiwa sahihi na makasisi wa vikundi mashuhuri 14,450 lilitolewa kwenye Seneti ya U.S., kuhimiza baraza hilo ‘liidhinishe mwafaka wa amani wa Paris uliotia ndani agano la ushirika wa mataifa.’ Ingawa Seneti ya U.S. ilishindwa kuidhinisha mwafaka huo, viongozi wa Jumuiya ya Wakristo waliendelea kufanya kampeni kwa ajili ya huo Ushirika. Na Ushirika huo ulizinduliwaje? Habari iliyopelekwa kutoka Uswisi, yenye tarehe ya Novemba 15, 1920, ilisomwa hivi: “Kufunguliwa kwa kusanyiko la kwanza la Ushirika wa Mataifa kulitangazwa kwenye saa tano asubuhi hii kwa kupigwa kengele zote za kanisa katika Geneva.”

      19. Wakati hayawani-mwitu alipotokea, jamii ya Yohana ilichukua mwendo gani wa tendo?

      19 Je! jamii ya Yohana, kikundi pekee duniani ambacho kilikubali kwa hamu nyingi Ufalme wa Kimesiya uliokuwa ukija, kilishiriki pamoja na Jumuiya ya Wakristo katika kumpa shikamoo huyo hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu? Mbali kabisa na hilo! Jumapili, Septemba 7, 1919, mkusanyiko wa watu wa Yehova kwenye Sida Pointi, Ohaiyo, ulikuwa na hotuba ya watu wote iliyokuwa na kichwa “Tumaini kwa Binadamu Wenye Kutaabika.” Siku iliyofuata, Star-Journal ya Sandusky iliripoti kwamba J. F. Rutherford, katika kuhutubia watu karibu 7,000, alikuwa “amesisitiza kwamba kutopendezwa kwa Bwana ni hakika kutajilia Ushirika . . . kwa sababu viongozi wa kidini—Wakatoliki na Waprotestanti—wakidai kuwa wawakilishi wa Mungu, wameacha mpango wake na wakakubali Ushirika wa Mataifa, wakiushangilia kuwa wonyesho wa kisiasa wa ufalme wa Kristo duniani.”

      20. Ni kwa sababu gani ilikuwa kufuru viongozi wa kidini kushangilia Ushirika wa Mataifa kuwa “wonyesho wa kisiasa wa Ufalme wa Mungu duniani”?

      20 Ushinde wenye kusikitisha sana wa Ushirika wa Mataifa ulipaswa kuashiria viongozi wa kidini kwamba vyombo hivyo vyenye kufanywa na mwanadamu si sehemu ya Ufalme wa Mungu duniani. Ni kufuru kama nini kudai hivyo! Hufanya ionekane kana kwamba Mungu alishiriki kufanyiza Ushirika wa Mataifa ambao ni kazi ya ovyo sana. Kwa habari ya Mungu “utendaji wake ni mkamilifu.” Ufalme wa Yehova wa kimbingu chini ya Kristo—wala si muungano wa wanasiasa wenye kuzozana, wengi wao wakiwa hawaitikadi kuwako kwa Mungu—ndiyo njia ambayo kwayo yeye ataleta amani na kufanya penzi lake lifanywe duniani kama katika mbingu.—Kumbukumbu 32:4; Mathayo 6:10, NW.

      21. Ni nini kinachoonyesha kwamba kahaba mkubwa anaunga mkono na kusifu mno mwandamizi wa Ushirika, Umoja wa Mataifa?

      21 Namna gani mwandamizi wa Ushirika, Umoja wa Mataifa? Tangu mwanzo wao, baraza hili limekuwa na kahaba akilipanda mgongoni mwalo, akishirikiana nalo waziwazi na akijaribu kuongoza liendako. Mathalani, katika ukumbusho wa mwaka wao wa 20 katika Juni 1965, wawakilishi wa Kanisa Katoliki la Roma na Kanisa Orthodoksi la Mashariki, pamoja na Waprotestanti, Wayahudi, Wahindu, Wabuddha, na Waislamu—waliosemekana kuwakilisha idadi ya watu wa dunia elfu mbili milioni—walikusanyika katika San Francisco kusherehekea uungaji-mkono na usifaji wao wa UM. Alipozuru UM Oktoba 1965, Papa Paul 6 alieleza habari zao kuwa “hilo tengenezo la kimataifa kubwa zaidi ya yote” na akaongeza: “Vikundi vya watu wa dunia vinategemea Umoja wa Mataifa kuwa ndilo tumaini la mwisho la itifaki na amani.” Mgeni mwingine wa kipapa, Papa John Paul 2, akihutubia UM katika Oktoba 1979, alisema: “Mimi natumaini Umoja wa Mataifa utadumu daima ukiwa ndilo baraza kuu la amani na haki.” Kwa uwazi sana, huyo papa alimtaja Yesu Kristo na Ufalme wa Mungu mara chache sana katika hotuba yake. Wakati wa ziara yake United States katika Septemba 1987, kama ilivyoripotiwa na The New York Times, “John Paul alisema kirefu juu ya daraka chanya la Umoja wa Mataifa katika kuendeleza . . . ‘ushirikiano mpya wa ulimwenguni pote.’”

      Jina, Fumbo

      22. (a) Ni hayawani wa aina gani ambaye kahaba mkubwa amechagua kupanda? (b) Yohana anaelezaje habari ya kahaba wa ufananisho Babuloni Mkubwa?

      22 Karibuni mtume Yohana atajifunza kwamba kahaba mkubwa amechagua kupanda hayawani hatari. Ingawa hivyo, kwanza uangalifu wake wageukia Babuloni Mkubwa mwenyewe. Yeye amepambwa kitajiri, lakini, oh, jinsi anavyokirihisha! “Na huyo mwanamke alikuwa amepambwa zambarau na nyekundu-nyangavu na alikuwa amerembwa kwa dhahabu na jiwe la thamani na lulu na katika mkono wake alikuwa na kikombe cha dhahabu ambacho kilikuwa kimejaa vitu vya kunyarafisha na vitu visivyo safi vya uasherati wake. Na juu ya kipaji cha uso wake paliandikwa jina, fumbo: ‘Babuloni Mkubwa, mama ya makahaba na ya vitu vya kunyarafisha vya dunia.’ Na mimi nikaona kwamba mwanamke alikuwa amelewa damu ya watakatifu na damu ya mashahidi wa Yesu.”—Ufunuo 17:4-6a, NW.

      23. Ni jina gani kamili la Babuloni Mkubwa, na maana yalo ni nini?

      23 Kama ilivyokuwa desturi katika Roma ya kale, malaya huyu anatambuliwa kwa jina lililo juu ya kipaji cha uso wake.d Ni jina refu: “Babuloni Mkubwa, mama ya makahaba na ya vitu vya kunyarafisha vya dunia.” Jina hilo ni “fumbo,” jambo fulani lenye maana iliyofichwa. Lakini kwa wakati wa Mungu fumbo hilo litafafanuliwa. Kwa kweli, malaika anampa Yohana habari ya kutosha kuruhusu watumishi wa Yehova leo wafahamu umaana kamili wa jina hili lenye maelezo. Sisi tunatambua Babuloni Mkubwa kuwa dini bandia yote. Yeye ndiye “mama ya makahaba” kwa sababu dini bandia zote moja moja katika ulimwengu, kutia ndani mafarakano katika Jumuiya ya Wakristo, ni kama mabinti wake, zikimwiga yeye katika kufanya ukahaba wa kiroho. Yeye pia ni mama ya “vitu vya kunyarafisha” katika njia ya kwamba yeye amezaa wazao wenye makuruhu kama vile ibada ya sanamu, uwasiliano na roho, kupiga ramli, unajimu, uaguzi wa kutazama vitanga vya mikono, kudhabihu binadamu, umalaya wa hekaluni, ulevi katika kuheshimu miungu bandia, na mazoea mengine machafu.

      24. Ni kwa sababu gani inafaa kwamba Babuloni Mkubwa amevalia “zambarau na rangi-nyekundu-nyangavu” na “amepambwa kwa dhahabu na jiwe la thamani na lulu”?

      24 Babuloni Mkubwa amevalia “zambarau na nyekundu-nyangavu,” rangi za jamaa ya kifalme, na “amerembwa kwa dhahabu na jiwe la thamani na lulu.” Inafaa kama nini! Fikiria tu yale majengo yote mazuri mno, sanamu-umbo na taswira azizi, aikoni zenye bei sana, na vikorokoro vingine vya kidini, pamoja na kiasi ambacho ni vigumu kuitikadi cha mali na pesa, kisichohesabika ambacho dini za ulimwengu huu zimerundika. Iwe ni katika Vatikani, katika milki ya uevanjeli wa TV ambao kitovu chayo ni United States, au katika misikiti na mahekalu yenye kuvutia ya Mashariki, Babuloni Mkubwa amerundika kama tungamo—na nyakati nyingine akapoteza—ukwasi mwingi mno.

      25. (a) Ni nini kinachofananishwa na “kikombe cha dhahabu ambacho kilijaa vitu vya kunyarafisha?” (b) Ni katika maana gani kahaba wa ufananisho amelewa?

      25 Tazama sasa alicho nacho kahaba huyu mkononi mwake. Haikosi Yohana alitweta kwa mshangao kukiona—kikombe cha dhahabu “kimejaa vitu vya kunyarafisha na vitu visivyo safi vya uasherati wake”! Hiki ndicho kikombe ambacho ndani yacho mna “divai ya kasirani ya uasherati wake” ambacho kwa hicho amefanya mataifa yote yalewe. (Ufunuo 14:8; 17:4) Kwa nje kinaonekana kuwa chenye utajiri, lakini yaliyomo ni yenye kunyarafisha, si safi. (Linga Mathayo 23:25, 26.) Ndani kina mazoea yote machafu na uwongo mwingi ambao huyo kahaba mkubwa ametumia kutongoza mataifa na kuwaleta chini ya uvutano wake. Lenye makuruhu hata kuchukiza zaidi, Yohana anaona kwamba huyo kahaba mwenyewe amelewa, amekunywa sana damu ya watumishi wa Mungu! Kwa kweli, baadaye sisi tunasoma kwamba “katika yeye ilipatikana damu ya manabii na ya watakatifu na ya wale wote ambao wamechinjwa juu ya dunia.” (Ufunuo 18:24, NW) Ni hatia ya damu kubwa mno kama nini!

      26. Kuna ithibati gani ya hatia ya damu upande wa Babuloni Mkubwa?

      26 Kwa muda wa karne zilizopita, milki ya ulimwengu ya dini bandia imemwaga damu nyingi kama bahari. Mathalani, katika Japani ya zamani za kale, mahekalu katika Kyoto yaligeuzwa kuwa ngome, na watawa-mashujaa-vita, wakiliitia “jina takatifu la Buddha,” walipigana vita mpaka barabara zikawa nyekundu kwa damu. Katika karne ya 20, viongozi wa kidini walipiga miguu wakiwa pamoja na majeshi ya nchi zao, na walichinjana, kukiwa na hasara ya angalau maisha milioni mia moja. Katika Oktoba 1987 Nixon aliyekuwa rais wa U.S. alisema: “Karne ya 20 imekuwa ndiyo yenye damu nyingi zaidi ya zote katika historia. Watu zaidi wameuawa katika vita vya karne hii kuliko katika vita vyote vilivyopiganwa kabla ya karne hii kuanza.” Dini za ulimwengu zimehukumiwa vibaya na Mungu kwa sababu ya ushiriki wazo katika yote haya; Yehova hukirihi “mikono ambayo inamwaga damu isiyo na hatia.” (Mithali 6:16, 17, NW) Mapema zaidi, Yohana alisikia kilio kutoka madhabahu: “Ni mpaka lini, Bwana Mwenye Enzi Kuu mtakatifu na wa kweli, wewe unajizuia usihukumu na kulipiza kisasi damu yetu juu ya wale ambao wanakaa juu ya dunia?” (Ufunuo 6:10, NW) Babuloni Mkubwa, mama ya makahaba na ya vitu vya kunyarafisha vya dunia, atahusika sana ujapo wakati wa kujibu swali hilo.

  • Kuhukumu Kahaba Mwenye Sifa Mbaya
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • [Picha katika ukurasa wa 244]

      “Majina ya Kufuru”

      Hayawani-mwitu mwenye pembe mbili alipoendeleza Ushirika wa Mataifa baada ya Vita ya Ulimwengu 1, hawara zake wa kidini walitafuta mara hiyo kulipa tendo hilo idhini ya kidini. Kama tokeo, tengenezo jipya la amani ‘likajawa na majina ya kufuru.’

      “Ukristo unaweza kuandaa nia njema, nguvu-msukumo inayotendesha ushrika [wa mataifa], na hivyo kugeuza mwafaka huo kutoka kipande cha karatasi tu na kuwa chombo cha ufalme wa Mungu.”—The Christian Century, U.S.A., Juni 19, 1919, ukurasa 15.

      “Wazo la Ushirika wa Mataifa ni mpanuo kuelekea mahusiano ya kimataifa wa wazo la Ufalme wa Mungu ukiwa utaratibu wa ulimwengu wa nia njema. . . . Ndicho kitu ambacho Wakristo wote husali kwa ajili yacho wanaposema, ‘Ufalme wako uje.”—The Christian Century, U.S.A., Septemba 25, 1919, ukurasa 7.

      “Saruji ya Ushirika wa Mataifa ni Damu ya Kristo.”—Dakt. Frank Crane, Mhudumu Mprotestanti, U.S.A.

      Baraza [la Taifa la Makanisa ya Kongrigeshonali] huunga mkono Agano [la Ushirika wa Mataifa] kuwa ndicho chombo pekee cha kisiasa kinachopatikana sasa ambacho kwacho Roho ya Yesu Kristo inaweza kupata mweneo mpana zaidi katika utumizi wenye mafaa kwenye mambo ya mataifa.”—The Congregationalist and Advance, U.S.A., Novemba 6, 1919, ukurasa 642.

      “Kongamano lataka Wamethodisti wote wategemeze na kuendeleza sana mawazo bora [ya Ushirika wa Mataifa] kama yanavyoonyeshwa na wazo la Mungu Baba na watoto wa Mungu wa kidunia.”—Kanisa la Kimethodisti la Wesley, Uingereza.

      “Tunapoyafikiria malengo yale, mawezekano na maazimio ya mwafaka huu, sisi tunaona kwamba una moyo wa mafundisho ya Yesu Kristo: Ufalme wa Mungu na uadilifu wake . . . Si kitu kilicho punde ya huo.”—Mahubiri ya Askofu Mkuu wa Kantabari wakati wa kufunguliwa kwa Kusanyiko la Ushirika wa Mataifa katika Geneva, Desemba 3, 1922.

      “Shirika la ule Ushirika wa Mataifa katika nchi hii lina haki takatifu ile ile kama sosaiti ya kimisheni yoyote ya ufadhili-binadamu, kwa sababu kwa wakati uliopo ndicho chombo chenye matokeo zaidi sana cha utawala wa Kristo Mwana-Mfalme wa amani miongoni mwa mataifa.”—Dakt. Garvie, mhudumu Mkongrigeshonali, Uingereza.

  • Fumbo Lenye Kutia Hofu Lafumbuliwa
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • Sura ya 34

      Fumbo Lenye Kutia Hofu Lafumbuliwa

      1. (a) Yohana anatendaje kama itikio anapoona kahaba mkubwa na mpandwaji wake mwenye kutia hofu, na kwa nini? (b) Jamii ya Yohana inatendaje leo kama itikio, matukio yanapokunjuka katika utimizo wa njozi ya kiunabii?

      TENDO-MWITIKIO la Yohana ni nini anapomwona “kahaba mkubwa” na mpandwaji wake mwenye kutia hofu? Yeye mwenyewe ajibu: “Basi, nilipoona yeye mimi nilistaajabu kwa staajabu kubwa.” (Ufunuo 17:6b, NW) Mawazo vivi hivi tu ya kibinadamu hayangeweza kutunga mwono kama huo. Hata hivyo ndio huo—mbali kule jangwani—malaya mpujufu akimpanda hayawani-mwitu wa kutisha mwenye rangi-damu-nyangavu! (Ufunuo 17:3) Jamii ya Yohana leo pia hustaajabu kwa staajabu kubwa matukio yanapokunjuka katika utimizo wa njozi ya kiunabii. Kama watu wa ulimwengu wangeweza kuiona, wao wangepaaza sauti kusema, ‘Haisadikiki!’ na watawala wa ulimwengu wangerudisha mwangwi wakisema, ‘Haifikiriki!’ Lakini njozi hiyo inakuwa uhalisi wenye kugutusha katika siku zetu. Tayari watu wa Mungu wamekuwa na ushiriki wenye kutokeza katika utimizo wa njozi hiyo, na hiyo inawahakikishia kwamba unabii huo utasonga mbele moja kwa moja mpaka upeo wao wenye kupiga butaa.

      2. (a) Katika kuitikia mshangao mkubwa wa Yohana, malaika anamwambia nini? (b) Jamii ya Yohana imefunuliwa nini, na hilo limefanywaje?

      2 Malaika anaona mshangao mkubwa wa Yohana. “Na hivyo,” Yohana aendelea, “malaika akasema kwa mimi: ‘Kwa nini wewe ulistaajabu? Mimi nitakuambia fumbo la mwanamke na la hayawani-mwitu ambaye anabeba yeye na ambaye ana vichwa saba na pembe kumi.’” (Ufunuo 17:7, NW) Aha, sasa malaika atalifumbua fumbo! Yeye amfafanulia Yohana mwenye kukodoa macho nyuso mbalimbali za njozi na matukio ya kidrama yanayokaribia kukunjuka. Hali kadhalika, inapotumikia chini ya mwelekezo wa kimalaika leo, jamiii ya Yohana yenye kutazama imefunuliwa uelewevu wa huo unabii. Je! “kufasiri si kazi ya Mungu?” Kama Yosefu mwaminifu, sisi tunaitikadi kwamba ni yake. (Mwanzo 40:8; linga Danieli 2:29, 30.) Watu wa Mungu wamewekwa kana kwamba wako katikati ya jukwaa, Yehova anapowafasiria maana ya njozi na matokeo yayo juu ya maisha zao. (Zaburi 25:14) Kwa wakati barabara, yeye amewafungulia uelewevu wao fumbo la mwanamke na hayawani-mwitu.—Zaburi 32:8.

      3, 4. (a) Ni hotuba gani ya watu wote iliyotolewa na N. H. Knorr katika 1942, nayo ilimtambulishaje hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu? (b) Ni maneno gani ambayo malaika alisema kwa Yohana yaliyozungumzwa na N. H. Knorr?

      3 Kutoka Septemba 18 kufika 20, 1942, wakati wa upeo wa Vita ya Ulimwengu 2, Mashahidi wa Yehova katika United States walikuwa na Ulimwengu Mpya wa Kitheokrasi Kusanyiko. Jiji kuu la kusanyiko, Cleveland, Ohaiyo, lilifunganishwa kwa waya za simu na majiji mengine zaidi ya 50 ya mkusanyiko, kukiwa na kilele cha hadhirina 129,699. Mahali ambako hali za wakati wa vita ziliruhusu, mikusanyiko mingine ilirudia programu hiyo kuzunguka ulimwengu. Wakati ule, wengi wa watu wa Yehova walitaraji kwamba vita hiyo ingeongezeka na kuwa vita ya Mungu ya Har–Magedoni; kwa sababu hiyo kile kichwa cha hotuba ya watu wote, “Amani—Je! Inaweza Kudumu?,” kiliamsha udadisi mwingi. N. H. Knorr, msimamizi mpya wa Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi angewezaje kuthubutu kuongea juu ya amani wakati kinyume kabisa ndilo jambo lililoelekea kuwa akibani kwa ajili ya mataifa?a Sababu ilikuwa kwamba jamii ya Yohana ilikuwa ikitoa “zaidi ya uangalifu wa kawaida” kwenye Neno la kiunabii la Mungu.—Waebrania 2:1; 2 Petro 1:19, NW.

      4 Hotuba “Amani—Je! Inaweza Kudumu?” ilitupa nuru gani juu ya unabii? Akitambulisha waziwazi hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu wa Ufunuo 17:3 kuwa Ushirika wa Mataifa, N. H. Knorr aliendelea kuzungumzia mwendo wao wenye msukosuko juu ya msingi wa maneno yafuatayo ya malaika kwa Yohana: “Hayawani-mwitu ambaye wewe uliona alikuwako, lakini hayuko, na bado yu karibu kupanda atoke ndani ya abiso, na yeye anapaswa kwenda zake ndani ya uharibifu.”—Ufunuo 17:8a, NW.

      5. (a) Ni jinsi gani kwamba “hayawani-mwitu . . . alikuwako” na kisha “hayuko”? (b) N. H. Knorr alijibuje swali “Je! Ushirika utabaki katika shimo?”

      5 “Hayawani-mwitu . . . alikuwako.” Ndiyo, alikuwa amekuwako akiwa Ushirika wa Mataifa kutoka Januari 10, 1920, na kuendelea, kukiwa na mataifa 63 yenye kushiriki kwa wakati mmoja au mwingine. Lakini, kwa zamu, Japani, Ujeremani, na Italia zilijiondoa, na nchi zilizokuwa Muungano wa Sovieti ziliondolewa kutoka Ushirika huo. Katika Septemba 1939 dikteta Mnazi wa Ujeremani alianzisha Vita ya Ulimwengu 2.b Ukiwa umeshindwa kuendeleza amani katika ulimwengu, Ushirika wa Mataifa ulitumbukia kabisa ndani ya abiso ya kutotenda. Kufikia 1942 ulikuwa haupo kabisa. Wala kabla ya hapo wala kwenye tarehe fulani ya baadaye Yehova hakufasiria watu wake kina kamili cha maana ya njozi hiyo, ila kwenye wakati huo hasa wenye hatari! Kwenye Ulimwengu Mpya wa Kitheokrasi Kusanyiko, N. H. Knorr angeweza kujulisha wazi, kupatana na unabii, kwamba “hayawani-mwitu . . . hayuko.” Kisha akauliza swali, “Je! Ushirika utabaki katika shimo?” Akinukuu Ufunuo 17:8, NW, yeye akajibu: “Ushirika wa mataifa ya kilimwengu utainuka tena.” Na ndivyo ikathibitika kuwa hasa—katika kutetea ukweli wa Neno la Yehova la kiunabii!

      Kupanda Kutoka Abiso

      6. (a) Ni lini hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu alipopanda kutoka abiso, na kwa jina gani jipya? (b) Ni kwa nini kwa kweli Umoja wa Mataifa ni uhuisho wa hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu?

      6 Hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu alipanda kweli kweli kutoka katika abiso. Katika Juni 26, 1945, kukiwa na kishindo cha sherehe ya vigelegele katika San Francisco, U.S.A., mataifa 50 yalipiga kura kukubali Katiba ya tengenezo la Umoja wa Mataifa. Baraza hili lilipaswa “kudumisha amani na usalama wa kimataifa.” Kulikuwako mifanano mingi kati ya Ushirika na UM. The World Book Encyclopedia hueleza: “Katika njia fulani, UM hushabihi Ushirika wa Mataifa, ambao ulipangwa kitengenezo baada ya Vita ya Ulimwengu 1 . . . Mengi ya mataifa yaliyoasisi UM yalikuwa pia yameasisi ule Ushirika. Kama Ushirika, UM ulisimamishwa kusaidia kutunza amani kati ya mataifa. Ala kuu za UM zafanana sana na zile za Ushirika.” Basi, UM kwa kweli ni uhuisho wa hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu. Uanachama wao wa mataifa yapatayo 190 unazidi kwa mbali sana ule wa Ushirika wenye mataifa 63; umechukua pia madaraka makubwa zaidi ya yale ya mtangulizi wao.

      7. (a) Ni katika njia gani wakaaji wa dunia wamestaajabu kwa kusifu mno huyo hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu aliyehuishwa? (b) Ni mradi gani ambao umetatiza UM, naye katibu mkuu wao alisema nini kwa habari hii?

      7 Mwanzoni, matumaini makubwa yalionyeshwa kwa ajili ya UM. Hiyo ilikuwa katika utimizo wa maneno haya ya malaika: “Na wakati wao waona jinsi hayawani-mwitu alikuwako, lakini hayuko, na bado atakuwapo, wale ambao hukaa juu ya dunia watastaajabu kwa kusifu mno, lakini majina yao hayajaandikwa juu ya hati-kunjo ya uhai tangu kuasisiwa kwa ulimwengu.” (Ufunuo 17:8b, NW) Wakaaji wa dunia wamesifu mno dude jipya hili, linalotenda kutoka makao makuu yalo yenye fahari kwenye East River wa New York. Lakini amani ya kweli na usalama vimetatiza UM. Katika sehemu kubwa ya karne ya 20, amani ya ulimwengu ilidumishwa tu kwa tisho la “angamizano hakika,” nayo mashindano ya kuunda silaha yameendelea kuongezeka kwa kadiri kubwa mno. Baada ya jitihada ya Umoja wa Mataifa ya miaka karibu 40, aliyekuwa katibu mkuu wao, Javier Pérez de Cuéllar, aliomboleza hivi katika 1985: “Sisi tunaishi katika enzi nyingine ya washupavu, na sisi hatujui la kufanya juu ya hilo.”

      8, 9. (a) Ni kwa nini UM hauna jawabu kwa matatizo ya ulimwengu, nao utapatwa na nini kulingana na amri ya Mungu? (b) Ni kwa nini waasisi na wasifaji wa UM hawakuandikisha majina yao katika “hati-kunjo ya uhai” ya Mungu? (c) Ufalme wa Yehova utatimiza jambo gani kwa kufaulu?

      8 UM hauna jawabu. Na kwa nini? Kwa sababu Mpaji uhai wa aina ya binadamu yote siye mpaji-uhai wa UM. Urefu wa maisha yao utakuwa mfupi, kwa kuwa kulingana na amri ya Mungu, ‘wapaswa kwenda zao ndani ya uharibifu.’ Waasisi na wasifaji mno wa UM hawakuandikisha majina yao katika hati-kunjo ya uhai ya Mungu. Watu wenye dhambi, wenye kufa, wengi wao wakiwa wadhihaki wa jina la Mungu, wangewezaje kufanikiwa kupata kupitia UM kitu ambacho Yehova Mungu amejulisha wazi kwamba yeye yu karibu kutimiza, si kwa njia za kibinadamu, bali kupitia Ufalme wa Kristo wake?—Danieli 7:27; Ufunuo 11:15.

      9 Kwa kweli UM ni kitu bandia chenye makufuru cha Ufalme wa Kimesiya wa Mungu kupitia Yesu Kristo, Mwana-Mfalme wa Amani wake—ambaye utawala wake wa kifalme hautakuwa na mwisho. (Isaya 9:6, 7, NW) Hata kama UM ungeweza kutiatia kama viraka amani fulani ya kitambo, vita vingefyatuka tena. Hiyo ni asili ya watu wenye dhambi. “Majina yao hayajaandikwa juu ya hati-kunjo ya uhai tangu kuasisiwa kwa ulimwengu.” Ufalme wa Yehova kupitia Kristo hautasimamisha tu amani ya milele duniani bali, juu ya msingi wa dhabihu ya ukombozi ya Yesu, utainua wafu, waadilifu na wasio waadilifu ambao wamo katika kumbukumbu la Mungu. (Yohana 5:28, 29; Matendo 24:15) Hii inatia ndani kila mmoja ambaye amebaki akiwa imara ijapokuwa mashambulizi ya Shetani na mbegu yake, na wengine ambao wangali watajionyesha wenyewe kuwa watiifu. Kwa wazi, hati-kunjo ya uhai ya Mungu haitakuwa kamwe na majina ya wafuasi washupavu wa Babuloni Mkubwa au ya wowote wanaoendelea kuabudu hayawani-mwitu.—Kutoka 32:33, NW; Zaburi 86:8-10; Yohana 17:3; Ufunuo 16:2; 17:5.

      Amani na Usalama —Tumaini la Bure

      10, 11. (a) UM ulipiga mbiu ya nini katika 1986, na itikio lilikuwa nini? (b) Ni “jamaa za kidini” ngapi zilizokusanyika katika Assisi, Italia, kusali kwa ajili ya amani, na je! Mungu anajibu sala kama hizo? Fafanua.

      10 Katika jitihada za kutegemeza matumaini ya aina ya binadamu, Umoja wa Mataifa ulipiga mbiu ya 1986 kuwa “Mwaka wa Amani ya Kimataifa,” ukiwa na kichwa “Kulinda Salama Amani na Wakati Ujao wa Binadamu.” Mataifa yenye kupiga vita yaliombwa yalaze silaha zayo, angalau kwa mwaka mmoja. Itikio layo lilikuwa nini? Kulingana na ripoti iliyotolewa na Taasisi ya Utafiti wa Amani ya Kimataifa, watu wapatao milioni tano walikufa kwa sababu ya vita wakati wa 1986 pekee! Ingawa sarafu kadhaa za pekee na stampu za mwadhimisho zilitolewa, mataifa yaliyo mengi yalifanya kidogo sana kwa habari ya kufuatia wazo bora la amani katika mwaka huo. Hata hivyo, dini za ulimwengu—zikitamani sikuzote kuafikiana na UM—zilianza kutangaza mwaka huo kwa njia mbalimbali. Katika Januari 1, 1986, Papa John Paul 2 alisifu kazi ya UM na akaweka wakfu mwaka mpya kwa ajili ya amani. Na katika Oktoba 27, akakusanya viongozi wa nyingi za dini za ulimwengu katika Assisi, Italia, ili kusali kwa ajili ya amani.

      11 Je! Mungu anajibu sala kama hizo kwa ajili ya amani? Basi, viongozi wa kidini hao walikuwa wakisali kwa Mungu yupi? Kama ungewauliza, kila kikundi kingekupa jibu tofauti. Je! kuna jamii ya mamilioni ya miungu inayoweza kusikia na kujibu maombi rasmi yaliyotolewa kwa njia nyingi mbalimbali? Wengi wa washiriki waliabudu Utatu wa Jumuiya ya Wakristo.c Wabuddha, Wahindu, na wengine walitoa sala zao kwa miungu isiyo na hesabu. Kwa ujumla, “jamaa za kidini” 12 zilikusanyika, zikiwa zinawakilishwa na watu mashuhuri kama Askofu Mkuu wa Kianglikana wa Kantabari, Dalai Lama wa Buddha, kasisi wa Orthodoksi la Urusi, Msimamizi wa Ushirika wa Patakatifu pa Shinto wa Tokyo, waabudu-mizimu wa Kiafrika, na Wahindi Waamerika wawili waliovalia vazi la kichwani la manyoya-manyoya. Kilikuwa kikundi chenye rangi za namna namna, bila kusema zaidi, kikifanyiza kipindi cha TV chenye kutazamisha. Kikundi kimoja kilisali bila kukoma kwa saa 12 katika wakati mmoja. (Linga Luka 20:45-47.) Lakini je! yoyote ya sala hizo ilipenya mawingu ya mvua yaliyoning’inia juu ya mkusanyiko huo? Kwa sababu zinazofuata, la:

      12. Ni kwa sababu zipi Mungu hakujibu sala za viongozi wa kidini wa ulimwengu kwa ajili ya amani?

      12 Tofauti na wale ambao “hutembea katika jina la Yehova,” hakuna mwanadini hata mmoja wa hao aliyekuwa akisali kwa Yehova, Mungu aliye hai, ambaye jina lake huonekana mara zapata 7,000 katika maandishi asilia ya Biblia. (Mika 4:5; Isaya 42:8, 12, NW)d Wakiwa kikundi wao hawakumwendea Mungu kwa jina la Yesu, walio wengi wao wakiwa hata hawaitikadi katika Yesu Kristo. (Yohana 14:13; 15:16) Hakuna baadhi yao wanaofanya mapenzi ya Mungu kwa ajili ya siku yetu, ambayo ni kupiga mbiu ulimwenguni pote ya Ufalme unaokuja wa Mungu—si UM—kuwa ndilo tumaini halisi kwa aina ya binadamu. (Mathayo 7:21-23; 24:14; Marko 13:10) Kwa sehemu iliyo kubwa zaidi matengenezo ya kidini yao yamejihusisha katika vita vyenye umwagaji-damu vya historia, kutia na vita viwili vya ulimwengu vya karne ya 20. Kwa hao, Mungu husema: “Hata ingawa nyinyi mnafanya sala nyingi, mimi sisikilizi; mikono yenu imejawa na umwagaji-damu.”—Isaya 1:15, NW; 59:1-3.

      13. (a) Ni kwa nini ni jambo la maana kwamba viongozi wa kidini wa ulimwengu wamepaswa kuungana mikono na UM katika kutoa mwito kwa ajili ya amani? (b) Vilio kwa ajili ya amani vitafikia upeo gani uliotabiriwa kimungu?

      13 Na zaidi, ni jambo la maana yenye kina kwamba viongozi wa kidini wamepaswa kuungana mikono na Umoja wa Mataifa katika kutoa mwito kwa ajili ya amani wakati huu. Wao wangependa kutumia uvutano juu ya UM kwa faida yao wenyewe, hasa katika enzi hii ya ki-siku-hizi wakati watu wao wanaacha dini. Kama viongozi wasio waaminifu katika Israeli wa kale, wao wanalia, “‘Kuna amani! Kuna amani!’ wakati hakuna amani.” (Yeremia 6:14, NW) Pasipo shaka vilio vyao kwa ajili ya amani vitaendelea, vikiwa vinainuka katika kuunga mkono upeo ambao kuhusu huo mtume Paulo alitolea unabii: “Siku ya Yehova inakuja sawasawa kama mwivi katika usiku. Wakati wowote wanaposema: ‘Amani na usalama!’ ndipo uharibifu wa ghafula utakuwa juu yao papo hapo kama maumivu makali ya ghafula ya taabu juu ya mwanamke mwenye mimba; na wao hawataponyoka kwa vyovyote.”—1 Wathesalonike 5:2, 3, NW.

      14. Huenda kilio cha “Amani na usalama!” kitakuwa cha namna gani, na mmoja anaweza kuepukaje kuongozwa vibaya?

      14 Katika miaka ya hivi karibuni, wanasiasa wametumia maneno “amani na usalama” kuelezea mipango mbalimbali ya wanadamu. Je! jitihada hizo za viongozi wa ulimwengu zinaonyesha mwanzo wa utimizo wa andiko la 1 Wathesalonike 5:3? Au je, Paulo alikuwa akizungumzia tukio hususa na lenye kutokeza sana hivi kwamba lingetambuliwa ulimwenguni? Kwa kuwa mara nyingi unabii wa Biblia hueleweka kikamili tu baada ya kutimia au wakati unapoendelea kutimia, itatubidi tungoje tuone itakuwaje. Kwa sasa, Wakristo wanajua kwamba hata ingawa huenda ikaonekana kana kwamba mataifa yamepata amani na usalama, hakuna kitu ambacho kwa kweli kitakuwa kimebadilika. Ubinafsi, chuki, uhalifu, mvunjiko wa jamaa, ukosefu wa adili, magonjwa, huzuni, na kifo bado vitakuwapo. Ndiyo sababu si lazima wewe uongozwe vibaya na kilio chochote cha “amani na usalama,” ikiwa umeamka kuona maana ya matukio ya ulimwengu na unatii maonyo ya kiunabii katika Neno la Mungu.—Marko 13:32-37; Luka 21:34-36.

      [Maelezo ya Chini]

      a J. F. Rutherford alikufa Januari 8, 1942, na N. H. Knorr alimfuata kuwa msimamizi wa Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi.

      b Katika Novemba 20, 1940, Ujeremani, Italia, Japani, na Hungary zilitia sahihi kwa ajili ya “Ushirika wa Mataifa mpya,” ikifuatwa siku nne baadaye na msambazo-redio wa Vatikani wa Misa na sala kwa ajili ya amani ya kidini na kwa ajili ya utaratibu mpya wa mambo. Huo ‘Ushirika mpya’ haukutokea.

      c Dhana ya Utatu ina shina kutoka Babuloni wa kale, ambako mungu-jua Shamashi, mungu-mwezi Sin, na mungu-nyota Ishta waliabudiwa wakiwa utatu. Misri ilifuata kigezo icho hicho, ikiabudu Osirisi, Isisi, na Horusi. Asshuri, mungu mkuu wa Ashuru, huonyeshwa taswira ya vichwa vitatu. Kwa kufuata kigezo hicho, mifano inapatikana katika makanisa ya Kikatoliki ikionyesha Mungu kuwa ana vichwa vitatu.

      d Webster’s Third New International Dictionary ya 1993 hufasili Yehova Mungu kuwa “mungu mkuu kupita wote anayetambuliwa na mungu pekee anayeabudiwa na Mashahidi wa Yehova.”

  • Kufisha Babuloni Mkubwa
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • Sura ya 35

      Kufisha Babuloni Mkubwa

      1. Malaika anaelezaje habari ya hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu, na ni hekima ya aina gani inayohitajiwa kuelewa mifananisho ya Ufunuo?

      KATIKA kueleza zaidi habari ya hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu wa Ufunuo 17:3, malaika anamwambia Yohana: “Hapa ndipo elimu iliyo na hekima inapofaa: Vichwa saba humaanisha milima saba, ambako mwanamke huketi juu ya kilele. Na wako wafalme saba: watano wameanguka, mmoja yupo, mwingine hajawasili bado, lakini yeye awasilipo lazima yeye abaki kitambo kifupi.” (Ufunuo 17:9, 10, NW) Malaika anawasilisha hekima kutoka juu, hekima pekee inayoweza kutoa uelewevu wa mifananisho katika Ufunuo. (Yakobo 3:17) Hekima hii inaipa jamii ya Yohana na waandamani wayo nuru juu ya hatari ya nyakati tunamoishi. Inajenga katika mioyo yenye kujitoa uthamini wa hukumu za Yehova, ambazo sasa karibu kutimizwa, na inakaza kikiki hofu yenye afya kuelekea Yehova. Kama Mithali 9:10, NW inavyotaarifu: “Hofu ya Yehova ndio mwanzo wa hekima, na maarifa ya kumjua Mmoja Aliye Mtakatifu Zaidi Sana ndio uelewevu.” Hekima ya kimungu inatufunulia nini juu ya hayawani-mwitu?

      2. Ni nini maana ya vichwa saba vya hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu, na inakuwaje kwamba “watano wameanguka, mmoja yupo”?

      2 Vichwa saba vya hayawani-mwitu mkali sana husimamia “milima” saba, au “wafalme” saba. Semi zote mbili hutumiwa Kimaandiko kurejezea mamlaka za kiserikali. (Yeremia 51:24, 25; Danieli 2:34, 35, 44, 45) Katika Biblia, serikali za ulimwengu sita hutajwa kuwa zikiathiri mambo ya watu wa Mungu: Misri, Ashuru, Babuloni, Umedi-Uajemi, Ugiriki, na Roma. Kati ya hizi, tano zilikuwa tayari zimekuja na zikaenda kufikia wakati Yohana alipopokea Ufunuo, lakini Roma ilikuwa ingali sana serikali ya ulimwengu. Hii inalingana vizuri na maneno haya, “watano wameanguka, mmoja yupo.” Lakini namna gani juu ya “mwingine” aliyekuwa akitazamiwa kuja?

      3. (a) Milki ya Roma ilikujaje kugawanywa? (b) Ni matukio gani yaliyotukia katika Magharibi? (c) Milki Takatifu ya Roma yapasa ionweje?

      3 Milki ya Roma ilidumu na hata ikapanuka kwa mamia ya miaka baada ya siku ya Yohana. Katika 330 W.K. Maliki Konstantino alihamisha jiji kuu lake kutoka Roma kwenda Bizanshamu, ambalo alilipa jina Konstantinopo. Katika 395 W.K., Milki ya Roma iligawanywa ikawa sehemu za Mashariki na Magharibi. Katika 410 W.K., Roma liliangushwa na Alariki, mfalme wa Wavisigothi (kabila la Kijeremani ambalo lilikuwa limeongolewa kuwa la “Ukristo” wa aina ya Aria). Makabila ya Kijeremani (ya “Kikristo” pia) yalishinda Hispania na eneo lililo kubwa zaidi la Roma katika Afrika Kaskazini. Zilikuwako karne za misukosuko, kutotulia, na kujirekebisha upya katika Ulaya. Wamaliki wenye sifa waliinuka katika Magharibi, kama vile Charlemagne, ambaye alifanya fungamano na Papa Leo 3 katika karne ya 9, na Frederick 2, ambaye alitawala katika karne ya 13. Lakini milki yao, ingawa iliitwa Milki Takatifu ya Roma ilikuwa ndogo zaidi ya ile Milki ya Roma ya mapema zaidi, wakati wa kilele cha usitawi wayo. Ilikuwa zaidi mrudisho au mwendelezo wa hiyo serikali ya kale kuliko kuwa milki mpya.

      4. Milki ya Mashariki ilikuwa na mafanikio gani, lakini kulitukia nini kwa sehemu kubwa ya lililokuwa eneo la Roma ya kale katika Afrika Kaskazini, Hispania, na Siria?

      4 Milki ya Mashariki ya Roma, yenye kitovu katika Konstantinopo, iliendelea ikiwa na uhusiano wenye wasiwasi na Milki ya Magharibi. Katika karne ya sita, maliki wa Mashariki Justiniani 1 aliweza kushinda sehemu kubwa ya Afrika ya Kaskazini, na pia akaingilia Hispania na Italia. Katika karne ya saba, Justiniani 2 alikombolea Milki hiyo maeneo ya Makedonia ambayo yalikuwa yameshindwa na wanamakabila wa Kislavi. Hata hivyo, Kufikia karne ya nane eneo kubwa la zamani la Roma ya kale katika Afrika Kaskazini, Hispania, na Siria lilikuwa limekuja chini ya milki mpya ya Islamu na hivyo likapita kutoka udhibiti wa Konstantinopo na Roma pia.

      5. Ingawa jiji la Roma lilianguka 410 W.K., ilikuwaje kwamba ilichukua karne nyingi zaidi kabla ya visehemu vyote vya Milki ya Roma ya kisiasa kutoweka katika mandhari ya ulimwengu?

      5 Jiji la Konstanipo lenyewe lilidumu kwa muda mrefu zaidi kidogo. Liliokoka mashambulizi ya mara nyingi kutoka kwa Waajemi, Waarabu, Wabulgari, na Warusi mpaka mwishowe katika 1203 likaangushwa—si na Waislamu bali na Wakrusedi kutoka Magharibi. Ingawa hivyo, katika 1453, lilikuja chini ya mamlaka ya mtawala Mwislamu wa Ottomani Mehmedi 2 na upesi likawa jiji kuu la Milki ya Ottomani, au ya Kituruki. Hivyo, ijapokuwa jiji la Roma lilianguka katika 410 W.K., ilichukua karne nyingi zaidi kabla ya visehemu vyote vya Milki ya Roma ya kisiasa kutoweka katika mandhari ya ulimwengu. Na hata hivyo, uvutano wayo bado ulitambulikana katika milki za kidini zenye msingi wa upapa wa Roma na makanisa ya Orthodoksi ya Mashariki.

      6. Ni milki zipi mpya kabisa zilizotokea, na ni ipi iliyopata kuwa yenye kufanikiwa zaidi sana?

      6 Hata hivyo, kufikia karne ya 15, nchi fulani zilikuwa zikijenga milki mpya kabisa. Ingawa baadhi ya serikali hizi mpya za kibepari zilipatikana katika maeneo ambayo hapo kwanza yalikuwa makoloni ya Roma, milki zazo hazikuwa mwendelezo vivi hivi wa Milki ya Roma. Ureno, Hispania, Ufaransa, na Uholanzi zote zikawa makao ya milki zilizotapakaa sana. Lakini iliyofanikiwa zaidi sana ilikuwa Uingereza, ambayo ikaja kusimamia milki kubwa mno ambayo juu yayo ‘jua halikutua kamwe.’ Milki hii ilienea katika nyakati mbalimbali juu ya sehemu kubwa ya Amerika Kaskazini, Afrika, India, na Esia Kusini-mashariki, pamoja na maeneo ya Pasifiki Kusini.

      7. Serikali ya ulimwengu ya uwili ilikujaje kuwako, na Yohana alisema ni kwa muda gani ‘kichwa’ au serikali ya ulimwengu ya saba ingeendelea?

      7 Kufikia karne ya 19, baadhi ya makoloni katika Amerika Kaskazini yalikuwa yamekwisha kujitenga na Uingereza yakaunda United States ya Amerika yenye kujitawala. Kisiasa, hitilafu fulani ziliendelea kati ya taifa jipya na iliyokuwa nchi-mama yao. Hata hivyo, vita ya ulimwengu ya kwanza ilizilazimisha hizo nchi zote mbili kutambua masilahi yazo ya pamoja na zikatia nguvu uhusiano maalumu kati yazo. Hivyo, namna ya serikali ya ulimwengu ya uwili ikatokea, ikiwa inafanyizwa na United States ya Amerika, sasa ikiwa ndilo taifa la ulimwengu lenye ukwasi zaidi sana, na Uingereza, kao la milki ya ulimwengu iliyo kubwa zaidi sana. Basi, hiki, ndicho ‘kichwa’ cha saba, au serikali kubwa ya ulimwengu, ambayo inaendelea mpaka ndani ya wakati wa mwisho na katika maeneo ambamo Mashahidi wa ki-siku-hizi wa Yehova walijiimarisha kwanza. Kikilinganishwa na utawala mrefu wa kichwa cha sita, hiki cha saba ‘chabaki kitambo kifupi’ mpaka Ufalme wa Mungu uangamizapo mataifa yote.

      Kwa Nini Huitwa Mfalme wa Nane?

      8, 9. Malaika anamwitaje hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu na ni katika njia gani huchipuka kutoka kwa wafalme saba?

      8 Malaika anamweleza Yohana zaidi hivi: “Na hayawani-mwitu ambaye alikuwako lakini hayuko, yeye pia mwenyewe ni mfalme wa nane, lakini huchipuka kutoka kwa wale saba, na yeye huenda zake ndani ya uharibifu.” (Ufunuo 17:11, NW) Hayawani-mwitu wa ufananisho rangi-nyekundu-nyangavu “huchipuka kutoka” kwa vichwa saba; yaani, yeye anazaliwa na, au yuko kwa sababu ya vichwa hivyo vya ‘hayawani-mwitu kutoka bahari,’ ambaye hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu ni mfano wake. Kwa njia gani? Basi, katika 1919 serikali ya Uingereza-Amerika ilikuwa ndiyo kichwa chenye kutawala. Vile vichwa sita vilivyotangulia vilikuwa vimeanguka, nacho cheo cha serikali kubwa ya ulimwengu yenye kutawala kilikuwa kimepitishwa kwenye kichwa hiki cha uwili na sasa kikawa katika kitovu chacho. Hiki kichwa cha saba, kikiwa ndicho mwakilishi wa sasa wa mstari wa serikali za ulimwengu, kilikuwa ndicho kani yenye kutenda katika kusimamisha Ushirika wa Mataifa na kingali ndicho mwendelezaji na mtegemezaji kifedha mkuu wa Umoja wa Mataifa. Hivyo, kwa njia ya ufananisho hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu—mfalme wa nane—“huchipuka kutoka” kwa vile vichwa saba vya kwanza. Ikionwa katika njia hii, taarifa ya kwamba yeye alichipuka kutoka kwa vichwa saba inapatana vizuri na ufunuo wa mapema zaidi kwamba hayawani-mwitu mwenye pembe mbili mithili ya mwana-kondoo (Serikali ya Ulimwengu Uingereza-Amerika, kichwa cha saba cha hayawani-mwitu wa kwanza) alihimiza kufanyizwa kwa huo mfano na akaupa uhai.—Ufunuo 13:1, 11, 14, 15.

      9 Kwa kuongezea, washiriki wa kwanza kabisa wa Ushirika wa Mataifa walikuwamo, pamoja na Uingereza, serikali ambazo zilitawala katika makao ya baadhi ya vichwa vilivyotangulia, yaani, Ugiriki, Irani (Uajemi), na Italia (Roma). Hatimaye, serikali zenye kutawala maeneo yaliyodhibitiwa na serikali za ulimwengu sita zilizotangulia zikaja kuwa washiriki waungaji mkono wa mfano wa hayawani-mwitu. Katika maana hii, vilevile, ingeweza kusemwa kwamba huyu hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu alichipuka kutoka kwa serikali za ulimwengu saba.

      10. (a) Inaweza kusemwaje kwamba hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu “yeye pia mwenyewe ni mfalme wa nane”? (b) Kiongozi mmoja wa nchi zilizokuwa Muungano wa Sovieti alionyeshaje uungaji-mkono wake wa Umoja wa Mataifa?

      10 Angalia kwamba hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu “yeye pia mwenyewe ni mfalme wa nane.” Hivyo, Umoja wa Mataifa leo unakusudiwa uonekane kuwa serikali ya ulimwengu. Nyakati fulani hata umetenda hivyo, ukituma majeshi uwanjani kusuluhisha magomvi ya kimataifa, kama vile katika Korea, Peninsula ya Sinai, nchi fulani za Kiafrika, na Lebanoni. Lakini huo ni mfano tu wa mfalme. Kama vile mfano wa kidini, huo hauna uvutano au uwezo halisi isipokuwa ule ambao unapewa na wale ambao waliutokeza na wanaouabudu. Katika pindi fulani, hayawani-mwitu huyu wa ufananisho huonekana dhaifu; lakini hajapatwa kamwe na aina ya kuachwa kwa wingi na washiriki wenye maelekeo ya udikteta ambao walifanya Ushirika wa Mataifa utetereke na kutumbukia ndani ya abiso. (Ufunuo 17:8) Ingawa anashikilia maoni yanayotofautiana sana katika maeneo mengine, kiongozi mmoja mashuhuri wa nchi zilizokuwa Muungano wa Sovieti katika 1987 alijiunga na mapapa wa Roma katika kuonyesha uungaji-mkono wa UM. Yeye hata alitaka kuwe na “mfumo mpana wa usalama wa kimataifa” wenye kutegemea UM. Kama Yohana ajifunzavyo upesi, wakati utakuja ambapo UM utatenda kwa mamlaka kubwa. Kisha huo, katika zamu yao, “huenda zake ndani ya uharibifu.”

      Wafalme Kumi kwa Saa Moja

      11. Malaika wa Yehova anasema nini juu ya pembe kumi zilizo juu ya hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu wa ufananisho?

      11 Katika sura ya Ufunuo iliyotangulia, malaika, wa sita na wa saba walimimina mabakuli ya kasirani ya Mungu. Hivyo sisi tuliarifiwa kwamba wafalme wa dunia wanakusanywa kwenye vita ya Mungu kwenye Har–Magedoni na kwamba ‘Babuloni Mkubwa apaswa kukumbukwa katika mwono wa Mungu.’ (Ufunuo 16:1, 14, 19, NW) Sasa tutajifunza kirefu zaidi jinsi hukumu za Mungu juu ya hawa zitatekelezwa. Sikiliza tena malaika wa Yehova anaponena kwa Yohana. “Na pembe kumi ambazo wewe uliona humaanisha wafalme kumi, ambao bado kupokea ufalme, lakini wao hupokea mamlaka wakiwa wafalme saa moja pamoja na hayawani-mwitu. Hawa wana fikira moja, na hivyo wao humpa hayawani-mwitu nguvu na mamlaka yao. Hawa watapigana na Mwana-Kondoo, lakini, kwa sababu yeye ni Bwana wa mabwana na Mfalme wa wafalme, Mwana-Kondoo atashinda wao. Pia, wale wenye kuitwa na wachaguliwa na waaminifu pamoja na yeye watafanya hivyo.”—Ufunuo 17:12-14, NW.

      12. (a) Pembe kumi ni picha ya nini? (b) Ni jinsi gani pembe kumi za ufananisho ‘hazikuwa zimepokea ufalme’? (c) Pembe kumi za ufananisho zinakuwaje na “ufalme” sasa, na ni kwa muda gani?

      12 Pembe kumi ni picha ya serikali zote za kisiasa ambazo zinatawala sasa katika mandhari ya ulimwengu na ambazo huunga mkono hayawani-mwitu. Ni nchi chache sana zilizoko sasa ambazo zilijulikana katika siku ya Yohana. Na zile zilizojulikana, kama Misri na Uajemi (Irani), leo zina muundo wa kisiasa ulio tofauti kabisa. Kwa sababu hiyo, katika karne ya kwanza, ‘pembe kumi hazikuwa zimepokea ufalme.’ Lakini sasa katika siku ya Bwana, zina “ufalme,” au mamlaka ya kisiasa. Milki kubwa-kubwa za kikoloni zilipoanguka, hasa tangu vita ya ulimwengu ya pili, mataifa mengi mapya yamezaliwa. Hizi, pamoja na serikali ambazo zimeimarika muda mrefu, lazima zitawale pamoja na hayawani-mwitu kwa kipindi kifupi—“saa moja” tu—kabla Yehova hajakomesha mamlaka zote za kisiasa za ulimwengu kwenye Har–Magedoni.

      13. Ni katika njia gani pembe kumi zina “fikira moja,” na hiyo huhakikisha mwelekeo gani kwa Mwana-Kondoo?

      13 Leo, utukuzo wa taifa ndio mojapo kani zenye nguvu zaidi sana zinazosukuma pembe kumi hizi. Zina “fikira moja” kwa kuwa hizo zinataka kuhifadhi enzi zao za kitaifa badala ya kukubali Ufalme wa Mungu. Hilo ndilo lilikuwa kusudi lao katika kuchangia Ushirika wa Mataifa na tengenezo la Umoja wa Mataifa katika ile mara ya kwanza—kuhifadhi amani ya ulimwengu na hivyo kulinda salama kuwako kwazo. Mwelekeo kama huo unahakikisha kwamba pembe kumi zitapinga Mwana-Kondoo, “Bwana wa mabwana na Mfalme wa wafalme,” kwa sababu Yehova amekusudia kwamba Ufalme wake chini ya Yesu Kristo hivi karibuni utachukua mahali pa falme hizi.—Danieli 7:13, 14; Mathayo 24:30; 25:31-33, 46.

      14. Inawezekanaje kwa watawala wa ulimwengu kupigana na Mwana-Kondoo, na tokeo litakuwa nini?

      14 Bila shaka, watawala wa ulimwengu huu hawawezi kufanya kitu chochote dhidi ya Yesu mwenyewe. Yeye yumo mbinguni, mbali sana wasimoweza kumfikia. Lakini ndugu za Yesu, wabakio wa mbegu ya mwanamke, wangali duniani na inaonekana wazi wanaumizika. (Ufunuo 12:17) Nyingi za pembe zimekwisha onyesha uhasama mkali kuwaelekea, na katika njia hii zimepigana na Mwana-Kondoo. (Mathayo 25:40, 45) Ingawa hivyo, karibuni, wakati utakuja wa Ufalme wa Mungu ‘kuponda-ponda na kuweka mwisho kwenye falme hizi zote.’ (Danieli 2:44, NW) Ndipo, wafalme wa dunia watakuwa katika pigano hadi tamati pamoja na Mwana-Kondoo, kama tutakavyoona karibuni. (Ufunuo 19:11-21) Lakini hapa tunajifunza mambo ya kutosha kung’amua kwamba mataifa hayatafanikiwa. Ingawa hayo pamoja na hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu wa UM wana “fikira moja” yao, wao hawawezi kumshinda “Bwana wa mabwana na Mfalme wa wafalme” aliye mkubwa, wala hawawezi kushinda “wale wenye kuitwa na wachaguliwa na waaminifu pamoja na yeye,” kutia ndani wafuasi wapakwa-mafuta wake ambao wangali duniani. Hawa pia watakuwa wamekwisha shinda kwa kushika ukamilifu katika kujibu mashtaka maovu ya Shetani.—Warumi 8:37-39; Ufunuo 12:10, 11.

      Kuteketeza Kahaba

      15. Malaika anasema nini juu ya kahaba na mwelekeo na tendo la pembe kumi na hayawani-mwitu kuelekea yeye?

      15 Watu wa Mungu sio peke yao wanaochukiwa na pembe kumi. Malaika sasa anavuta uangalifu wa Yohana kwenye kahaba: “Na yeye anasema kwangu mimi: ‘Maji ambayo wewe uliona, ambapo kahaba anaketi, humaanisha vikundi vya watu na umati wa watu na mataifa na ndimi. Na pembe kumi ambazo wewe uliona, na hayawani-mwitu, hizi zitachukia kahaba na zitafanya yeye kuwa mwenye kuteketezwa na mwenye uchi, na zitakula kabisa sehemu zake zenye mnofu na zitachoma yeye kabisa kabisa kwa moto.’”—Ufunuo 17:15, 16, NW.

      16. Ni kwa nini Babuloni Mkubwa hataweza kutegemea maji yake yamuunge mkono wa himaya wakati serikali za kisiasa zinapomgeukia?

      16 Kama vile Babuloni wa kale alivyotegemea ulinzi wa maji yake, Babuloni Mkubwa leo anategemea washiriki wake wengi mno “vikundi vya watu na umati wa watu na mataifa na ndimi.” Kwa kufaa malaika huelekeza uangalifu wetu kwenye hao kabla ya kusimulia tukio lenye kugutusha: Serikali za kisiasa za dunia hii zitamgeukia kijeuri Babuloni Mkubwa. “Vikundi vya watu na umati wa watu na mataifa na ndimi” wote hao watafanya nini wakati huo? Tayari watu wa Mungu wanaonya Babuloni Mkubwa kwamba maji ya mto Eufrati yatakauka. (Ufunuo 16:12) Mwishowe maji hayo yatakauka kabisa. Hayo hayataweza kumpa kahaba kizee mwenye kunyarafisha tegemezo lolote lenye kufaa katika saa yake ya uhitaji ulio mkubwa zaidi sana.—Isaya 44:27; Yeremia 50:38; 51:36, 37.

      17. (a) Ni kwa sababu gani ukwasi wa Babuloni Mkubwa hautamwokoa? (b) Mwisho wa Babuloni Mkubwa utakuwaje wenye aibu kabisa? (c) Mbali na pembe kumi, au mataifa moja moja, ni nini kingine kinachojiunga katika jeuri dhidi ya Babuloni Mkubwa?

      17 Kwa hakika, ukwasi mkubwa mno wa vitu vya kimwili hautaweza kumwokoa Babuloni Mkubwa. Huenda hata ukaharakisha kuharibiwa kwake, kwa kuwa njozi huonyesha kwamba wakati hayawani-mwitu na pembe kumi wanapomwonyesha chuki yao watamvua majoho yake ya kifalme na vito vyake vyote vya thamani. Wao watapora ukwasi wake. ‘Wanamfanya kuwa uchi,’ wakifichua kiaibu tabia yake halisi. Mteketezo wee! Pia mwisho wake ni wenye aibu kabisa. Wanamharibu, na ‘kula sehemu zake zenye mnofu,’ wakimwacha mifupa mitupu isiyo na uhai. Mwishowe, wao ‘humchoma kabisa kabisa kwa moto.’ Yeye huchomwa kabisa kama mwenye ugonjwa wa tauni, bila hata maziko ya heshima! Si mataifa yale tu, kama yanavyowakilishwa na pembe kumi, yanayomharibu kahaba mkubwa, bali pia “hayawani-mwitu,” kumaanisha UM wenyewe, hujiunga nayo katika kuonyesha jeuri hii. Utatoa idhini yao ili dini bandia iharibiwe. Yaliyo mengi ya yale mataifa 190 na zaidi yaliyo ndani ya UM yameonyesha tayari, kwa kiolezo chayo cha kupiga kura, uhasama wayo kuelekea dini, hasa ile ya Jumuiya ya Wakristo.

      18. (a) Ni uwezekano gani wa mataifa kugeukia dini za Kibabuloni ambao tayari umeonekana? (b) Ni nini itakayokuwa sababu ya msingi ya shambulio la ujumla juu ya kahaba mkubwa?

      18 Ni kwa nini hayo yangemtenda kijeuri hivyo hawara wao wa zamani? Sisi tumeona katika historia ya hivi majuzi uwezekano kama huo wa kugeukia dini ya Kibabuloni. Upinzani rasmi wa kiserikali umepunguza sana uvutano wa dini katika nchi kama vile China na nchi zilizokuwa Muungano wa Sovieti. Katika maeneo ya Kiprotestanti ya Ulaya, ubaridi wenye kuenea pote na mashaka vimeyaacha makanisa yakiwa tupu, hivi kwamba karibu dini imekufa. Milki kubwa mno ya Kikatoliki imegawanywa na uasi na kutoafikiana ambavyo viongozi wake wameshindwa kutuliza. Ingawa hivyo, haitupasi kupoteza mwono wa uhakika wa kwamba hili shambulio la mwisho kabisa, la ujumla juu ya Babuloni Mkubwa linakuja likiwa wonyesho wa hukumu ya Mungu isiyobadilika juu ya kahaba mkubwa.

      Kufikiliza Fikira ya Mungu

      19. (a) Utekelezo wa hukumu ya Yehova dhidi ya kahaba mkubwa unaweza kutolewaje kielezi na hukumu yake dhidi ya Yerusalemu asi-imani katika 607 K.W.K.? (b) Hali ya ukiwa, ya kutokaliwa ya Yerusalemu baada ya 607 K.W.K. ilitangulia kutoa tamathali ya nini kwa siku yetu?

      19 Yehova anatekelezaje hukumu hii? Hii inaweza kutolewa kielezi na tendo la Yehova dhidi ya watu wake waasi-imani katika nyakati za kale, ambao kuwahusu yeye alisema: “Katika manabii wa Yerusalemu mimi nimeona vitu vibaya sana, kufanya uzinzi na kutembea katika ubandia; na wao wameimarisha mikono ya watenda maovu ili kwamba isiwapase kurudi, kila mmoja kutoka ubaya wake mwenyewe. Kwangu mimi wao wote wamekuwa kama Sodoma, na wakaaji wake ni kama Gomora.” (Yeremia 23:14, NW) Katika 607 K.W.K., Yehova alitumia Nebukadneza ‘avue mavazi, atwae vitu vizuri, na aache uchi na bila nguo’ jiji hilo lenye uzinzi wa kiroho. (Ezekieli 23:4, 26, 29, NW) Yerusalemu la wakati huo lilikuwa kigezo cha Jumuiya ya Wakristo ya leo, na kama alivyoona Yohana katika njozi ya mapema zaidi, Yehova ataipa Jumuiya ya Wakristo na dini nyingine yote bandia adhabu inayofanana na hiyo. Ukiwa, hali ya kutokaliwa ya Yerusalemu baada ya 607 K.W.K. huonyesha vile Jumuiya ya Wakristo ya kidini itakavyoonekana baada ya kuvuliwa ukwasi wayo na kufichuliwa kiaibu. Na sehemu inayobaki ya Babuloni Mkubwa haitakuwa afadhali.

      20. (a) Yohana anaonyeshaje kwamba kwa mara nyingine tena Yehova atatumia watawala wa kibinadamu kutekeleza hukumu? (b) “Fikira” ya Mungu ni nini? (c) Ni katika njia gani mataifa yatafikiliza “fikira moja,” yayo lakini kwa kweli ni fikira ya nani itatimizwa?

      20 Kwa mara nyingine tena Yehova anatumia watawala wa kibinadamu kutekeleza hukumu. “Kwa maana Mungu alitia hilo ndani ya mioyo yao kufikiliza fikira yake, hata kufikiliza fikira yao moja kwa kumpa ufalme wao hayawani-mwitu, mpaka hapo maneno ya Mungu yatakuwa yametimilizwa.” (Ufunuo 17:17, NW) “Fikira” ya Mungu ni nini? Kupangia wafishaji wa Babuloni Mkubwa waungane pamoja, ili kumharibu kabisa. Bila shaka, matilaba ya watawala katika kumshambulia yatakuwa kufikiliza “fikira moja” yao wenyewe. Wao watahisi kwamba ni kwa masilahi yao ya utukuzaji wa taifa kumgeukia huyo kahaba mkubwa. Huenda wakaja kuona kule kuendelea kwa dini iliyopangwa kitengenezo ndani ya mipaka yao kuwa tisho kwa enzi zao. Lakini Yehova atakuwa kwa kweli akiongoza mambo kwa werevu; wao watafikiliza fikira yake kwa kuharibu kwa dharuba moja adui yake mzinzi wa muda mrefu!—Linga Yeremia 7:8-11, 34.

      21. Kwa kuwa hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu atatumiwa katika kuharibu Babuloni Mkubwa, kwa wazi mataifa yatafanya nini kwa habari ya Umoja wa Mataifa?

      21 Ndiyo, mataifa yatatumia hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu, Umoja wa Mataifa, katika kuharibu Babuloni Mkubwa. Wao hawatendi kwa utangulizi wao wenyewe, kwa maana Yehova hutia ndani ya mioyo yao “hata kufikiliza fikira moja yao kwa kumpa ufalme wao hayawani-mwitu.” Wakati ujapo, kwa wazi mataifa yataona uhitaji wa kuimarisha Umoja wa Mataifa. Itakuwa kana kwamba, wanaupa meno, wakiupa mamlaka yoyote na nguvu waliyo nayo ili kwamba uweze kugeukia dini bandia na kupiga vita kwa kufaulu dhidi yayo “mpaka hapo maneno ya Mungu yatakuwa yametimilizwa.” Hivyo, kahaba wa kale atakuja kwenye mwisho wake kabisa. Na apotelee mbali!

      22. (a) Kwenye Ufunuo 17:18, ni nini kinachoashiriwa kwa njia ambayo malaika humalizia ushahidi wake? (b) Mashahidi wa Yehova wanaitikiaje kufumbuliwa kwa fumbo hilo?

      22 Kana kwamba anakazia uhakika wa kutekelezwa kwa hukumu ya Yehova juu ya milki ya ulimwengu ya dini bandia, malaika anamalizia ushahidi wake kwa kusema: “Na mwanamke ambaye wewe uliona anamaanisha jiji kubwa ambalo lina ufalme juu ya wafalme wa dunia.” (Ufunuo 17:18, NW) Kama Babuloni wa wakati wa Belshaza, Babuloni Mkubwa “amepimwa uzani katika mizani na akapatikana anapungukiwa.” (Danieli 5:27, The New English Bible) Kufishwa kwake kutakuwa kwepesi na kwa kukata maneno. Nao Mashahidi wa Yehova wanaitikiaje kufumbuliwa kwa fumbo la kahaba mkubwa na la hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu? Wao huonyesha bidii katika kupiga mbiu ya siku ya hukumu ya Yehova, huku wakijibu “kwa upendezi” watafutaji wa ukweli wenye mioyo myeupe. (Wakolosai 4:5, 6; Ufunuo 17:3, 7, NW) Kama vile sura yetu ifuatayo itakavyoonyesha, wote wenye kutamania kuokoka wakati kahaba mkubwa anapofishwa lazima watende, na kutenda chakachaka!

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki