-
Kupiga Mbiu ya Kurudi kwa BwanaMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Unabii Mbalimbali Unaohusu Wakati na Kuwapo kwa Bwana
Asubuhi moja katika Januari 1876, Russell mwenye umri wa miaka 23 alipokea nakala ya jarida la kidini linaloitwa Herald of the Morning. Kutokana na picha katika jalada, yeye angeweza kuona kwamba lilihusiana na Uadventisti. Mhariri, Nelson H. Barbour, wa Rochester, New York, aliamini kwamba lengo la kurudi kwa Kristo si kuharibu familia za dunia bali kuzibariki na kwamba kuja kwake kungekuwa si katika mwili bali akiwa roho. Aa! hilo lilipatana na yale ambayo Russell na washirika wake katika Allegheny walikuwa wameamini kwa muda fulani!b Ingawa hivyo, ajabu ni kwamba Barbour aliamini kutokana na unabii mbalimbali unaohusu wakati wa Kibiblia kwamba Kristo alikuwa tayari yupo (bila kuonekana) na kwamba wakati ulikuwa umefika wa kufanya kazi ya mavuno ya kukusanya “ngano” (Wakristo wa kweli waliojumuika kuwa jamii ya Ufalme).—Mt., sura 13.
-
-
Kupiga Mbiu ya Kurudi kwa BwanaMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Russell alipokuwa akisafiri na kuhubiri, ikawa wazi kwake kwamba kitu fulani zaidi kilihitajiwa ili kuendeleza mbegu za kweli alizokuwa akipanda zikiwa hai na zimetiliwa maji. Jawabu lilikuwa nini? “Jarida la kila mwezi,” akasema Russell. Hivyo yeye na Barbour waliamua kufufua utangazaji wa jarida Herald, lililokuwa limeacha kuchapwa kwa sababu ya maandikisho kufutwa na fedha kumalizika. Russell alichanga fedha zake mwenyewe ili kulifufua hilo jarida, akiwa mmoja wa wahariri washirika walo.
Yote yalienda sawasawa kwa kitambo—yaani, mpaka 1878.
Russell Aachana na Barbour
Katika toleo la Agosti 1878 la Herald of the Morning, mlitokea makala iliyoandikwa na Barbour ambayo ilikana thamani yenye kubadilishana na kifo cha Kristo. Russell, ambaye alikuwa mchanga kuliko Barbour kwa miaka karibu 30, angeweza kuona kwamba kwa kweli, huko kulikuwa ni kukana sehemu yenye maana ya fundisho la fidia. Hivyo katika toleo lililofuata (Septemba 1878), Russell, katika makala moja yenye kichwa “Kule Kulipia,” alitetea fidia na kupinga taarifa za Barbour. Ubishi huo uliendelea katika kurasa za jarida hilo kwa miezi michache iliyofuata. Hatimaye, Russell aliamua kujiondoa katika ushirika na Bw. Barbour akaacha kuendelea kulitegemeza Herald kifedha.
-
-
Kupiga Mbiu ya Kurudi kwa BwanaMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
[Sanduku/Picha katika ukurasa wa 48]
“Nakuachia ‘Herald’”
Katika masika ya 1879, C. T. Russell aliacha kabisa kutegemeza gazeti “Herald of the Morning,” ambalo alikuwa ameshiriki kulitangaza pamoja na N. H. Barbour. Katika barua aliyomwandikia Barbour yenye tarehe ya Mei 3, 1879, Russell alifafanua sababu yake: “Kumezuka tofauti ya maoni kati yetu kwa habari ya fundisho la neno la Baba yetu [kuhusu thamani yenye kubadilisha ya fidia] na ingawa nakupa sifa kwa weupe wote wa moyo na unyoofu katika maoni yako, ambayo nadai mwenyewe maoni yaliyo kinyume, hata hivyo lazima niongozwe na uelewevu wangu mwenyewe wa neno la Baba yetu, na kwa sababu hiyo nakufikiria wewe kuwa unakosea. . . . Mambo yenye kuleta tofauti yaonekana kwangu kuwa ya msingi sana na ya maana sana hivi kwamba ushirika kamili na sikitiko kama lile lipaswalo kuwamo miongoni mwa watangazaji na wahariri wa jarida au gazeti, haupo tena kati yangu nawe, na kwa sababu ndivyo ilivyo, mimi nahisi kwamba uhusiano wetu wapaswa kukoma.”
Katika barua ya kufuatia ya tarehe ya Mei 22, 1879, Russell aliandika hivi: “Sasa nakuachia ‘Herald.’ Najiondoa nisihusiane nalo kabisa, nisiulize chochote kutoka kwako . . . Tafadhali toa tangazo katika nambari ifuatayo ya ‘Herald’ juu ya kujiondoa huko na uondoe jina langu.” Kuanzia toleo la Juni 1879, jina la Russell halikutokea tena akiwa mhariri-msaidizi wa “Herald.”
Barbour aliendelea kutangaza “Herald” mpaka 1903, wakati, kulingana na maandishi yapatikanayo ya maktaba, lilipokoma kuchapishwa. Barbour alikufa miaka michache baadaye, katika 1906.
-