-
Kuishi kwa Mafanikio na Ugonjwa Wako—Jinsi Gani?Amkeni!—2001 | Januari 22
-
-
Hali kadhalika, kukubali kwamba wewe ni mgonjwa hakumaanishi umeshindwa, lakini humaanisha “kupiga hatua kuelekea upande mwingine,” ndivyo alivyosema mwanamke mmoja mwenye ugonjwa wa kudumu.
-
-
Kuishi kwa Mafanikio na Ugonjwa Wako—Jinsi Gani?Amkeni!—2001 | Januari 22
-
-
Helen, mwanamke mwenye umri wa miaka 70 aliyedhoofishwa sana na ugonjwa wa kukakamaa kwa tishu, athibitisha hilo: “Kuwa tena na usawaziko wa kiakili na kihisia-moyo hakutegemei ugonjwa wako bali jinsi unavyoitikia ugonjwa huo.” Mtu mmoja ambaye amekabiliana na ulemavu kwa miaka kadhaa asema hivi: “Mtazamo chanya ni kama mkuku unaosawazisha merikebu.”
-
-
Kuishi kwa Mafanikio na Ugonjwa Wako—Jinsi Gani?Amkeni!—2001 | Januari 22
-
-
Kwa mfano, mfikirie Helen, aliyetajwa awali.
Kwa miaka 25 iliyopita, ugonjwa wa kukakamaa kwa tishu umedhoofisha misuli yake. Mwanzoni, alikuwa akitembea kwa msaada wa kifaa cha matembezi. Baadaye, aliposhindwa kutumia mkono wake wa kulia, alianza kutumia wa kushoto. Halafu, mkono wake wa kushoto ukadhoofika kabisa. Hatimaye, miaka minane iliyopita, alishindwa kabisa kutembea. Sasa anahitaji kuoshwa, kulishwa, na kuvishwa mavazi na wengine. Hilo humhuzunisha sana, hata hivyo, yeye asema: “Mwito wangu ungali, ‘Fikiria mambo unayoweza kufanya wala si yale uliyokuwa ukifanya.’” Na kwa msaada wa mumewe na wauguzi wanaomtembelea vilevile ubunifu wake mwenyewe, yeye huweza kufanya kazi fulani ambazo amekuwa akifurahia. Kwa mfano, kuwaeleza wengine ahadi ya Biblia ya ulimwengu wenye amani unaokuja kumekuwa sehemu muhimu sana ya maisha yake tangu alipokuwa na umri wa miaka 11, na leo bado anafanya hivyo kila juma. (Mathayo 28:19, 20) Helen aeleza anavyofanya:
“Mimi humwomba muuguzi anayenitembelea anishikie gazeti. Tunasoma pamoja matangazo ya vifo na kuteua kadhaa. Kisha mimi humwambia muuguzi huyo mambo ninayotaka yaandikwe kwenye barua nitakayowatumia watu wa ukoo wa yule aliyekufa, halafu muuguzi huyo hupiga chapa barua hiyo. Mimi huambatanisha barua hiyo na broshua Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa,a ambayo inaeleza tumaini la Biblia la ufufuo lenye kufariji. Mimi hufanya hivyo kila Jumapili alasiri. Mimi hufurahi kwa sababu bado naweza kujulisha wengine habari njema za Ufalme wa Mungu.”
Weka miradi inayofaa na unayoweza kutimiza. Sababu moja inayomfanya Helen ajaribu kubadili mambo yanayoweza kubadilishwa ni kwamba kufanya hivyo humwezesha kuweka na kutimiza miradi.
-
-
Kuishi kwa Mafanikio na Ugonjwa Wako—Jinsi Gani?Amkeni!—2001 | Januari 22
-
-
“Haidhuru mradi waonekana mdogo kadiri gani, kuutimiza hukuchochea kufanya zaidi,” asema Lex, mkazi wa Uholanzi. Zaidi ya miaka 20 iliyopita, alipokuwa na umri wa miaka 23, alihusika katika aksidenti iliyomfanya apooze. Wakati wa vipindi vingi vya matibabu ya maungo vilivyofuata, alitiwa moyo ajiwekee miradi, kama vile kunawa uso kwa kitambaa. Ilikuwa kazi ya kuchosha sana, lakini alifaulu. Alipoona kwamba alikuwa amefaulu kutimiza mradi huo, aliweka mradi mwingine—kufunua na kufunika tyubu ya dawa ya meno bila msaada. Alifaulu tena. “Ijapokuwa haikuwa rahisi,” asema Lex, “niligundua kwamba ningeweza kufanya mengi zaidi ya vile nilivyofikiri.”
Kwa kweli, Lex alitimiza miradi mikubwa zaidi kwa msaada wa mke wake. Kwa mfano, sasa yeye huandamana na Tineke, kwenda nyumba kwa nyumba kwa kiti cha magurudumu ili kushiriki na wengine ujuzi wa Biblia. Kila juma yeye pia humtembelea na kumtia moyo mtu mmoja aliyelemaa kabisa ambaye anajifunza naye Biblia. “Kuwasaidia wengine,” asema Lex, “hunipa uradhi mkubwa.”
-
-
Kuishi kwa Mafanikio na Ugonjwa Wako—Jinsi Gani?Amkeni!—2001 | Januari 22
-
-
Mwanamke mmoja mwenye ugonjwa wa kudumu alisuluhisha tatizo hilo kwa kuweka mipaka ya wakati aliotumia akizungumza na mumewe kuhusu ugonjwa wake. “Hatukuwa na budi kuweka mipaka ya mazungumzo hayo,” yeye asema. Kwa kweli, ugonjwa wako hauhitaji kuzuia mambo mengineyo unayoweza kushiriki. Mgeni mmoja, baada ya kuongea na rafikiye aliye kitandani kuhusu sanaa, historia, na sababu zinazomfanya awe na imani katika Yehova Mungu, alisema: “Yeye hajaruhusu ugonjwa wake uathiri utu wake. Nilifurahi mno kuongea naye.”
Kuwa mcheshi daima kutawafanya marafiki wako wafurahie kukutembelea. Mbali na hayo, kicheko hukunufaisha wewe binafsi. “Ucheshi hukusaidia kukabiliana na hali mbalimbali zinazosababishwa na mambo tofauti-tofauti,” asema mwanamume mmoja mwenye maradhi ya kutetemeka. Kwa kweli, kicheko chaweza kuwa dawa bora. Mithali 17:22 yasema: “Moyo uliochangamka ni dawa nzuri.” Hata kucheka kwa dakika chache kwaweza kuboresha afya yako. Isitoshe, “tofauti na matibabu mengine tunayojaribu, kicheko ni salama kabisa, hakina madhara, na kinaburudisha,” asema mtungaji Susan Milstrey Wells, ambaye pia ana ugonjwa wa kudumu. “Tunapocheka tunaepuka msononeko.”
-
-
Kuishi kwa Mafanikio na Ugonjwa Wako—Jinsi Gani?Amkeni!—2001 | Januari 22
-
-
Mathalani, Lex na Tineke, waliotajwa awali, walifaulu kusafiri ng’ambo. “Mwanzoni, tulikuwa na wasiwasi kidogo,” asema Lex, “lakini tulikuwa na likizo ya kupendeza sana!” Kwa kweli, huenda ukaishi na ugonjwa wako, lakini si lazima ugonjwa huo udhibiti maisha yako.
Pata nguvu kwa kuwa na imani. Wakristo wa kweli ambao wamefaulu kukabiliana na ulemavu mbaya wanasema kwamba imani yao kwa Yehova Mungu na pia ushirika wao na kutaniko la Kikristo ni vyanzo vya faraja na nguvu daima.c Yafuatayo ni baadhi ya maelezo yao kuhusu umuhimu wa kusali, kujifunza Biblia, kutafakari kuhusu wakati ujao, na kuhudhuria mikutano ya Kikristo kwenye Jumba la Ufalme.
● “Bado mimi hushuka moyo mara kwa mara. Hilo linapotukia, mimi husali kwa Yehova, naye huimarisha tena azimio langu la kuendelea kufanya yote niwezayo.”—Zaburi 55:22; Luka 11:13.
● “Kusoma Biblia na kutafakari yale ninayosoma hunisaidia sana kudumisha amani yangu ya akili.”—Zaburi 63:6; 77:11, 12.
● “Funzo la Biblia hunikumbusha kwamba uhai halisi utakuja wakati ujao na kwamba sitakuwa kilema milele.”—Isaya 35:5, 6; Ufunuo 21:3, 4.
● “Kuwa na imani katika wakati ujao ulioahidiwa katika Biblia hunitia nguvu kushughulika na maisha siku kwa siku.”—Mathayo 6:33, 34; Waroma 12:12.
● “Kuhudhuria mikutano kwenye Jumba la Ufalme hunisaidia nikazie akili mambo yajengayo wala si ugonjwa wangu.”—Zaburi 26:12; 27:4.
● “Ushirika wenye kutia moyo na washiriki wa kutaniko huuchangamsha moyo wangu.”—Matendo 28:15.
-
-
Kuishi kwa Mafanikio na Ugonjwa Wako—Jinsi Gani?Amkeni!—2001 | Januari 22
-
-
Ng’amua kwamba hata ukiwa na mtazamo chanya, unaweza kuwa na siku mbaya au majuma ambayo athari za ugonjwa wako hukulemea sana. Hata hivyo, yaelekea utaona maendeleo baada ya muda. Ndivyo ilivyokuwa kwa mwanamke mmoja, aliyesema hivi: “Nilisisimuka sana nilipotambua kwamba kwa siku nzima sikuwa nimefikiria kansa yangu. . . . Muda fulani uliopita, singeweza kamwe kudhani kwamba hilo lingewezekana.”
-