-
“Zawadi Zikiwa Wanadamu” Huchunga Kundi la Mungu kwa HamuHuduma ya Ufalme—2002 | Machi
-
-
3 Kuwatia Moyo Wasiotenda: Wazee wanajitahidi sana kuwatia moyo wale wasio wa kawaida au wasiotenda, wakiwasaidia kurudia utendaji wao wa kutaniko kwa ukawaida. Ziara za wachungaji wenye upendo zimesaidia wengi wahudhurie mikutano ya kutaniko kwa ukawaida na kujengwa kiroho hivi kwamba wameanza kushiriki tena katika huduma ya shambani. Jitihada zote hizo za wazee huonyesha upendo wa Yehova na uongozi wa Yesu Kristo. Aliweka kielelezo cha kuonyesha anawajali kondoo wake wowote ambao huenda wakawa wamekengeuka au kupotea.—Mt. 18:12-14; Yn. 10:16, 27-29.
-
-
“Zawadi Zikiwa Wanadamu” Huchunga Kundi la Mungu kwa HamuHuduma ya Ufalme—2002 | Machi
-
-
5 Wakristo fulani waliojiweka wakfu wameacha kushirikiana na kutaniko, na kuwa wasiotenda kiroho kwa sababu wamelemewa na magonjwa, matatizo ya kiuchumi, au misongo ya familia. Bila kuwachambua, wazee wanaweza kuwahakikishia kwa fadhili kwamba Yehova huwajali kondoo wake wote naye atawategemeza katika hali ngumu. (Zab. 55:22; 1 Pet. 5:7) Wachungaji wa kundi walio macho wanaweza kuwasaidia watambue kwamba ‘wakimkaribia Mungu, atawakaribia,’ na kuwapa faraja na pumziko.—Yak. 4:8; Zab. 23:3, 4.
-