Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yehova Hubariki Ibada Safi
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Yehova Anachukia Ibada ya Kiunafiki

      7, 8. Yehova anaionaje ibada ya kidesturi ya wanafiki wa kidini?

      7 Wakati Isaya anapotafakari juu ya watu walioishi wakati mmoja naye, anajua sana kwamba ni wachache wenye mwelekeo ambao Yehova huutafuta katika waabudu wake. Kwa sababu hiyo, Yerusalemu lenye uasi-imani linaistahili ile hukumu inayokaribia kulipata. Angalia jinsi Yehova anavyoiona ibada inayoendelea ndani ya jiji hilo: “Yeye achinjaye ng’ombe ni kama yeye amwuaye mtu; na yeye atoaye dhabihu ya mwana-kondoo ni kama yeye avunjaye shingo ya mbwa; na yeye atoaye matoleo ni kama yeye atoaye damu ya nguruwe; na yeye afukizaye uvumba ni kama yeye abarikiye sanamu; naam, wamezichagua njia zao wenyewe, na nafsi zao zafurahia machukizo yao.”—Isaya 66:3.

      8 Maneno haya yanatukumbusha maneno ya Yehova yaliyoandikwa katika sura ya kwanza ya Isaya. Hapo Yehova aliwaambia watu wake wapotovu kwamba, licha ya yeye kutopendezwa na vitendo vyao vya kufuata desturi rasmi tu ya ibada, kwa kweli vitendo hivyo vilizidisha pia hasira yake ya uadilifu kwa sababu waabudu hao walikuwa wanafiki. (Isaya 1:11-17) Vivyo hivyo, sasa Yehova anafananisha matoleo yao na vitendo vya uhalifu mbaya sana. Hawawezi kuutuliza moyo wa Yehova kwa kumtolea dhabihu ya ng’ombe dume wa bei kubwa, kama vile tu wasivyoweza kuutuliza kwa kuua binadamu kimakusudi! Dhabihu nyingine zinafananishwa na kutoa toleo la mbwa au nguruwe, wanyama wachafu chini ya Sheria ya Kimusa, tena wasiofaa kamwe kutolewa kama dhabihu. (Mambo ya Walawi 11:7, 27) Je, Yehova anauachilia unafiki huo wa kidini bila kutoa adhabu?

      9. Wayahudi walio wengi wameitikiaje vikumbusha vya Yehova kupitia Isaya, na kutakuwa na matokeo gani yasiyoepukika?

      9 Sasa Yehova anasema hivi: “Mimi nami nitachagua mapigo yao, nitaleta hofu zao juu yao; kwa sababu nilipoita, hawakuitika;na niliponena,hawakusikia; bali walifanyayaliyo maovu machoni pangu, na kuyachagua nisiyoyafurahia.” (Isaya 66:4) Bila shaka Isaya anaweza kuyatamka maneno haya kwa usadikisho wa moyoni. Kwa muda wa miaka mingi amekuwa chombo cha Yehova, huku ‘akiita’ watu Wake na ‘kunena’ nao. Nabii anajua sana kwamba, kwa ujumla hakuna mtu amekuwa akisikiliza. Kwa sababu wameendelea kutenda mabaya, hawawezi kukosa adhabu. Kweli Yehova atachagua adhabu yao na kuwaletea watu wake waasi-imani matukio yenye kutisha.

  • Yehova Hubariki Ibada Safi
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 11. (a) Ni nini kinachoongezea dhambi ya waasi-imani katika siku za Isaya? (b) Watu wanaoishi wakati mmoja na Isaya wanawatupaje waaminifu ‘kwa ajili ya jina la Mungu’?

      11 Isaya anaendelea kusema hivi: “Lisikilizeni neno la BWANA, ninyi mtetemekao kwa sababu ya neno lake; Ndugu zenu wawachukiao ninyi, waliowatupa kwa ajili ya jina langu, wamesema, Na atukuzwe BWANA, tupate kuiona furaha yenu; lakini watatahayarika.” (Isaya 66:5) “Ndugu” za Isaya, ambao ni wananchi wenzake hasa, ndio wanaopaswa kubeba daraka walilopewa na Mungu la kumwakilisha Yehova Mungu na kutii enzi yake kuu. Wameshindwa kufanya hivyo wakawa na dhambi nzito kweli kweli. Lakini kinachoongezea dhambi yao ni kwamba wanawachukia wanaume walio waaminifu na wanyenyekevu, kama vile Isaya. Waasi-imani hao wanawachukia waaminifu na kuwatupa kwa sababu wanamwakilisha Yehova Mungu kwa njia ya kweli. Ni katika maana hiyo kwamba waaminifu hao wanatupwa ‘kwa ajili ya jina la Mungu.’ Wakati huo huo, watumishi hawa wa Yehova wasio wa kweli wanadai kumwakilisha, wakijifanya eti wanamcha Mungu sana kwa kutumia maneno yanayosikika kama ya kidini, kama vile ‘Yehova na atukuzwe!’a

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki