-
Je, Una Sababu ya Kuamini Kwamba Kutakuwa na Paradiso?Mnara wa Mlinzi—2004 | Oktoba 15
-
-
a Katika kitabu The Geography of the Bible, Denis Baly anasema: “Lazima aina ya mimea iliyokuwako nyakati za Biblia iwe ilibadilika sana.” Kwa sababu gani? ‘Kwa kuwa wanadamu walihitaji miti kwa ajili ya kuni na ujenzi, walianza kukata miti na hivyo kufanya nchi iathiriwe na uharibifu unaotokana na hali ya hewa. Pole kwa pole, ukataji huo wa miti ulifanya hali ya hewa iwe kisababishi kikuu cha uharibifu huo.’
-
-
Je, Una Sababu ya Kuamini Kwamba Kutakuwa na Paradiso?Mnara wa Mlinzi—2004 | Oktoba 15
-
-
16, 17. (a) Nyakati za hivi karibuni, nchi hiyo inatofautianaje na Nchi ya Ahadi ya nyakati za kale? (b) Kwa nini tunaweza kuamini kwamba wakati fulani Nchi ya Ahadi ilikuwa kama paradiso?
16 Ikiwa maoni yako kuhusu nchi hiyo yanategemea jinsi ambavyo eneo hilo limekuwa hivi karibuni, huenda ukadhani kwamba hilo lilikuwa eneo kame na lenye mchanga, lenye majangwa ya mawe-mawe, na joto kali. Hata hivyo, kuna sababu ya kuamini kwamba eneo hilo lote lilikuwa tofauti kabisa nyakati za Biblia. Katika jarida Scientific American, mtaalamu wa kilimo, Dakt. Walter C. Lowdermilk alisema kwamba nchi hiyo “imeharibika kwa sababu ya kutumiwa vibaya kwa miaka mingi.” Mtaalamu huyo aliandika: “Nchi hiyo yenye kupendeza sasa imekuwa ‘jangwa’ kwa sababu ya wanadamu wala si kwa sababu ya hali za kiasili.” Hata uchunguzi wake ulionyesha kwamba “pindi fulani nchi hiyo ilikuwa paradiso ya malisho.” Hivyo ni wazi kwamba wanadamu wametumia vibaya na kuharibu nchi ambayo ilikuwa “paradiso ya malisho.”a
-