-
Je, Hizi Ndizo Siku za Mwisho Kwelikweli?Mnara wa Mlinzi—1997 | Aprili 1
-
-
a Tito alikuwa kwenye upande wa ushindi kwa wazi. Hata hivyo, hakutimiza mambo mawili aliyotaka. Aliwapa nafasi ya kujisalimisha kwa amani, lakini viongozi wa hilo jiji walikataa kwa ushupavu, na isivyoelezeka. Na hatimaye kuta za jiji zilipobomolewa, aliamuru kwamba hekalu lisiharibiwe. Hata hivyo lilichomwa kabisa! Unabii wa Yesu ulikuwa umeonyesha kwa wazi kwamba Yerusalemu lingeangamizwa kabisa na kwamba hekalu lingebomolewa kabisa.—Marko 13:1, 2.
-
-
Je, Hizi Ndizo Siku za Mwisho Kwelikweli?Mnara wa Mlinzi—1997 | Aprili 1
-
-
Wafuasi wa Yesu Wauliza Swali Lenye Maana
Ni lazima wafuasi wa Yesu walishangaa. Yesu alikuwa ametoka tu kuwaambia waziwazi, kwamba majengo ya hekalu la Yerusalemu yenye kuvutia yangeharibiwa kabisa! Utabiri huo ulikuwa wenye kustaajabisha. Upesi baadaye, walipokuwa wameketi juu ya Mlima wa Mizeituni, wanne kati ya wanafunzi walimwuliza Yesu hivi: “Tuambie, Ni wakati gani mambo haya yatakuwa, nayo itakuwa ni nini ishara ya kuwapo kwako na ya umalizio wa mfumo wa mambo?” (Mathayo 24:3; Marko 13:1-4) Wawe waling’amua au la, jibu la Yesu lingekuwa na matumizi zaidi ya moja.
-
-
Je, Hizi Ndizo Siku za Mwisho Kwelikweli?Mnara wa Mlinzi—1997 | Aprili 1
-
-
Mwisho wa Yerusalemu
Kwanza fikiria yale aliyosema Yesu juu ya Yerusalemu na hekalu lalo. Miongo zaidi ya mitatu mapema, alitabiri wakati wa magumu mabaya kwa mojawapo ya majiji makubwa zaidi ulimwenguni. Ona hasa maneno yake yaliyorekodiwa kwenye Luka 21:20, 21: “Mwonapo Yerusalemu limezingirwa na majeshi yaliyopiga kambi, ndipo jueni kwamba kufanywa ukiwa kwalo kumekaribia. Ndipo waacheni wale walio katika Yudea waanze kukimbia hadi kwenye milima, na waacheni wale walio katikati yalo waondoke, na waacheni wale walio katika sehemu za mashambani wasiingie ndani yalo.” Ikiwa Yerusalemu lingezungukwa, kuzingirwa na majeshi yaliyopiga kambi, “wale walio katikati yalo” wangeweza ‘kuondokaje’ tu, kama vile Yesu alivyokuwa ameamuru? Kwa wazi, Yesu alikuwa akidokeza kwamba kipindi chenye fursa kingetokea. Je, kilitokea?
Mwaka wa 66 W.K., majeshi ya Waroma chini ya amri ya Sesho Galo yalikuwa yameyarudisha majeshi ya uasi ya Kiyahudi Yerusalemu na kuyafungia jijini humo. Waroma hata walilipiga jiji hilo lenyewe hata wakafikia ukuta wa hekalu. Lakini ndipo Galo alipoyaelekeza majeshi yake yafanye jambo la kushangaza kikweli. Aliyaamuru yaondoke! Kwa kusisimuka askari-jeshi Wayahudi walianza kufuatia na kudhuru maadui wao Waroma waliokuwa wakikimbia. Hivyo, kipindi chenye fursa alichotabiri Yesu kikatokea. Wakristo wa kweli walitii onyo lake wakatoka Yerusalemu. Huo ulikuwa uamuzi wenye hekima, kwa kuwa miaka minne tu baadaye, Majeshi ya Waroma yalikuwa yamerudi, yakiongozwa na Jemadari Tito. Wakati huu kuponyoka kusingewezekana.
Majeshi ya Waroma yalizunguka Yerusalemu tena; yalijenga boma lenye miti iliyochongoka kulizingira. Yesu alikuwa ametabiri hivi kuhusu Yerusalemu: “Siku zitakuja juu yako wakati maadui wako watakapojenga kukuzunguka wewe boma lenye miti iliyochongoka nao watakuzunguka na kukutaabisha kutoka kila upande.”a (Luka 19:43) Upesi, Yerusalemu lilianguka; hekalu lalo tukufu likafanywa magofu yenye kufuka moshi. Maneno ya Yesu yalitimizwa kabisa!
-