-
Kuijua “Akili ya Kristo”Mnara wa Mlinzi—2000 | Februari 15
-
-
Yosefu pia alikuwa mtu mwenye kumcha Mungu. Kwa uaminifu, yeye alifunga safari ya kilometa 150 kwenda Yerusalemu kila mwaka kwa ajili ya Sikukuu ya Kupitwa. Maria pia alihudhuria, hata ingawa ni wanaume tu waliokuwa na wajibu wa kuhudhuria. (Kutoka 23:17; Luka 2:41) Katika pindi moja kama hiyo, Yosefu na Maria walimpata Yesu mwenye umri wa miaka 12 hekaluni akiwa katikati ya walimu baada ya kumtafuta sana. Yesu akawaambia wazazi wake waliokuwa na wasiwasi: “Je, hamkujua kwamba ni lazima mimi niwe katika nyumba ya Baba yangu?” (Luka 2:49) “Baba”—ni lazima neno hilo liwe lilitokeza hisia nzuri ya upendo kwa kijana Yesu. Kwanza, yaonekana alikuwa ameambiwa kwamba Yehova ndiye Baba yake halisi. Na zaidi, ni lazima Yosefu alikuwa baba-mlezi mzuri kwa Yesu. Kwa kweli Yehova hangemchagua mtu mkali wala mkatili amlee Mwana Wake mpendwa!
11. Yesu alijifunza ufundi gani, na katika nyakati za Biblia, kazi hiyo ilihusisha nini?
11 Katika miaka aliyokaa Nazareti, Yesu alijifunza useremala, yaelekea kutoka kwa babake mlezi, Yosefu. Yesu alikuwa stadi sana hivi kwamba yeye mwenyewe aliitwa “seremala.” (Marko 6:3)
-
-
Kuijua “Akili ya Kristo”Mnara wa Mlinzi—2000 | Februari 15
-
-
12. Ni nini kinachoonyesha kwamba yaelekea Yosefu alikufa kabla ya Yesu, na jambo hilo lingemaanisha nini kwa Yesu?
12 Akiwa mtoto wa kwanza, yaelekea Yesu alisaidia kutunza familia, hasa kwa sababu inaonekana Yosefu alikufa kabla ya Yesu.b Gazeti Zion’s Watch Tower la Januari 1, 1900, lilisema: “Mapokeo yanaonyesha kwamba Yosefu alikufa Yesu akiwa angali mchanga, na kwamba [Yesu] alianza useremala ili kuiruzuku familia. Jambo hilo laungwa mkono na ushuhuda wa Kimaandiko mahali ambapo Yesu mwenyewe anaitwa seremala, na mamake na ndugu zake wanatajwa, lakini Yosefu hatajwi. (Marko 6:3) . . . Basi inawezekana kwamba kile kipindi kirefu cha miaka kumi na minane ya maisha ya Bwana wetu, tokea wakati wa lile tukio [linalotajwa kwenye Luka 2:41-49] hadi wakati alipobatizwa, alikitumia kufanya mambo ya kawaida maishani.” Yaelekea Maria na watoto wake, kutia ndani Yesu, walihuzunishwa na kifo cha mume na baba mpendwa.
-
-
Kuijua “Akili ya Kristo”Mnara wa Mlinzi—2000 | Februari 15
-
-
b Mara ya mwisho ambapo Yosefu anatajwa moja kwa moja ni wakati Yesu mwenye umri wa miaka 12 alipopatikana hekaluni. Yosefu hatajwi kuwapo kwenye sherehe ya arusi kule Kana, mwanzoni mwa huduma ya Yesu. (Yohana 2:1-3) Mwaka wa 33 W.K., Yesu aliyetundikwa mtini alimkabidhi Maria kwa mtume mpendwa Yohana ili amtunze. Yaelekea Yesu hangalifanya hivyo kama Yosefu angalikuwa bado hai.—Yohana 19:26, 27.
-