-
Yehova Amkweza Mtumishi Wake wa KimesiyaUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
5. (a) Wasomi fulani Wayahudi wameonyesha matumizi gani kuhusu unabii wa Isaya? (Ona kielezi-chini.) (b) Yule Mtumishi anatambulishwa wazi kuwa nani katika kitabu cha Biblia cha Matendo?
5 Kabla ya kufika kwa Ukristo, na kwa kadiri fulani wakati wa zile karne za mapema za Wakati wa Kawaida, wasomi wachache Wayahudi walitumia unabii huu kumhusu Mesiya. Usahihi wa kutumia unabii huo kwa njia hiyo unaonekana katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo. Kitabu cha Matendo kinaripoti kwamba yule towashi Mwethiopia aliposema kuwa hajui ni nani anayetambuliwa kuwa Mtumishi wa unabii wa Isaya, Filipo ‘alimtangazia habari njema juu ya Yesu.’ (Matendo 8:26-40; Isaya 53:7, 8) Vivyo hivyo, vitabu vingine vya Biblia humtambulisha Yesu Kristo kuwa ndiye Mtumishi wa Kimesiya wa unabii wa Isaya.a
-
-
Yehova Amkweza Mtumishi Wake wa KimesiyaUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
a Targumi ya Jonathan ben Uzziel (karne ya kwanza W.K.), iliyotafsiriwa na J. F. Stenning, inasema hivi inapofasiri Isaya 52:13: “Tazama, mtumishi wangu, Yule Mtiwa-Mafuta (au, yule Mesiya), atapata ufanisi.” Hivyo hivyo, Talmudi ya Kibabiloni (karibu karne ya tatu W.K.) inasema hivi: “Yule Mesiya—jina lake nani? . . . [; wale] wa nyumba ya Rabi [husema, Yule mgonjwa], kwa kuwa inasemwa, ‘Hakika yeye amebeba magonjwa yetu.’”—Sanhedrin 98b; Isaya 53:4.
-