-
Yesu ‘Aimarisha Haki Duniani’Mkaribie Yehova
-
-
16, 17. (a) Yesu alionyeshaje haki alipohubiri habari njema za Ufalme wa Mungu? (b) Yesu alionyeshaje kwamba haki yake ilikuwa yenye rehema?
16 Pili, Yesu alionyesha haki alipohubiri habari njema za Ufalme wa Mungu. Hakuwa na ubaguzi. Badala yake, alijitahidi sana kuwahubiria watu wa kila aina, matajiri kwa maskini. Tofauti na Yesu, Mafarisayo waliwapuuza watu maskini wa kawaida na kuwaita kwa madharau ʽam-ha·ʼaʹrets, yaani, “watu wa ardhi.” Kwa ujasiri, Yesu alipinga ukosefu huo wa haki. Alipowafundisha watu habari njema, alipokula nao, alipowalisha, alipowaponya, au hata kuwafufua, aliunga mkono haki ya Mungu ambaye anataka “watu wa namna zote” waokolewe.c—1 Timotheo 2:4.
-
-
Yesu ‘Aimarisha Haki Duniani’Mkaribie Yehova
-
-
c Mafarisayo waliamini kwamba watu wa hali ya chini, ambao hawakujua Sheria, walikuwa watu “waliolaaniwa.” (Yohana 7:49) Walisema kwamba mtu hakupaswa kuwafundisha watu hao wala kufanya biashara nao wala kula nao wala kusali nao. Walisema kwamba mtu akimruhusu binti yake aolewe na mmoja wao lingekuwa jambo baya kuliko kumpeleka kwa wanyama wakali sana. Waliamini kwamba watu hao wa hali ya chini hawatafufuliwa.
-