-
Kutoa Ushahidi kwa Watu wa Lugha na Dini ZoteHuduma ya Ufalme—1998 | Februari
-
-
23 Kutoa Ushahidi kwa Wayahudi: (Ona sura ya 9 katika kitabu Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu.) Tofauti na dini zile nyingine zisizo za Kikristo, Dini ya Kiyahudi imetia mizizi katika historia, si mithiolojia. Kupitia Maandiko ya Kiebrania yaliyopulizwa, kiungo muhimu chatolewa katika jitihada ya wanadamu ya kumtafuta Mungu wa kweli. Lakini, tofauti na Neno la Mungu, fundisho la msingi la Dini ya Kiyahudi ya kisasa ni itikadi katika nafsi ya kibinadamu isiyoweza kufa. Msingi wa masikilizano waweza kuanzishwa kwa kuthibitisha kwamba twaabudu Mungu wa Abrahamu na kwa kukubali kwamba sisi hukabili magumu yaleyale katika ulimwengu wa leo.
24 Ukikutana na Myahudi asiye na imani katika Mungu, kumwuliza kama sikuzote amehisi hivyo huenda kukakusaidia ufahamu ni nini kitakachomvutia zaidi. Kwa mfano, huenda ikawa hajapata kusikia kamwe maelezo yenye kuridhisha juu ya sababu imfanyayo Mungu aruhusu kuteseka. Wayahudi wenye moyo mweupe wanaweza kutiwa moyo kuchunguza upya utambulisho wa Yesu akiwa Mesiya, si kupitia kuwakilishwa kwake vibaya na Jumuiya ya Wakristo, bali katika njia ambayo waandikaji Wayahudi wa Maandiko ya Kigiriki wanavyomweleza.
-
-
Kutoa Ushahidi kwa Watu wa Lugha na Dini ZoteHuduma ya Ufalme—1998 | Februari
-
-
Wayahudi
Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote? (Broshua)
Mashahidi wa Yehova—Huamini Nini? (Trakti Na. 18)
A Peaceful New World—Will It Come? (Trakti Na. 17)
-