Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Hekima ya “Neno la Mungu”
    Mkaribie Yehova
    • 14, 15. Biblia inatuambia nini kuhusu mwanamke fulani aliyekuja hekaluni, na simulizi hilo linatufundisha nini kumhusu Yehova?

      14 Masimulizi halisi yaliyo katika Biblia mara nyingi yanatufundisha kuhusu utu wa Yehova. Fikiria simulizi la mwanamke fulani ambaye Yesu alimwona hekaluni. Alipokuwa ameketi karibu na masanduku ya hazina, Yesu aliangalia jinsi watu walivyokuwa wakitumbukiza michango yao humo. Matajiri wengi walikuja na kutumbukiza “kutokana na ziada yao.” Lakini Yesu alimtazama sana mjane mmoja maskini. Mjane huyo alitoa mchango wa “sarafu ndogo mbili, ambazo zina thamani ndogo sana.”b Alitoa fedha zote alizokuwa nazo. Yesu, ambaye alidhihirisha kikamili maoni ya Yehova, alisema hivi: ‘Mjane huyu maskini alitumbukiza ndani zaidi ya wote wale waliokuwa wakitumbukiza fedha ndani ya masanduku ya hazina.’ Kulingana na maneno hayo, alitumbukiza fedha nyingi kuliko jumla ya fedha zilizotolewa na watu wengine wote.—Marko 12:41-44; Luka 21:1-4; Yohana 8:28.

      15 Je, haishangazi kwamba kati ya watu wote waliokuja hekaluni siku hiyo, ni mjane huyo peke yake ndiye aliyetajwa katika Biblia? Kupitia mfano huo, Yehova anatufundisha kwamba yeye ni Mungu anayethamini mambo tunayofanya. Anakubali kwa furaha michango tunayomtolea kwa nafsi yetu yote, pasipo kuilinganisha na michango inayotolewa na wengine. Bila shaka Yehova ametumia njia bora sana kutufundisha ukweli huo wenye kutia moyo!

  • Hekima ya “Neno la Mungu”
    Mkaribie Yehova
    • 18, 19. (a) Kwa nini hatupaswi kutatanika wakati simulizi fulani la Biblia linazusha maswali ambayo hatuwezi kujibu mara moja? (b) Tunahitaji kufanya nini ili kufahamu Neno la Mungu, na jambo hilo linaonyeshaje hekima kuu ya Yehova?

      18 Kwa upande mwingine, tunapojifunza Biblia kwa uangalifu na kwa unyofu, tunapata kumjua Yehova kama anavyofafanuliwa katika Biblia nzima. Kwa hiyo, hatutataniki wakati simulizi fulani linazusha maswali ambayo hatuwezi kupata jibu mara moja. Kwa mfano: Tunapounganisha vipande vya mchezo wa chemshabongo, huenda tusipate kipande fulani mwanzoni au huenda tusielewe jinsi kipande fulani kinavyoungana na vingine. Lakini, labda tumeunganisha vipande vya kutosha kutusaidia kuelewa jinsi picha kamili itakavyokuwa. Vivyo hivyo, tunapojifunza Biblia, pole kwa pole tunajifunza jinsi Yehova Mungu alivyo, na hatimaye tunapata kumjua vizuri kabisa. Hata ikiwa mwanzoni hatuelewi simulizi fulani au hatuoni jinsi linavyopatana na utu wa Mungu, tayari tumejifunza kupitia funzo letu la Biblia mambo mengi sana ya kutusadikisha kwamba bila shaka Yehova ni Mungu mwenye upendo, asiyependelea, na mwenye haki.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki