-
Ripoti ya Ulimwenguni Pote2006 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Kyrgyzstan: Svetlana, ambaye ni painia msaidizi, hakuweza kumpata mtu yeyote katika nyumba fulani kwenye eneo lake. Siku moja alipokuwa kwenye eno hilo, aliamua tena kubisha mlango wa nyumba hiyo ingawa hakudhani angempata yeyote. Alishangaa na kufurahi alipomkuta mwanamke fulani kijana. Mwanamke huyo alifurahi sana kutembelewa na Shahidi wa Yehova naye akasema kwamba alikuwa akijifunza Biblia hapo awali, lakini hakujua jinsi ambavyo angeweza kuwapata tena akina ndugu. Svetlana alimuuliza kama angependa kupata magazeti kwa ukawaida. Mwanamke huyo alijibu kwamba anataka magazeti na pia funzo la Biblia. Funzo lilianzishwa mara moja, na sasa mwanamke huyo huhudhuria mikutano ya Kikristo.
-
-
Ripoti ya Ulimwenguni Pote2006 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha katika ukurasa wa 43]
Svetlana, Kyrgyzstan
-