Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutumika Katika Kutaniko la Lugha ya Kigeni
    Mnara wa Mlinzi—2006 | Machi 15
    • Endelea Kufanya Maendeleo

      Monifa anasema hivi: “Kujifunza lugha nyingine ndiyo kazi ngumu zaidi ambayo nimewahi kufanya. Kuna nyakati nimetamani kuacha. Lakini mimi hukumbuka jinsi mwanafunzi wangu wa Biblia anavyopenda kusikiliza kweli za kiroho katika Kikorea changu kibaya na shangwe ambayo akina ndugu wanaonyesha ninapofanya hata maendeleo madogo.” Jambo kuu ni kwamba, usikate tamaa haraka. Mradi wako ni kuweza kuwafundisha wengine kweli za Kimaandiko zinazookoa uhai. (1 Wakorintho 2:10) Hivyo, kujifunza kufundisha Biblia katika lugha nyingine kunahitaji uwe makini na ujitahidi kwa muda mrefu. Unapoendelea kujifunza, epuka kulinganisha isivyofaa maendeleo yako na ya wengine. Wale wanaojifunza lugha mpya hawafanyi maendeleo kwa kadiri ileile wala kwa njia ileile. Hata hivyo, ni muhimu kutambua maendeleo yako mwenyewe. (Wagalatia 6:4) Joon ambaye ameanza kujifunza Kichina anasema hivi: “Kujifunza lugha ni kama kupanda ngazi. Unapohisi kwamba hufanyi maendeleo, ndipo unapotambua kwamba umefanya maendeleo makubwa.”

      Kujifunza lugha mpya ni kazi inayoendelea muda wote wa maisha yako. Kwa hiyo, furahia kujifunza lugha mpya, na usitarajie ukamilifu. (Zaburi 100:2) Hatuwezi kuepuka kufanya makosa. Kukosea ni mojawapo ya njia za kujifunza. Alipoanza kuhubiri katika Kiitaliano, Mkristo mmoja alimwuliza mwenye nyumba, “Je, unajua ufagio wa maisha?” Alikuwa akimaanisha, “kusudi la maisha.” Shahidi mmoja aliyekuwa anajifunza Kipolishi alialika kutaniko kuimba mbwa badala ya wimbo. Mwingine aliyekuwa akijifunza Kichina alipobadili matamshi kidogo tu, aliwahimiza wasikilizaji wake wawe na imani katika mkoba wa vitabu wa Yesu badala ya kuwa na imani katika dhabihu ya Yesu. Kukosea humsaidia mtu kukumbuka kabisa maneno sahihi aliyojifunza.

  • Kutumika Katika Kutaniko la Lugha ya Kigeni
    Mnara wa Mlinzi—2006 | Machi 15
    • Mtu mzima anaweza kudhoofika kiakili, kihisia, na kiroho asipoweza kuwasiliana vizuri kwa miezi mingi au hata kwa miaka mingi. Janet, ambaye sasa anazungumza vizuri Kihispania, anakumbuka: “Nilifadhaika sana kwa sababu ya kupungukiwa kwangu.” Hiroko, ambaye alijifunza Kiingereza, anakumbuka akiwaza hivi: ‘Hata mbwa na paka wa eneo hili wanaelewa Kiingereza vizuri zaidi kuliko mimi.’ Halafu Kathie anasema hivi: “Kabla ya kuhamia kutaniko la Kihispania, nilikuwa na mafunzo mengi ya Biblia na ziara za kurudia, lakini baada ya kuhamia kutaniko hilo sikuwa na funzo la Biblia wala ziara ya kurudia. Nilihisi kwamba sikuwa nikifanya chochote.”

      Katika hali kama hiyo, ni muhimu kuwa na mtazamo unaofaa. Alipovunjika moyo, Hiroko alifikiri hivi: “Ikiwa wengine wanaweza kujifunza lugha nyingine, mimi pia ninaweza.” Kathie anasema: “Nilifikiri kuhusu mume wangu, ambaye anafanya maendeleo mazuri na kutimiza mengi kutanikoni. Hilo lilinisaidia kushinda matatizo mwanzoni, na hivyo nikaanza kufanya maendeleo makubwa zaidi. Bado nina mengi ya kujifunza, lakini hatua kwa hatua ninaweza sasa kuhubiri na kufundisha, na hilo hunifurahisha.” Mume wake Jeff, anaongeza hivi: “Inaweza kuvunja moyo kutoelewa kila jambo linalosemwa wakati wa matangazo na kwenye mikutano ya wazee. Ninahitaji kuwa mnyoofu na mnyenyekevu ili kuuliza yale yaliyosemwa. Hata hivyo akina ndugu wanafurahi kunisaidia.”

      Ili kuepuka uchovu wa kiroho unaposhirikiana na kutaniko linalotumia lugha ya kigeni, unapaswa kutilia maanani hali yako ya kiroho. (Mathayo 5:3) Kazuyuki, ambaye kwa miaka mingi ametumika katika eneo la Kireno, anasema hivi: “Ni muhimu tule chakula cha kutosha cha kiroho. Kwa sababu hiyo, tukiwa familia, tunajifunza na kutayarisha mikutano katika lugha yetu ya asili na pia katika Kireno.” Mara kwa mara wengine huhudhuria mikutano inayofanywa katika lugha yao ya asili. Isitoshe, ni muhimu kupumzika vya kutosha.—Marko 6:31.

  • Kutumika Katika Kutaniko la Lugha ya Kigeni
    Mnara wa Mlinzi—2006 | Machi 15
    • Kuna thawabu kubwa kwa wale wanaoweza kutumika katika kutaniko la lugha ya kigeni. Barbara, ambaye alihamia kutaniko la Kihispania pamoja na mume wake, anasema hivi: “Hilo ni mojawapo ya mambo ambayo yameniletea furaha zaidi maishani. Ni kama ninajifunza tena kweli ya Biblia. Ninathamini sana nafasi hiyo, hasa kwa kuwa hatuwezi kuwa wamishonari katika nchi nyingine.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki