-
Latvia2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Kabla ya Vita vya Pili vya Ulimwengu, muuguzi anayeitwa Teofīlija Kalvīte aliolewa na meya wa Daugavpils. Kwa kuhuzunisha, muda mfupi baada ya vita kuanza, ilitangazwa kwamba mume wake amepotea. Teofīlija mwenyewe alipata shida nyingi na kuona mateso na vifo vingi. Baada ya vita, akawa msimamizi wa Shirika la Msalaba Mwekundu la Latvia, na serikali ikampa angalau tuzo 20 katika miaka 61 ya kazi yake ya kitiba. Teofīlija alipokuwa na miaka 65 hivi, alikutana na Shahidi anayeitwa Paulīne Serova, ambaye alimweleza yale ambayo Biblia inasema kuhusu sababu ya Mungu ya kuruhusu uovu. Teofīlija alikubali kweli, na tangu wakati huo akawa na pendeleo zuri la kuwasaidia watu kupata afya ya kiroho. Alikufa akiwa mwaminifu mwaka wa 1982.
-
-
Latvia2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha katika ukurasa wa 197]
Paulīne Serova alimweleza kweli kwa mara ya kwanza muuguzi anayeitwa Teofīlija Kalvīte
-