-
Latvia2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Miaka minne baadaye, Ferdinand alipokuwa akihubiri katika duka la kuoka mikate katika mji wa kwao wa Liepaja, alikutana na mwanamume ambaye baadaye alikuja kuwa painia mwenzake. Mwokaji huyo alienda mbio kwenye duka jirani la kinyozi aliyekuwa ndugu yake, na kumwambia, “Heinrich! Njoo haraka!” Kisha akasema: “Kuna mtu dukani kwangu ambaye anasema mambo nisiyoweza kuyaamini.” Kinyozi huyo, Heinrich Zech, hakuona vigumu kuamini kweli ya Biblia, naye akabatizwa baada ya muda mfupi. Alijiunga na Ferdinand, na wote wawili wakatembelea majiji mengi kwa baiskeli ili kueneza ujumbe wa Ufalme.
-
-
Latvia2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha katika ukurasa wa 180]
Heinrich Zech na mke wake, Elsa, mbele ya duka lao huko Liepaja
-