Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Latvia
    2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • Kisha, akina ndugu waliruhusiwa na polisi kufanya mikutano ya hadhara, na watu 975 walisikiliza hotuba za Biblia jijini Riga, Liepaja, na Jelgava. Hotuba hizo zilitolewa katika Kijerumani, lugha ya pili ya Walatvia wengi. Wengi walitaka kuwe na mikutano zaidi.

  • Latvia
    2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • Mapema mwaka wa 1927, kijana mmoja anayeitwa Ferdinand Fruck na mama yake, Emilie, walibatizwa. Miaka minne baadaye, Ferdinand alipokuwa akihubiri katika duka la kuoka mikate katika mji wa kwao wa Liepaja, alikutana na mwanamume ambaye baadaye alikuja kuwa painia mwenzake. Mwokaji huyo alienda mbio kwenye duka jirani la kinyozi aliyekuwa ndugu yake, na kumwambia, “Heinrich! Njoo haraka!” Kisha akasema: “Kuna mtu dukani kwangu ambaye anasema mambo nisiyoweza kuyaamini.” Kinyozi huyo, Heinrich Zech, hakuona vigumu kuamini kweli ya Biblia, naye akabatizwa baada ya muda mfupi. Alijiunga na Ferdinand, na wote wawili wakatembelea majiji mengi kwa baiskeli ili kueneza ujumbe wa Ufalme.

  • Latvia
    2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • Huko Liepaja, makasisi waligawanya vikaratasi vilivyosema kuwa akina ndugu hawamwamini Yesu Kristo na kuwahimiza watu wakatae vichapo vyao. Pia, walitumia gazeti kuu la kanisa kuwapaka matope Wanafunzi wa Biblia.

  • Latvia
    2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • [Picha katika ukurasa wa 180]

      Heinrich Zech na mke wake, Elsa, mbele ya duka lao huko Liepaja

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki