Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Latvia
    2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • Baada ya vita, mwisho-mwisho wa miaka ya 1940, hatimaye ofisi ya tawi ya Ujerumani ilifaulu kuwatumia barua akina ndugu huko Jelgava, Kuldīga, Riga, na Ventspils.

  • Latvia
    2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • Akina ndugu walitumia kila nafasi kuhubiri isivyo rasmi. Kwa mfano, Marta Baldone, ambaye alifanya kazi ya kuwakanda watu katika kituo cha afya huko Ventspils, aliwahubiria wateja wake. Mmoja wao ni Alexandra Preklonskaya (sasa Rezevskis). Alexandra anakumbuka hivi: “Marta alinifundisha kwamba jina la Mungu ni Yehova, nami nikalipenda sana jina hilo.”

  • Latvia
    2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • Ingawa hakuwa amebatizwa, Valija Lange, kutoka Ventspils, ni mmoja wa waliokamatwa na KGB (Halmashauri ya Usalama wa Kitaifa ya Sovieti) katika misako ya Septemba 1950. Alipohojiwa usiku wa manane huko Riga, aliulizwa: “Kwa nini unapinga serikali na wewe ni raia wa Muungano wa Sovieti?” Valija akajibu kwa utulivu na heshima: “Ninakusudia tu kumtumikia Yehova Mungu, kuelewa mafundisho yake, na kuwaeleza wengine mafundisho hayo.”

      Jina la Valija, na majina ya Mashahidi 19 wengine, yaliorodheshwa katika hati moja ya Oktoba 31, 1950.

  • Latvia
    2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • Akina ndugu waliendelea kuhubiri na kufanya wanafunzi kambini. Mmoja wa wanafunzi hao ni Jānis Garšk̗is. Alibatizwa mwaka wa 1956 na sasa anaishi Ventspils. Anasema: “Nashukuru kwamba Mungu aliacha nipelekwe katika kambi ya kazi ngumu, la sivyo singejifunza kweli.” Huo ni mtazamo mzuri kama nini!

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki