-
Latvia2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Māris Krūmin̗š, ambaye pia anatumika Betheli, alihitaji kufanya mabadiliko makubwa maishani ili amtumikie Yehova. “Baada ya kutumikia jeshini,” anasema Māris, “nilikosa mwelekeo maishani. Baadaye, nilifukuzwa chuoni kwa kukosa mihadhara fulani. Kwa sababu sikuwa na kusudi maishani, niliingilia uhalifu, na jioni moja baada ya kusababisha fujo nikiwa mlevi, nikakamatwa. Nikiwa gerezani, nilifikiria sheria ambazo nilikuwa nimevunja, nami nikagundua kwamba nyingi zinatokana na sheria za Mungu. Kwa mara ya kwanza maishani, nilimwomba Mungu msamaha na kuahidi kwamba nitamtafuta.
“Baada ya kuachiliwa kutoka gerezani, nilienda katika makanisa mbalimbali lakini kila mara nilitamaushwa. Hivyo, nilianza kusoma Biblia na vitabu vingine vya dini. Mwaka wa 1990, nilipokuwa ndani ya gari-moshi, nilikutana na mtu ambaye tulikuwa tumesomea shule moja, naye akanieleza kwamba yeye ni Shahidi wa Yehova. Katika safari hiyo fupi, Yehova alifungua moyo wangu nilipokuwa nikimsikiliza rafiki yangu wa zamani akinieleza kusudi la Mungu kwa wanadamu na sababu ya mateso yaliyo ulimwenguni. Nilianza kujifunza, kisha nikawa mhubiri mwaka wa 1991. Nilibatizwa 1992. Mwaka mmoja baadaye, nikawa mshiriki wa familia ya Betheli ya Latvia, na mwaka wa 1995 nikamwoa Simona, painia kutoka Finland.”
-
-
Latvia2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha katika ukurasa wa 207]
Akiwa gerezani, Māris Krūmin̗š alisali kwa Mungu kwa mara ya kwanza
-