-
Latvia2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
IMANI YA KIKRISTO INAJARIBIWA
Mwaka wa 1993, imani ya wanafunzi wanne wa muziki jijini Jelgava ilijaribiwa wakati kwaya yao ilipoagizwa kuimba katika sherehe ya Siku ya Uhuru. Ingawa walikuwa wapya katika kweli, wasichana hao waliazimia kumpendeza Mungu. Kwa hiyo, walimwandikia msimamizi wa kwaya na kumwomba kwa heshima awaruhusu wasihudhurie maadhimisho hayo kwa sababu ya dhamiri yao ya Kikristo. Msimamizi huyo alitendaje? Aliwaandikia wazazi wa wasichana hao barua yenye masharti makali, akisema kwamba wanafunzi hao watafukuzwa shuleni wasipoimba. Sawa na wale Waebrania watatu, wasichana hao walimtii Yehova.—Dan. 3:14, 15, 17; Mdo. 5:29.
Mmoja wa wasichana hao ni Dace Puncule. Anakumbuka hivi: “Kusali kwa Mungu na msaada wa akina ndugu ulitusaidia kuendelea kuwa waaminifu. Tulifukuzwa, lakini sijuti kamwe kwamba nilisimama imara kwa ajili ya kweli. Kusema kweli, Yehova amenitunza sana. Baada ya miezi kadhaa, nilipata kazi katika ofisi ya sheria, na uzoefu niliopata huko ulinisaidia baadaye Betheli, ambako nimetumika tangu 2001.”
-
-
Latvia2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha katika ukurasa wa 210]
Dace Puncule alifukuzwa shuleni kwa kukataa kuimba nyimbo za kitaifa
-