-
Latvia2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Mwaka huohuo, Margaret (Madge) Brown, painia kutoka Scotland aliyetumikia Ireland na kubatizwa mwaka wa 1923, alihamia Latvia na kuolewa na Percy Dunham. Wakati huo upinzani ulizidi kuongezeka. Madge anaandika hivi: “Mnamo Februari 9, 1933, gazeti fulani la Riga lilidai sisi ni Wakomunisti. Asubuhi iliyofuata, mlango ulibishwa nami nikaufungua. Polisi waliingia kwa fujo huku wakiwa na bunduki zao na kuamuru kwa sauti, ‘Mikono juu!’ Kwa saa saba, walitafuta vitabu vilivyopigwa marufuku. Wakati wa mchana, niliwapa chai, nao wakanywa.
“Akiba kuu ya vichapo vya akina ndugu ilikuwa imefichwa darini. Mapema, ofisa-msimamizi alipopekua mifuko ya nguo ya mume wangu, alipata funguo. Akauliza, ‘Ni za wapi?’ Percy akamjibu, ‘Ni za chumba cha dari.’ Lakini polisi hawakupanda kwenye chumba hicho. Ajabu ni kwamba kabla ya kuondoka, ofisa huyo alimrudishia Percy funguo! Ingawa walikagua vichapo fulani, walisema hawakuona haja ya kuvichukua.
“Hata hivyo, walivichukua pamoja na barua, pesa, mashini ya kuchapisha na taipureta. Polisi walifanya misako mingine katika nyumba za familia sita za Mashahidi Walatvia lakini hawakupata uthibitisho wowote wa uvunjaji wa sheria wala hawakuwashtaki.”
-
-
Latvia2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Mnamo Oktoba 27, akina Dunham walilazimika kuondoka Latvia na kuwaacha ndugu na dada zao wapendwa. Walitumwa kwenye ofisi ya tawi ya Australia, ambako Percy alikufa mwaka wa 1951, na Madge akafa mwaka wa 1998, wote wakiwa na tumaini la kwenda mbinguni.
-