-
Tumaini Hakika kwa WafuMtu Fulani Umpendaye Anapokufa
-
-
[Blabu katika ukurasa wa 27]
Hisia nyororo za Yesu alipokuwa akimfufua Lazaro zilionyesha kutamani kwake sana kuondoa madhara ya kifo
-
-
Tumaini Hakika kwa WafuMtu Fulani Umpendaye Anapokufa
-
-
“Lazaro, Njoo Huku Nje!”
Hicho kilikuwa kisa chenye kugusa moyo. Lazaro alikuwa mgonjwa sana. Dada zake wawili, Maria na Martha, walimpelekea neno Yesu, aliyekuwa ng’ambo ya Mto Yordani: “Bwana, ona! yule ambaye una shauku naye ni mgonjwa.” (Yohana 11:3, NW) Walijua kwamba Yesu alimpenda Lazaro. Je! Yesu asingetaka kumwona rafiki yake mgonjwa? Ajabu, badala ya kwenda Bethania mara moja, Yesu alikaa alikokuwa kwa siku mbili zilizofuata.—Yohana 11:5, 6.
Lazaro alikufa muda fulani baada ya kupelekwa kwa ule ujumbe kuhusu ugonjwa wake. Yesu alijua wakati ambapo Lazaro alikufa, naye alikusudia kufanya jambo fulani kuhusu hilo. Kufikia wakati Yesu alipowasili Bethania hatimaye, rafiki yake mpendwa alikuwa amekufa zimepita siku nne. (Yohana 11:17, 39) Je! Yesu angeweza kurudisha kwenye uhai mtu aliyekuwa amekufa muda mrefu hivyo?
Aliposikia kwamba Yesu alikuwa akija, Martha, mwanamke mwenye matendo, alikimbia nje kwenda kumlaki. (Linganisha Luka 10:38-42.) Akiwa ameguswa na huzuni ya Martha, Yesu alimtia moyo hivi: “Ndugu yako atainuka.” Alipoonyesha imani yake katika ufufuo wa wakati ujao, Yesu alimwambia hivi waziwazi: “Mimi ndio ufufuo na uhai. Yeye ambaye hudhihirisha imani katika mimi, hata ingawa afa, atakuja kwenye uhai.”—Yohana 11:20-25, NW.
Alipowasili kwenye kaburi, Yesu alielekeza kwamba jiwe lililokuwa likifunga mwingilio walo liondolewe mbali. Kisha, baada ya kusali kwa sauti kubwa, aliamuru hivi: “Lazaro, njoo huku nje!”—Yohana 11:38-43, NW.
Macho yote yalikaziwa kaburi hilo. Kisha, umbo la mtu likatoka katika giza hilo. Miguu na mikono yake ilikuwa imefungwa vitambaa, na uso wake ulikuwa umefungwa kwa nguo. “Mfungueni na acheni aende,” akaamuru Yesu. Vitambaa vya mwisho vilivyofunguliwa vikaanguka chini. Ndiyo, huyo alikuwa ndiye Lazaro, yule mtu aliyekuwa amekufa muda wa siku nne!—Yohana 11:44, NW.
Je! Kweli Hilo Lilitukia?
Simulizi la kuinuliwa kwa Lazaro linatokezwa katika Gospeli ya Yohana likiwa jambo la hakika la kihistoria. Maelezo madogomadogo ni dhahiri mno kuweza kuwa mfano tu. Kushuku kwamba tukio hilo halikuwa jambo la kihistoria ni kutilia shaka miujiza yote ya Biblia kutia na ufufuo wa Yesu Kristo mwenyewe. Na kukana ufufuo wa Yesu ni kukana imani ya Kikristo kwa ujumla.—1 Wakorintho 15:13-15.
Kwa kweli, ikiwa wakubali kuwako kwa Mungu, hupaswi uwe na tatizo la kuamini katika ufufuo. Kutoa kielezi: Mtu aweza kurekodi wasia wake katika vidio, na baada ya yeye kufa, watu wa ukoo na marafiki zake waweza kwa kweli kumwona na kumsikia, aelezapo njia mali zake zipasavyo kushughulikiwa. Miaka mia moja iliyopita, jambo hilo lilikuwa lisilofikirika. Na kwa watu wengine wanaoishi sasa katika sehemu za mbali za ulimwengu, ufundi wa kurekodi mambo kwenye vidio ni jambo lisiloeleweka hata kidogo hivi kwamba laonekana kuwa la kimuujiza. Ikiwa kanuni za kisayansi zilizoanzishwa na Muumba zaweza kutumiwa na wanadamu kuunda upya picha iwezayo kuonwa na kusikiwa, je, Muumba asiweze kufanya zaidi ya hivyo? Basi je, si jambo la akili kusema kwamba Yeye aliyeumba uhai ana uwezo wa kuuumba upya?
Muujiza wa kurudishwa kwa Lazaro kwenye uhai ulitumika kuongeza imani katika Yesu na ufufuo. (Yohana 11:41, 42; 12:9-11, 17-19) Kwa njia yenye kugusa moyo, huo hufunua pia utayari na tamaa ya Yehova na Mwana wake kufanya ufufuo.
‘Mungu Atakuwa na Tamaa Sana’
Itikio la Yesu kwa kifo cha Lazaro lafunua hisia nyororo sana za Mwana wa Mungu. Hisia zake zenye kina katika pindi hii zaonyesha waziwazi kutamani kwake sana kufufua wafu. Twasoma hivi: “Maria, alipowasili ambapo Yesu alikuwa naye alipomwona, alianguka penye miguu yake, akimwambia: ‘Bwana, kama ungalikuwa hapa, ndugu yangu asingalikufa.’ Kwa hiyo, Yesu alipomwona akitoa machozi na Wayahudi waliokuja pamoja naye wakitoa machozi, akapiga kite katika roho na kuwa mwenye kutaabika; naye akasema: ‘Mmemlaza wapi?’ Wakamwambia: ‘Bwana, njoo uone.’ Yesu akatokwa na machozi. Kwa hiyo Wayahudi wakaanza kusema: ‘Ona, jinsi alivyokuwa na shauku naye!’”—Yohana 11:32-36, NW.
Huruma ya Yesu ya kuhisiwa moyoni inaonyesha hapa na mafungu haya matatu ya maneno: “akapiga kite,” “kuwa mwenye kutaabika,” na “akatokwa na machozi.” Maneno ya lugha ya awali yaliyotumiwa katika kuandika kisa hiki chenye kugusa moyo yaonyesha kwamba Yesu aliathiriwa sana na kifo cha rafiki yake mpendwa Lazaro na kumwona dada ya Lazaro akitoa machozi hivi kwamba macho Yake yalifurika machozi.a
Jambo la kutazamisha sana ni kwamba hapo awali Yesu alikuwa amewarudisha watu wengine wawili kwenye uhai. Na alikusudia kabisa kufanya vivyo hivyo na Lazaro. (Yohana 11:11, 23, 25) Hata hivyo, “akatokwa na machozi.” Basi, kurudisha wanadamu kwenye uhai, si utaratibu fulani tu wa Yesu. Hisia zake nyororo na zenye kina kama zilivyodhihirishwa kwenye pindi hii zaonyesha kwa wazi kutamani kwake sana kuondoa madhara ya kifo.
-
-
Tumaini Hakika kwa WafuMtu Fulani Umpendaye Anapokufa
-
-
a Neno la Kigiriki linalofasiriwa “akapiga kite” linatoka kwenye kitenzi (em·bri·maʹo·mai) kimaanishacho kuathiriwa sana, au kwa njia ya kuumiza. Msomi mmoja wa Biblia aonyesha hivi: “Hapa laweza kumaanisha tu kwamba Yesu alishikwa kwa nguvu na hisiamoyo yenye kina sana hivi kwamba kupiga kite kulitokezwa moyoni Mwake kwa lazima.” Usemi unaotafsiriwa “kuwa mwenye kutaabika” watokana na neno la Kigiriki (ta·rasʹso) lionyeshalo kufadhaika. Kulingana na mtunga-kamusi fulani, linamaanisha “kumsababishia mtu msukosuko wa kindani, . . . kuathiri kwa umivu au huzuni kubwa.” Usemi huu “akatokwa na machozi” watokana na kitenzi cha Kigiriki (da·kryʹo) kimaanishacho “kudondoa machozi, kutoa machozi kimyakimya.”
-