-
Je, Unathamini Uhai Kama Vile Mungu Anavyouthamini?“Jitunzeni Katika Upendo wa Mungu”
-
-
16. Ni kanuni gani ya Biblia inayohusu kutoa mimba? (Ona pia maelezo ya chini.)
16 Hata uhai wa mtoto ambaye hajazaliwa una thamani machoni pa Mungu. Katika Israeli la kale, ikiwa mtu angemjeruhi mwanamke mjamzito na mwanamke huyo au mtoto wake afe, Mungu alimwona mtu huyo kuwa muuaji, na alipaswa kulipa “nafsi kwa nafsi.”c (Kutoka 21:22, 23) Wazia basi jinsi Yehova anavyojisikia anapoona watoto wengi sana ambao hawajazaliwa wakiuawa kila mwaka, na wengi wao wanauawa kwa sababu ya ubinafsi na maadili mapotovu.
17. Unaweza kumtia moyo jinsi gani mtu aliyetoa mimba kabla ya kujifunza kanuni za Mungu?
17 Namna gani ikiwa mwanamke alitoa mimba kabla ya kujifunza kweli za Biblia? Je, inamaanisha kwamba Mungu hawezi kumwonyesha rehema? Sivyo hata kidogo! Mtu akitubu kikweli, anaweza kupata msamaha wa Yehova kwa msingi wa damu ya Yesu iliyomwagwa. (Zaburi 103:8-14; Waefeso 1:7) Kwa kweli, Kristo mwenyewe alisema: “Nimekuja kuwaita, si watu waadilifu, bali watenda-dhambi watubu.”—Luka 5:32.
-
-
Je, Unathamini Uhai Kama Vile Mungu Anavyouthamini?“Jitunzeni Katika Upendo wa Mungu”
-
-
c Wachanganuzi wa Biblia wanasema “haiwezekani kwamba” maandishi ya Kiebrania katika andiko hilo “yanarejelea madhara yanayompata mwanamke peke yake.” Pia, ona kwamba kulingana na Biblia, hukumu ya Yehova haikutegemea umri wa kiini-tete au kijusi.
-