-
Kutumikia kwa Uaminifu-Mshikamanifu Pamoja na Tengenezo la YehovaMnara wa Mlinzi—1997 | Agosti 1
-
-
Kukazia Fikira Kutokamilika Kwaweza Kumomonyoa Uaminifu-Mshikamanifu
4. (a) Kwa nini ni rahisi kuwachambua walio na mamlaka? (b) Kora alithibitikaje kuwa asiye na uaminifu-mshikamanifu kwa tengenezo la Yehova?
4 Ndugu akiwa katika wadhifa wenye madaraka, makosa yake yaweza kuonekana wazi zaidi. Jinsi ilivyo rahisi kuchambua ‘unyasi ulio katika jicho la ndugu yetu huku tukilipuuza boriti lililo katika jicho letu wenyewe’! (Mathayo 7:1-5) Hata hivyo, kufikiria sana makosa kwaweza kukuza ukosefu wa uaminifu-mshikamanifu. Kwa kutoa kielezi, fikiria tofauti kati ya Kora na Daudi. Kora alikuwa na madaraka mengi, na labda alikuwa amekuwa mwaminifu kwa miaka mingi, lakini akatamani makuu. Alikuja kuonea uchungu mamlaka ya Musa na Aroni, binamu zake. Ingawa Musa alikuwa msikivu zaidi kati ya watu, kwa wazi Kora alianza kumtazama kwa macho ya kutafuta makosa. Yamkini aliona makosa ya Musa. Hata hivyo, makosa hayo, hayakufanya ukosefu wa uaminifu-mshikamanifu wa Kora kwa tengenezo la Yehova ustahili. Aliharibiwa kutoka miongoni mwa kutaniko hilo.—Hesabu 12:3; 16:11, 31-33.
5. Kwa nini huenda ikawa Daudi alihisi kushawishiwa kumwasi Sauli?
5 Kwa upande mwingine, Daudi alitumikia chini ya Mfalme Sauli. Sauli ambaye wakati mmoja alikuwa mfalme mzuri, kwa kweli alikuja kuwa mwovu. Daudi alihitaji imani, uvumilivu, na hata werevu ili kusalimika mashambulizi ya Sauli mwenye wivu. Hata hivyo, Daudi alipokuwa na fursa ya kulipiza kisasi, alisema kwamba hilo lilikuwa ‘lisilowazika, kwa maoni ya Yehova,’ kwamba atende tendo la ukosefu wa uaminifu-mshikamanifu dhidi ya mtu ambaye Yehova alikuwa amemtia mafuta.—1 Samweli 26:11, NW.
6. Hatupaswi kamwe kufanya nini, hata tukiona udhaifu na makosa katika wazee?
6 Baadhi ya wanaoongoza miongoni mwetu waonekanapo kukosea katika hukumu, wasemapo kwa maneno makali, au waonekanapo kuonyesha upendeleo, je, tutalalamika dhidi yao, labda tukichangia roho ya uchambuzi kutanikoni? Je, tutakosa kuhudhuria mikutano ya Kikristo ikiwa njia moja ya kuteta dhidi yao? Kwa hakika la! Sawa na Daudi, hatutaruhusu kamwe makosa ya mwingine yatufanye tukose uaminifu-mshikamanifu kwa Yehova na kwa tengenezo lake!—Zaburi 119:165.
7. Ni yapi baadhi ya mazoea yenye ufisadi yaliyodhihirika kuhusiana na hekalu katika Yerusalemu, na Yesu alihisije juu ya hilo?
7 Kielelezo kikuu zaidi cha kibinadamu cha uaminifu-mshikamanifu kilikuwa Yesu Kristo, anayefafanuliwa kiunabii kuwa “mwenye uaminifu-mshikamanifu” wa Yehova. (Zaburi 16:10, NW) Kulitumia hekalu la Yerusalemu kwa ufisadi lazima kuwe kulifanya uaminifu-mshikamanifu uwe jambo gumu. Yesu alijua kwamba kazi ya kuhani mkuu na zile dhabihu zilifananisha kimbele huduma yake mwenyewe na kifo chake cha kidhabihu, naye alijua jinsi lilivyokuwa jambo la maana watu wajifunze kutokana na hayo. Kwa hiyo alijawa na ghadhabu ya uadilifu alipoona kwamba hekalu lilikuwa limekuwa “pango la wapokonyaji.” Akiwa na mamlaka yenye kupewa na Mungu, alichukua hatua ya kulisafisha mara mbili.a—Mathayo 21:12, 13; Yohana 2:15-17.
8. (a) Yesu alionyeshaje uaminifu-mshikamanifu kwa mpango wa hekalu? (b) Twaweza kuonyeshaje kwamba twathamini kumwabudu Yehova pamoja na tengenezo lake safi?
8 Hata hivyo, Yesu alitegemeza mpango huo wa hekalu kwa uaminifu-mshikamanifu. Tangu utotoni, alihudhuria zile sikukuu kwenye hilo hekalu na alifundisha humo mara nyingi. Hata alilipa kodi ya hekalu—ingawa kwa kweli hakuwa na wajibu wa kufanya hivyo. (Mathayo 17:24-27) Yesu alimpongeza yule mjane maskini kwa kutumbukiza “riziki yake yote” kwenye sanduku la hazina ya hekalu. Punde baada ya hapo, Yehova alilikataa kabisa hekalu hilo. Lakini hadi wakati huo, Yesu alikuwa mwenye uaminifu-mshikamanifu kwalo. (Marko 12:41-44; Mathayo 23:38) Leo tengenezo la Mungu la kidunia ni bora zaidi kuliko mfumo wa Kiyahudi pamoja na hekalu la mfumo huo. Yakubalika kwamba tengenezo hilo si kamilifu; ndiyo sababu marekebisho hufanywa nyakati nyingine. Lakini halina ufisadi, wala Yehova Mungu haelekei kuweka jingine mahali pa hilo. Tusiruhusu kamwe kutokamilika kokote tunakoona ndani yake kutukasirishe au kutusukume kuwa na mtazamo wenye kuchambua na wa kulalamika. Badala ya hivyo, acheni tuige uaminifu-mshikamanifu wa Yesu Kristo.—1 Petro 2:21.
-
-
Kutumikia kwa Uaminifu-Mshikamanifu Pamoja na Tengenezo la YehovaMnara wa Mlinzi—1997 | Agosti 1
-
-
15. Watu fulani katika karne ya kwanza walionyeshaje kwamba walikuwa na uaminifu-mshikamanifu mbalimbali usiofaa?
15 Njia nyingine yenye hila ya ukosefu wa uaminifu-mshikamanifu ni uaminifu-mshikamanifu usiostahili. Uaminifu-mshikamanifu wa kweli katika maana ya Kibiblia hauturuhusu kuweka uaminifu wetu wa kiraia mbele ya uaminifu-mshikamanifu kwa Yehova Mungu. Wayahudi wengi katika karne ya kwanza walishikamana kwa ushupavu na Sheria ya Kimusa na mfumo wa mambo wa Kiyahudi. Hata hivyo, wakati wa Yehova ulikuwa umefika ili aondoe baraka zake kutoka katika taifa hilo lenye kuasi na kuzielekeza kwa taifa la Israeli la kiroho. Kwa kulinganishwa ni wachache tu waliokuwa wenye uaminifu-mshikamanifu kwa Yehova na ambao walikubali badiliko hilo lenye maana sana. Hata miongoni mwa Wakristo wa kweli, baadhi ya wale Wageuzao watu wafuate dini ya Kiyahudi walisisitiza kuyarudia yale “mambo ya msingi yaliyo dhaifu na yasiyo na maana” ya Sheria ya Musa, ambayo ilikuwa imetimizwa katika Kristo.—Wagalatia 4:9; 5:6-12; Wafilipi 3:2, 3.
16. Watumishi wa Yehova wenye uaminifu-mshikamanifu huitikiaje marekebisho?
16 Kwa kutofautisha, watu wa Yehova katika nyakati za kisasa wamejithibitisha kuwa wenye uaminifu-mshikamanifu katika nyakati zenye mabadiliko. Nuru ya kweli iliyofunuliwa iendeleapo kung’aa, marekebisho yanafanywa. (Mithali 4:18) Majuzi, “mtumwa mwaminifu na mwenye busara” ametusaidia kurekebisha uelewevu wetu juu ya neno “kizazi” linalotumiwa kwenye Mathayo 24:34 na juu ya wakati wa kuhukumiwa kwa “kondoo” na “mbuzi” wanaotajwa kwenye Mathayo 25:31-46, na pia juu ya maoni yetu kuelekea utumishi wa kiraia wa aina fulani-fulani. (Mathayo 24:45) Bila shaka waasi-imani fulani wangependezwa ikiwa Mashahidi wa Yehova wengi wangeshikilia sana uelewevu uliotangulia wa habari hizo na kukataa kufanya maendeleo. Hakujawa na itikio lolote la aina hiyo. Kwa nini? Watu wa Yehova ni wenye uaminifu-mshikamanifu.
-
-
Kutumikia kwa Uaminifu-Mshikamanifu Pamoja na Tengenezo la YehovaMnara wa Mlinzi—1997 | Agosti 1
-
-
Kutumikia kwa Uaminifu-Mshikamanifu Katika Betheli
“Acheni mambo yote yatukie kwa adabu na kwa mpango.” Ndivyo alivyoandika mtume Paulo. (1 Wakorintho 14:40) Paulo alijua kwamba ili kutaniko litende, kungekuwa na uhitaji wa “mpango,” wa utaratibu. Hali kadhalika leo, lazima wazee wafanye maamuzi juu ya mambo yenye kutumika, kama vile kuwapa washiriki wa kutaniko migawo ya kwenda kwenye mafunzo ya kitabu mahali mbalimbali, kupanga mikutano kwa ajili ya utumishi wa shambani, na kuchunguza kuhubiriwa kwa maeneo. Nyakati nyingine huenda mipango hiyo ikatokeza mitihani ya uaminifu-mshikamanifu. Mipango hiyo si amri zenye kupuliziwa kimungu, nayo haiwezi kupata kibali cha kila mtu mmoja-mmoja.
Je, nyakati nyingine, waona ugumu wa kuwa mwenye uaminifu-mshikamanifu kwa baadhi ya mipango yenye kutumika inayofanywa katika kutaniko la Kikristo? Ikiwa ndivyo, huenda ukaona kielelezo cha Betheli kuwa chenye kusaidia. Zile ofisi zote za tawi 104 za Watch Tower Society kutia na makao makuu ya Marekani,* zinaitwa Betheli, neno la Kiebrania linalomaanisha “Nyumba ya Mungu.” Wajitoleaji wanaoishi na kufanya kazi kwenye majengo ya Betheli wanataka mahali hapo padhihirishe staha na kicho kwa Yehova. Hilo hutaka kila mmoja awe mwenye uaminifu-mshikamanifu.
Mara nyingi, wenye kuzuru Betheli husema juu ya utaratibu na usafi waonao huko. Wafanyakazi ni wenye utaratibu na wenye furaha; usemi wao na adabu zao na hata kuonekana kwao kwadhihirisha dhamiri komavu za Kikristo, ambazo zimezoezwa na Biblia. Washiriki wote wa familia ya Betheli hushikamana kwa uaminifu-mshikamanifu na viwango vya Neno la Mungu.
Kwa kuongezea, Baraza Linaloongoza huwaandalia kijitabu cha maagizo kiitwacho Dwelling Together in Unity, ambacho hutaja kwa fadhili mipango fulani yenye kutumika inayohitajiwa kwa ajili ya familia kubwa kama hiyo ili wafanye kazi vizuri pamoja. (Zaburi 133:1) Mathalani, kinashughulikia vyumba, milo, usafi wa kiafya, mavazi na mapambo, na mambo kama hayo. Washiriki wa familia ya Betheli hutegemeza na kushikamana na mipango hiyo kwa uaminifu-mshikamanifu, hata wakati ambapo labda mapendezi ya kibinafsi yatawaongoza kuelekea upande mwingine. Wanakiona kijitabu hicho cha maagizo kuwa miongozo yenye mafaa inayokusudiwa kuendeleza muungano na upatano, wala si sheria na kanuni ngumu. Waangalizi ni wenye uaminifu-mshikamanifu katika kutegemeza utaratibu huo mbalimbali wenye msingi katika Biblia, nao huutumia katika njia chanya ili kujenga na kutia moyo washiriki wa familia ya Betheli kufuatia utumishi wao mtakatifu wa Betheli.
-