-
Kuhuburi na Kufundisha Ulimwenguni Pote2008 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Madagaska
Mwaka uliopita katika kijiji chenye wakaaji 500, kasisi mmoja alipewa kitabu Biblia Inafundisha na Shahidi mmoja katika kijiji kingine. Baada ya kukisoma kwa uangalifu, kasisi huyo alisadiki kwamba alikuwa amepata kweli, na aliwaambia washiriki wa kanisa lake mambo aliyokuwa amejifunza. Muda si muda, yeye pamoja na familia yake na watu wengine 20 walijitenga na kanisa hilo na wakaanza kufanya mikutano, kama Mashahidi wa Yehova wanavyofanya kila mahali. Mapainia wa pekee walikuja kuwasaidia. Walijifunza Biblia na watu wengi waliopendezwa na wakapanga mikutano ya Funzo la Kitabu la Kutaniko na Mnara wa Mlinzi ifanywe kwa kawaida. Mnamo Oktoba, watu watano wakawa wahubiri ambao hawajabatizwa, na sasa mapainia hao wamefanya mipango ili kuwe na Mkutano wa Watu Wote na Shule ya Huduma ya Kitheokrasi. Wastani wa watu 40 hivi wanahudhuria mikutano, na mafunzo ya Biblia zaidi ya 20 yanaongozwa.
-
-
Kuhuburi na Kufundisha Ulimwenguni Pote2008 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha katika ukurasa wa 44]
Funzo la “Mnara wa Mlinzi” katika kijiji cha Antanandava, Madagaska
-