-
Vijana—Fanyeni Maendeleo Yenu Yawe WaziMnara wa Mlinzi—2009 | Mei 15
-
-
Kujitayarisha kwa Ajili ya Ndoa Yenye Mafanikio
12. Kwa nini Mkristo anayefikiria kufunga ndoa anapaswa kutumia kanuni iliyo katika Methali 20:25?
12 Vijana fulani wamekimbilia kufunga ndoa, wakifikiri kwamba ndoa ndiyo suluhisho la kupata furaha, kuepuka upweke, matatizo nyumbani, na maisha yenye kuchosha. Hata hivyo, kuweka nadhiri za ndoa ni jambo zito. Watu fulani katika nyakati za Biblia walikimbilia kuweka nadhiri takatifu bila kuchunguza kwa uangalifu mambo yaliyohusika. (Soma Methali 20:25.) Nyakati nyingine, vijana hawafikirii kwa uzito kuhusu madaraka ya ndoa. Baadaye, wanagundua kwamba hawakujua kuwa ndoa inahusisha mambo mengi zaidi.
13. Wale wanaofikiria kuanzisha uchumba wanapaswa kufikiria maswali gani, na wamepewa mashauri gani yenye faida?
13 Kwa hiyo, kabla ya kuanza uchumba, jiulize hivi: ‘Kwa nini ninataka kufunga ndoa? Ninatazamia nini? Je, huyu ni mwenzi anayenifaa? Je, niko tayari kutimiza madaraka yangu katika ndoa?’ Ili kukusaidia ujichunguze kwa busara, “mtumwa mwaminifu na mwenye busara” amechapisha habari hususa kuhusu ndoa.b (Mt. 24:45-47) Ona habari hizo kuwa mashauri ambayo Yehova anakupa. Chunguza kwa uangalifu mambo hayo na uyatumie. Usijiruhusu kamwe uwe “kama farasi au nyumbu wasio na uelewaji.” (Zab. 32:8, 9) Uwe mkomavu katika uelewaji wako kuhusu madaraka ya ndoa. Ikiwa unahisi kwamba uko tayari kuanzisha uchumba, kumbuka sikuzote kwamba unapaswa kuwa “kielelezo . . . katika usafi wa kiadili.”—1 Tim. 4:12.
14. Maendeleo ya kiroho yatakusaidia jinsi gani ukifunga ndoa?
14 Ukomavu wa kiroho unamsaidia mtu kufanikiwa pia baada ya kufunga ndoa. Mkristo mkomavu anajitahidi sana kufikia “kipimo cha kimo ambacho ni cha ujazo wa Kristo.” (Efe. 4:11-14) Anafanya bidii kusitawisha utu kama wa Kristo. Akiwa Kielelezo chetu, “Kristo hakujipendeza mwenyewe.” (Rom. 15:3) Mume au mke akiendelea kutafuta, si faida yake mwenyewe tu, bali faida ya mwenzi wake, maisha ya familia yatakuwa yenye amani na yenye kuburudisha. (1 Kor. 10:24) Mume ataonyesha upendo wa kujidhabihu, na mke ataazimia kujitiisha kwa mume wake kama Yesu anavyojitiisha kwa Kichwa chake.—1 Kor. 11:3; Efe. 5:25.
-
-
Vijana—Fanyeni Maendeleo Yenu Yawe WaziMnara wa Mlinzi—2009 | Mei 15
-
-
b “Je, Ananifaa?” katika kitabu Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 2; “Mwongozo wa Mungu Katika Kuchagua Mwenzi wa Ndoa,” katika gazeti la Mnara wa Mlinzi la Mei 15, 2001 (15/5/2001); na “Je, Ni Hekima kwa Matineja Kufunga Ndoa?” katika gazeti la Amkeni! la Septemba 22, 1983 (22/9/1983), la Kiingereza au gazeti la Kifaransa la Desemba 22, 1983 (22/12/1983).
-