-
Kuhuburi na Kufundisha Ulimwenguni Pote2008 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Visiwa vya Solomon
Painia wa kawaida anayeitwa Emily ndiye Shahidi pekee katika eneo la kisiwa cha San Cristobal. Anaongoza mafunzo ya Biblia 20, na watatu kati yao wamekuwa wahubiri ambao hawajabatizwa kutia ndani wazazi wake. Lance na Diane, ambao ni watumishi wa kimataifa walichukua likizo na wakasafiri kwa muda wa saa 14 kwenye meli iliyosongamana ili kwenda kumsaidia Emily wakati wa Ukumbusho. Lance anasema: “Tulipofika, tulitaka tu kulala, lakini tukaona ni vizuri tumtembelee chifu wa kijiji hicho kwanza. Baada ya kumweleza kusudi la kutembelea eneo hilo, chifu huyo aliuliza: ‘Watu wengi hawajapata mwaliko wa Ukumbusho. Je, wao pia wanaweza kuhudhuria?’ Tukiwa na tabasamu changamfu, tulimwambia kwamba kila mtu amekaribishwa.
“Wakati wa kuanza Ukumbusho ulipokaribia, ni wanawake wawili tu na watoto kadhaa waliokuwa wameketi. Hata hivyo, tuliona watu wengi wakiwa karibu na miti, kwa hiyo tuliwakaribisha. Giza lilipoingia, tuliwasha taa kwa kutumia jenereta. Hotuba ya Ukumbusho iliendelea na kila mtu alisikiliza kwa makini.” Watu 130 hivi walisikiliza hotuba hiyo, kutia ndani mhudumu wa kanisa la Seventh Day Adventist ambaye alitaka Biblia Tafsiri ya Ulimwengu Mpya kwa sababu ilieleweka kwa urahisi kuliko Biblia aliyotumia. Katika tukio hilo la pekee, mafunzo ya Biblia matano yalianzishwa.
-
-
Kuhuburi na Kufundisha Ulimwenguni Pote2008 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha katika ukurasa wa 64]
Lance, Diane, na Emily
-