-
Yehova Amkweza Mtumishi Wake wa KimesiyaUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
“Mtumishi Wangu”—Yeye Ni Nani?
4. Baadhi ya wasomi Wayahudi wametoa maoni gani kuhusu utambulisho wa “mtumishi,” lakini kwa nini maoni hayo hayapatani na unabii wa Isaya?
4 Muda mfupi uliopita Isaya amekuwa akisimulia habari za kufunguliwa kwa Wayahudi kutoka uhamishoni Babiloni. Sasa anatazama mbele kwenye tukio kubwa hata zaidi anapoandika maneno ya Yehova: “Tazama, mtumishi wangu atatenda kwa busara [“ufahamu wenye kina,” “NW”], atatukuzwa, na kuinuliwa juu, naye atakuwa juu [“atakwezwa,” “NW”] sana.” (Isaya 52:13) “Mtumishi” huyu ni nani hasa? Muda wa karne zilizopita, wasomi Wayahudi walitoa maoni mbalimbali. Wengine wao walidai kwamba aliwakilisha taifa zima la Israeli likiwa uhamishoni Babiloni. Lakini maelezo hayo hayapatani na unabii wenyewe. Mtumishi wa Mungu anateseka kwa hiari yake. Ingawa hana hatia, anateseka kwa ajili ya dhambi za wengine. Hakika maelezo hayo hayapatani na hali ya taifa la Kiyahudi, lililoingia uhamishoni kwa sababu ya njia zake zenye dhambi. (2 Wafalme 21:11-15; Yeremia 25:8-11) Wengine walidai kwamba Mtumishi huyo aliwakilisha watu wa vyeo vya juu ambao walijiona kuwa wenye haki katika Israeli, na kwamba watu hao walipatwa na mateso kwa ajili ya Waisraeli wenye dhambi. Hata hivyo, nyakati za kuteseka katika Israeli, hakuna kikundi fulani cha watu hususa kilichotaabika kwa ajili ya kingine.
5. (a) Wasomi fulani Wayahudi wameonyesha matumizi gani kuhusu unabii wa Isaya? (Ona kielezi-chini.) (b) Yule Mtumishi anatambulishwa wazi kuwa nani katika kitabu cha Biblia cha Matendo?
5 Kabla ya kufika kwa Ukristo, na kwa kadiri fulani wakati wa zile karne za mapema za Wakati wa Kawaida, wasomi wachache Wayahudi walitumia unabii huu kumhusu Mesiya. Usahihi wa kutumia unabii huo kwa njia hiyo unaonekana katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo. Kitabu cha Matendo kinaripoti kwamba yule towashi Mwethiopia aliposema kuwa hajui ni nani anayetambuliwa kuwa Mtumishi wa unabii wa Isaya, Filipo ‘alimtangazia habari njema juu ya Yesu.’ (Matendo 8:26-40; Isaya 53:7, 8) Vivyo hivyo, vitabu vingine vya Biblia humtambulisha Yesu Kristo kuwa ndiye Mtumishi wa Kimesiya wa unabii wa Isaya.a Tunapozungumzia unabii huu, tutaona ulinganifu mbalimbali usioweza kukanushwa uliopo kati ya yule ambaye Yehova anamwita “mtumishi wangu” na Yesu wa Nazareti.
-
-
Yehova Amkweza Mtumishi Wake wa KimesiyaUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
a Targumi ya Jonathan ben Uzziel (karne ya kwanza W.K.), iliyotafsiriwa na J. F. Stenning, inasema hivi inapofasiri Isaya 52:13: “Tazama, mtumishi wangu, Yule Mtiwa-Mafuta (au, yule Mesiya), atapata ufanisi.” Hivyo hivyo, Talmudi ya Kibabiloni (karibu karne ya tatu W.K.) inasema hivi: “Yule Mesiya—jina lake nani? . . . [; wale] wa nyumba ya Rabi [husema, Yule mgonjwa], kwa kuwa inasemwa, ‘Hakika yeye amebeba magonjwa yetu.’”—Sanhedrin 98b; Isaya 53:4.
-