-
Ibada ya Kweli Yapanuka Ulimwenguni PoteUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Hata hivyo, mamilioni ya watu wamevutiwa na nuru ya Yehova. Watu hao ni kutia ndani “wafalme” (wale ambao wamekuwa warithi watiwa-mafuta wa Ufalme wa kimbingu) na “mataifa” (ule umati mkubwa wa kondoo wengine).
-
-
Ibada ya Kweli Yapanuka Ulimwenguni PoteUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
b Ingawa Wakristo fulani wenye bidii na wenye tumaini la kidunia walishirikiana na Israeli wa Mungu kabla ya mwaka wa 1930, idadi yao ilianza kuongezeka sana katika miaka ya 1930.
-
-
Ibada ya Kweli Yapanuka Ulimwenguni PoteUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Mataifa Yatoka Pande Zote Kuja Kukutanikia Yerusalemu
9, 10. Ni nani wanaoonekana wakitoka pande mbalimbali kuja kukutanikia Yerusalemu, na Yehova anawapokeaje?
9 Yehova anaeleza jinsi mpanuko utakavyofanyika, akitumia mifano inayofahamika na watu wa wakati wa Isaya. “Mwanamke” huyo anatazama akiwa pale alipo juu ya Mlima Sayuni na kuangaza-angaza macho yake kwenye upeo wa mashariki. Anaona nini? “Wingi wa ngamia utakufunika, ngamia vijana wa Midiani na Efa; wote watakuja kutoka Sheba; wataleta dhahabu na uvumba; na kuzitangaza sifa za BWANA.” (Isaya 60:6) Misafara ya ngamia inayotumiwa na wafanya-biashara wa makabila mbalimbali inashika njia kwenda Yerusalemu ikipita katika barabara zinazoelekea huko. (Mwanzo 37:25, 28; Waamuzi 6:1, 5; 1 Wafalme 10:1, 2) Ngamia wako kila mahali, kama mafuriko yanayoifunika nchi! Misafara hiyo inaleta zawadi za thamani kubwa, kuonyesha kwamba wafanya-biashara hao wanakuja wakiwa na makusudio ya amani. Wanataka kumwabudu Yehova na kumpa kilicho bora.
10 Si wafanya-biashara hawa tu walio mwendoni. “Makundi yote ya Kedari yatakusanyika kwako, kondoo waume wa Nebayothi watakutumikia.” Ndiyo, hata makabila yaliyo na desturi ya kuchunga mifugo yanasafiri kwenda Yerusalemu. Yanakuja na zawadi za mali zao zenye thamani kubwa zaidi, yaani makundi ya kondoo, kisha wanajitoa wawe wahudumu. Yehova atawapokeaje? Yeye anasema: “Watapanda juu ya madhabahu yangu kwa kibali, nami nitaitukuza nyumba ya utukufu wangu.” (Isaya 60:7) Yehova anazikubali zawadi zao, nazo zitatumiwa katika ibada safi.—Isaya 56:7; Yeremia 49:28, 29.
11, 12. (a) Yule “mwanamke” anaona nini anapokaza macho magharibi? (b) Kwa nini watu wengi sana wanafanya haraka kwenda Yerusalemu?
11 Sasa Yehova anamwagiza yule “mwanamke” atazame kwenye upeo wa magharibi. Halafu Yehova anauliza: “Ni nani hawa warukao kama wingu, na kama njiwa waendao madirishani kwao?” Yehova mwenyewe anajibu hivi: “Hakika yake visiwa vitaningojea, na merikebu za Tarshishi kwanza, ili kuleta wana wako kutoka mbali, na fedha yao na dhahabu yao pamoja nao, kwa ajili ya jina la BWANA, Mungu wako, kwa ajili yake Mtakatifu wa Israeli, kwa kuwa amekutukuza wewe.”—Isaya 60:8, 9.
12 Wazia kwamba umesimama pamoja na “mwanamke” huyo, ukikaza macho magharibi ng’ambo ya Bahari Kuu. Unaona nini? Wingu la mbali la madoa meupe yakielea juu ya maji. Wanaonekana kama ndege. Lakini wanapokaribia zaidi, unaona kwamba kumbe ni merikebu zenye matanga yaliyotwekwa. ‘Zimekuja kutoka mbali.’a (Isaya 49:12) Mashua zinazoenda kasi kuelekea Sayuni ni nyingi sana hivi kwamba zinaonekana kama kundi la njiwa wanaoelekea nyumbani. Haraka yote hiyo ya nini? Kikosi hicho kina hamu nyingi ya kuwafikisha pwani waabudu wa Yehova waliomo, ambao wametoka bandari za mbali. Kwa kweli, wote wale wanaowasili sasa hivi—Waisraeli na wageni pia, kutoka mashariki au magharibi na kutoka nchi za karibu au za mbali—wanafanya haraka kwenda Yerusalemu wakafanye vitu vyote walivyo navyo viwe wakfu kwa jina la Yehova, Mungu wao.—Isaya 55:5.
-
-
Ibada ya Kweli Yapanuka Ulimwenguni PoteUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Halafu wingu la watu watiifu, ambao ndio “utajiri wa mataifa” na “wingi wa bahari,” likafanya haraka kujiunga na ndugu za Kristo waliobaki.b Leo watumishi wote hawa wa Yehova wanaotoka pembe nne za dunia na kutoka hali zote za maisha wanajiunga na Israeli wa Mungu kumsifu Bwana wao Mwenye Enzi Kuu, Yehova, na kukweza jina lake kuwa ndilo tukufu zaidi katika ulimwengu mzima.
14. Wale wanaowasili sasa hivi ‘wanapandaje juu ya madhabahu ya Mungu’?
14 Ingawa hivyo, inamaanisha nini kwamba watu hawa wanaowasili sasa hivi kutoka kwenye mataifa “watapanda juu ya madhabahu [ya Mungu]”? Dhabihu huwekwa juu ya madhabahu. Mtume Paulo alitumia usemi unaohusisha dhabihu alipoandika hivi: “Nawasihi sana nyinyi . . . mtoe miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, yenye kukubalika kwa Mungu, utumishi mtakatifu pamoja na nguvu zenu za kufikiri kuzuri.” (Waroma 12:1) Wakristo wa kweli wana moyo wa kujitoa. (Luka 9:23, 24) Wanatoa wakati wao, nguvu zao, na stadi zao kuendeleza ibada safi. (Waroma 6:13) Kwa kufanya hivyo, wanatoa dhabihu zinazokubalika za kumsifu Mungu. (Waebrania 13:15) Jambo la kwamba mamilioni ya waabudu wa Yehova leo, vijana kwa wazee, wameweka tamaa zao za kibinafsi nyuma ya masilahi ya Ufalme wa Mungu, linachangamsha moyo kama nini! Wanaonyesha roho ya kweli ya kujidhabihu.—Mathayo 6:33; 2 Wakorintho 5:15.
Wale Wanaowasili Sasa Hivi Wanashiriki Katika Mpanuko
15. (a) Nyakati za kale, rehema ya Yehova ilionyeshwaje kuhusiana na wageni? (b) Nyakati za kisasa, “wageni” wameshiriki jinsi gani kuijenga ibada ya kweli?
15 Wale wanaowasili sasa hivi wanatoa mali zao na hata huduma zao binafsi kumtegemeza “mwanamke” wa Yehova. “Wageni watajenga kuta zako, na wafalme wao watakuhudumu; maana katika ghadhabu yangu nalikupiga, lakini katika upendeleo wangu nimekurehemu.” (Isaya 60:10) Rehema ya Yehova ilionyeshwa karne ya sita K.W.K. wakati wageni waliposaidia kazi ya ujenzi Yerusalemu. (Ezra 3:7; Nehemia 3:26) Katika utimizo mkubwa wa leo, “wageni,” yaani umati mkubwa, wanaunga mkono mabaki watiwa-mafuta kujenga ibada ya kweli. Wanasaidia kujenga sifa za Kikristo katika wanafunzi wao wa Biblia, na hivyo wanajenga makutaniko ya Kikristo na kuimarisha “kuta” za tengenezo la Yehova. (1 Wakorintho 3:10-15) Pia wanajenga kwa njia halisi, wakijibidiisha kujenga Majumba ya Ufalme, Majumba ya Kusanyiko, na majengo ya Betheli. Hivyo wanajiunga na ndugu zao watiwa-mafuta kutunza mahitaji ya tengenezo la Yehova linalopanuka.—Isaya 61:5.
16, 17. (a) “Malango” ya tengenezo la Mungu yamewekwaje wazi? (b) “Wafalme” wamemhudumiaje Sayuni? (c) Itakuwaje kwa wale wanaojaribu kuyafunga “malango” ambayo Yehova anataka yaachwe wazi?
16 Matokeo ya programu ya ujenzi wa kiroho ni kwamba, kila mwaka mamia ya maelfu ya “wageni” huanza kushirikiana na tengenezo la Yehova, na njia huwa wazi ili wengi hata zaidi waingie. Yehova anasema hivi: “Malango yako nayo yatakuwa wazi daima; hayatafungwa mchana wala usiku; ili watu wapate kukuletea utajiri wa mataifa, na wafalme wao wakiongozwa pamoja nao.” (Isaya 60:11) Ingawa hivyo, ni akina nani wale “wafalme” wanaoongoza kuuletea Sayuni utajiri wa mataifa? Nyakati za kale Yehova aligusa mioyo ya watawala fulani ili ‘kumhudumia’ Sayuni. Kwa mfano, Koreshi alichukua hatua ya kwanza ya kuwaagiza Wayahudi warudi Yerusalemu ili wakalijenge upya hekalu. Baadaye, Artashasta alichanga rasilmali na kumwagiza Nehemia ajenge upya kuta za Yerusalemu. (Ezra 1:2, 3; Nehemia 2:1-8) Kwa kweli “moyo wa mfalme huwa katika mkono wa BWANA; kama mifereji ya maji.” (Mithali 21:1) Mungu wetu anaweza kugusa mioyo ya hata watawala walio na nguvu zaidi watende kupatana na mapenzi yake.
17 Nyakati za kisasa “wafalme” au wenye mamlaka wengi wa kiserikali wamejaribu kufunga “malango” ya tengenezo la Yehova. Hata hivyo, wengine wametumikia Sayuni kwa kufanya maamuzi yaliyosaidia kuyaweka “malango” hayo yakiwa wazi. (Waroma 13:4) Mwaka wa 1919, wenye mamlaka wa kiserikali walimfungua Joseph F. Rutherford na waandamani wake kutoka gerezani walikokuwa wamefungwa bila haki. (Ufunuo 11:13) Serikali za kibinadamu ‘zilimeza kabisa’ mafuriko ya mnyanyaso yaliyomiminwa na Shetani kwa nguvu nyingi baada ya anguko lake kutoka mbinguni. (Ufunuo 12:16) Serikali fulani zimeunga mkono maoni ya kuvumiliana na imani za kidini za watu, nyakati nyingine zikiwatetea Mashahidi wa Yehova hasa. Huduma ya aina hiyo imefanya iwe rahisi zaidi makundi ya watu watiifu yakubali kupita katika yale “malango” yaliyo wazi na kuingia katika tengenezo la Yehova.
-