-
Yehova Hubariki Ibada SafiUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
15. Ni uzazi gani unaotabiriwa, na unatimizwaje mwaka wa 537 K.W.K.?
15 Hali hiyo ya kurudishwa inaonyeshwa kwa kufaa sana katika mistari ifuatayo ya Isaya: “Kabla hajaona utungu alizaa; kabla maumivu yake hayajampata, alizaa mtoto mwanamume. Ni nani aliyesikia neno kama hili? Ni nani aliyeona mambo kama haya? Je! nchi yaweza kuzaliwa siku moja? Taifa laweza kuzaliwa mara? Maana Sayuni, mara alipoona utungu, alizaa watoto wake.” (Isaya 66:7, 8)
-
-
Yehova Hubariki Ibada SafiUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
16. Katika utimizo wa kisasa wa Isaya 66:7, 8, Sayuni inafananisha nini, na wazao wake wamezaliwaje upya?
16 Katika utimizo wa kisasa, Sayuni inawakilisha “mwanamke” wa kimbingu wa Yehova, yaani tengenezo lake la kimbingu la viumbe-roho. Mwaka wa 1919 “mwanamke” huyu alishangilia kuona kuzaliwa kwa wana wake watiwa-mafuta duniani ili wawe watu waliopangwa kitengenezo, maana yake “taifa.” Tukio hilo la kuzaliwa upya lilifanyika upesi sana, tena kwa ghafula.c Katika muda wa miezi michache tu, watiwa-mafuta wakiwa kikundi walitoka katika hali ya kutotenda iliyo kama kifo, wakaanza maisha ya utendaji wa kujibidiisha sana katika “nchi” yao, yale makao yao ya utendaji wa kiroho waliyopewa na Mungu. (Ufunuo 11:8-12) Kufikia miezi ya mwishoni mwa mwaka wa 1919, hata walitangaza kuchapishwa kwa gazeti jipya la kukamilishana na Mnara wa Mlinzi. Kichapo hicho kipya kiliitwa The Golden Age (sasa Amkeni!), na kilikuwa ushuhuda wa kwamba watu wa Mungu wametiwa nguvu mpya, wakiwa wamepangwa tena kuwa tengenezo kwa ajili ya utumishi.
17. Yehova anawahakikishiaje watu wake kwamba hakuna cha kumzuia asitimize kusudi lake kuhusiana na Israeli wa kiroho?
17 Katika ulimwengu mzima hakuna nguvu yoyote ambayo ingeweza kuzuia uzaliwa huo mpya. Mstari unaofuata unasema lilo hilo: “Je! mimi nilete wana karibu na kuzaliwa, nisizalishe? asema BWANA; mimi nizalishaye, je! nilifunge tumbo? asema Mungu wako.” (Isaya 66:9) Sawa na vile hatua za kuzaa mtoto zisivyoweza kuepukwa zikiisha kuanza, ndivyo kuzaliwa upya kwa Israeli wa kiroho hakungeweza kuzuiliwa baada ya kuanza. Ni kweli kwamba upinzani ulikuwako, na yaelekea kwamba kutakuwako upinzani zaidi wakati ujao. Lakini ni Yehova peke yake aliye na uwezo wa kukomesha kitu anachokianzisha. Hata hivyo, yeye hafanyi hivyo kamwe! Ingawa hivyo, Yehova anawatendeaje watu wake waliotiwa nguvu mpya?
-
-
Yehova Hubariki Ibada SafiUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
c Uzaliwa unaotajwa hapa kwa njia ya unabii sio ule ule unaoelezwa kwenye Ufunuo 12:1, 2, 5. Katika sura hiyo ya Ufunuo, “mwana, wa kiume,” anafananisha Ufalme wa Kimesiya, ulioanza kazi mwaka wa 1914. Hata hivyo, “mwanamke” wa unabii anayetajwa katika maandiko hayo mawili ni yule yule.
-
-
Yehova Hubariki Ibada SafiUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Utunzaji Mwororo wa Yehova
18, 19. (a) Yehova anatumia mfano gani wenye kugusa moyo, nao unatumikaje kuwahusu watu wake walio uhamishoni? (b) Leo mabaki watiwa-mafuta wamefaidikaje na lishe na utunzaji wenye upendo?
18 Mistari minne inayofuata inaufafanua utunzaji mwororo wa Yehova kwa njia ya kuvutia. Kwanza, Isaya anasema hivi: “Furahini pamoja na Yerusalemu, shangilieni kwa ajili yake, ninyi nyote mmpendao; furahini pamoja naye kwa furaha, ninyi nyote mliao kwa ajili yake; mpate kunyonya, na kushibishwa kwa maziwa ya faraja zake, mpate kukama, na kufurahiwa kwa wingi wa utukufu wake.” (Isaya 66:10, 11) Hapa Yehova anatumia mfano wa mwanamke anayenyonyesha kitoto chake kichanga. Mtoto mchanga anapoumwa na njaa, kazi yake ni kulia-lia tu. Lakini anapoletwa karibu na matiti ya mama yake anyonye, sasa yeye huacha kihoro chake na kutosheka akiwa na furaha kamili.
-
-
Yehova Hubariki Ibada SafiUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
19 Israeli wa kiroho pia alibarikiwa kwa lishe tele baada ya kurudishwa mwaka wa 1919. Tangu wakati huo, chakula cha kiroho kinachotolewa kupitia “mtumwa mwaminifu na mwenye busara” kimekuwa kikitiririka kwa ukawaida. (Mathayo 24:45-47) Kweli huu umekuwa wakati wa faraja na shangwe kwa mabaki watiwa-mafuta. Lakini kumekuwako na baraka nyingine nyingi.
-